“Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; nao waupendao watakula matunda yake.” (Mith.18:21) Naomba kuwasilisha ujumbe maalum kuhusu matumizi ya vinywa vyetu kwa nia ya kujifunza faida na athari zake. Ni muhimu kutambua ya kwamba maneno yatokayo katika vinywa vyetu ya nguvu. Maneno mazuri yana “nguvu za uumbaji” na maneno mabaya ni kama “silaha za maangamizi”. Maandiko tuliyosoma hapa juu yanatujulisha jinsi ambavyo, nguvu za ulimi zimebeba mauti na uzima. Hebu tujihoji kwa kifupi hapa. Hivi kweli maneno yanayotoka vinywani mwetu yanazalisha matunda gani? Je! tunatumia maneno ya ndimi zetu kujenga au kuangamiza wengine? Maneno yatokayo vinywani mwetu ni ya namna gani? Yamejaa sumu ya chuki au ladha ya upendo? Yamejaa sumu ya uchungu au dawa ya baraka? Ni maneno ya lawama au kutia moyo? Ni maneno yanayotabiri ushindi au kushindwa? Maneno ni kama vifaa vya matumizi ya kutusaidia kufikia malengo ya kimaendeleo au kushusha moyo na kusababisha mkandamizo wa moyo na msongo wa mawa...
Karibu tuzungumze hapa ndipo kituo chako bora cha maarifa ,karibu useme, niseme, waseme na sisi tunasema 2018. ni sehemu pekee ya kila mmoja kutoa maoni yake na uwelewa wake juu ya kuelimisha jamii. ukiwa unachochote cha kutaka kutushirikisha kupitia jukwaa hili la wana jamii, usisite kututumia baraua pepe kwenda kwa bahatimagweiga467@gmail.com au wasiliana nasi kwa simu namba 0757472165, 0659991953. huduma zetu ni masaa 24