Skip to main content

Posts

Showing posts from December 10, 2018

WANAWAKE WENGI HUFUNGA NA KUOMBA WANAUME WA NAMNA HII.

Ndugu zangu, nimeongea kuhusu baraka na heri ya kuwa na mwanamke wa pekee pia ni vizuri kwa wakina dada na wanawake kutambua kuwa nao wanatamani sana kuwa na mume wa namna hii. Hii pia ni namna moja ya sisi wanaume kujidai katika ndoa zetu. Mke huyu ana heri anapompata mume wa namna hii: 1️⃣ Mume anayemjua Mungu na anaishi maisha ya kumpendaza Mungu. 2️⃣ Mume anayetambua kuwa yeye ni baba wa familia, mume wa ndoa na mlinzi wa familia. 3️⃣ Mume anayejua kuwa mke wake anatakiwa kusikiliza na siyo kukaripia na kugombezwa kama mtoto na wakati mwengine kutamkiwa maneno makali mbele ya watoto. 4️⃣ Mume ambaye ana uwezo wa kujishusa pale anapofanya kosa, anapoumiza hisia za mke wake. 5️⃣ Mume ambaye anatambua ulimwengu wa mwanamke na anatambua mahitaji ya mke wake. 6️⃣ Mume ambaye anashirikisha mambo ya familia na ndoa kwa mke wake na wanapanga mipango mbalimbali ya familia kwa pamoja. 7️⃣ Mume ambaye anatambua kuwa ni wajibu wake kuwa na muda wa pekee wa kuwa na mke wake, kama vile ...
Kila hatua utakayopiga kwenye maisha yako lazima itakuwa na watu wa kuzungumza juu ya hatua zako. kwa maana nyingine tunasema kwamba kadiri unavyojitahidi kufanikiwa ndivyo unaongeza kiwango cha madui kwenye maisha yako. ila idadi yao haina madhara kwako kama utaamua kupuuza kile ambacho wanakisema juu yako. wapo wengine ambao hata kama ni watu wako wa karibu lazima watajinua kuyazungumzia maendeleo yako.haijarishi umekuwa ukiwasaidia kwa kiasi gani au unawasaidia kwa kiwango gani bado hahao watakugeukia na kuwa na kuwa mwiba kwenye maendeleo yako. kinachohitajika hapo ni kuwapuza na kutofanyia kazi yale ambayo unaamini kwamba yatakuwa na matokeo hasi kwenye maisah yako binafsi. endelea kuamini kuwa mabadiliko yako yapo mikononi mwako kwa sababu tunasema kijana mpumbavu atayavunja maisha yake kwa akili zake mwenyewe. jikite zaidi kwenye kutafuta mabadiliko juu ya malengo yako na mipango yako . wanadamu siku zote wema wao huwa haupo katika yale ambayo umejitoa kwa ajili yao bali we...