Skip to main content

UCHUMBA NA MAHUSIANO

                                     MAANA YA UCHUMBA

Ingawa neno “uchumba” halipatikani katika Bibilia, tumepewa kanuni kwamba Wakristo wanastahili kupitia kabla ya ndoa. Kanuni ya kwanza ni kwamba ni lazima tutafautishe mtazamo wa dunia kuhusu uchumba kwa sababu mtazamo wa Mungu wahitilafiana na ule wa dunia (2 Petero 2:20). Huku ikiwa mtazamo wa dunia juu ya uchumba huenda usiwe na jinsi tunavyo taka, cha muimu ni kutambua tabia ya mtu kabla tufanye ahadi naye. Lazima tujue ikiwa huyu mtu ameokoka katika roho wa kristo (Yohana 3:3-8) na kama huyo mtu ako na nia ile kama ya kristo (Wafilipi 2:5). Lengo kuu la uchumba ni kumtafuta mpenzi wa maisha. Bibilia inatuambia kwamba, kama Wakristo tusioe wasio Wakristo (2 Wakorintho 6:14-15) kwa sababu hii itafanya uhusiano wetu na Kristo na tuaibishe tabia zetu na kanuni zetu ziwe hafifu.

Wakati mtu amejitoa kw uhusiano, hata kama ni wa uchumba, ni muimu kukumbuka kumpenda Mungu kuliko vitu vyote (Mathayo 10:37). Kusema au kuamini kuwa mtu mwingine ni “vitu vyote” au kitu cha maana katika maisha ni kuabudu sanamu, ambayo ni dhambi (Wagalatia 5:20; Wakolosai 3:5). Pia hatustahili kuichafua miili yetu kwa kufanya usherati (1 Wakorontho 6:9, 13; 2 Timotheo 2:22). Dhambi ya usherati sio dhambi kwa mwili pekee bali ni kinyume na Mungu (1 Wakorintho 6:18). Ni muimu kuwaeshimu na kuwachukulia kuwa watu wa heshima vile tunavyojipenda wenyewe (Warumi 12:9-10). Na hii ni kweli kwa uhusiano wa uchumba. Hata kama mnachumbiana, kuifuata kanuni hii ndio njia nzuri kuwa na msingi salama wa ndoa. Mojawapo ya maamuzi tutakayofanya, kwa sababu wakati watu wawili wanaoana, hushikana na kuwa mwili mmoja kwa uhusiano ambao Mungu anaunuia uwe wa kudumu na usiovunjika (Mwanzo 2:24; Mathayo 19:5).

English

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....