Skip to main content

Posts

Showing posts from July 19, 2018

NGUVU ZA VITA YA KIMAWAZO

Leo ningependa tuangalie kidogo kuhusu vita ya kimawazo Siku moja nikiwa nimelala, naliota ufalme wa Mungu na ule wa Shetani upo katika vita. Kila upande ulikuwa unafanya bidii kuhakikisha mawazo/matakwa yake yanatekelezwa kupitia mtu. Naam niliota kuna kitu Mungu anataka kizaliwe duniani kupitia mtu na Shetani naye akawa akipinga kile cha Mungu kwa kuleta cha kwake kizaliwe kupitia mtu huyo huyo. Baada ya kutafakari ndoto ile ndipo nikapata ujumbe huu, sasa endelea kujifunza. Kwanza ni vizuri ukafahamu kwamba, ikiwa Mungu ana mawazo ya amani juu yako(Yeremia 29:11), basi, Shetani pia ana mawazo ya uharibifu juu yako. Na hii ina maana kila siku mwanadamu atakutana na vita ya nini atekeleze katika ufahamu wake, naam hii ndiyo vita ya mawazo. Mungu atapigana kuhakikisha mawazo yake juu yako yanafanikiwa na Shetani naye atapigana kuhakikisha mawazo yake kupitia wewe yanafanikiwa. Kumbuka kwamba Mungu anapotaka kufanya jambo lolote chini ya jua anatumia njia ya kuweka wazo ndani y...

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...