Skip to main content

Posts

Showing posts from July 23, 2018

MANENO YA LEO NA TUJENGANE MEDIA 2018

Katika maisha unapaswa kukubaliana na mapungufu amabayo unayo katika nyakati amabazo unapiatia kwenye maisha yako. Wapo watu mbalimbali ambao wanakumbana na changamoto nyingi sana katka maisha yao kutokana na kushindwa kukubaliana na mpungufu ama yake binafsi au ya watu wanao mzunguka. Jifunze kuwa mwepesi wa kukubaliana na vitu kama hivyo kwenye maisha yako na baada ya hapo uchukue hatua mapema kukabiliana na hiyo hali. Kuendelea kulaumu hakukupi wewe daraja la kuvukia kuelekea kwenye nafasi ya wateule wanaokubali kushindana na changamoto katika maisha yao na sio kusindwa kizembe na chanagamoto. Ikunbukwe kwamba mtu pekee mwenye dhamana ya kunusuru malengo yako ni wewe mwenyewe. Unapaswa kujibidisha katika kufikiria mambo yalio chanya na kuachana na vitu hasi kama vile kuendelea kushindana na watu ambao wana mapungufu yalio kinyume kabisa na mlengo yako. Jijengee mfumo wa kusamehe, kuikubali na kukbaliana na mapungufu yako pamoja na mapungufu ya wenzio, jisamehe mwenyewe pale ...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

MAMBO YANAYOVUNJA UHUSIANO KATIKA MAPENZI NA NDOA ZETU

HAYA NDIO MAMBO MAKUU YANAYOVUNJA UHUSIANO WETU NA WEZI WETU. 1. Kutokuwa na mawasiliano ya karibu na mwenzi wako. 2. Kutojali maumivu ya mwenzi wako. 3. Ubishi usiokuwa na maana. 4. Kupenda kujihesabia haki. 5. Kutokubali makosa. 6. Kutokuwa na roho ya msamaha. 7. Kutokuwa muwazi kwa mwenzi wako. 8. Usaliti wa mapenzi. 9. Kuigiza kupenda. 10. Kutomheshimu mwenzi wako. 11. Kuwa mjuaji kila kitu unajifanya unajua. 12. Kutokutambua uthamani wa mwenzi wako katika maisha yako. 13. Kuwa na jeuri. 14. Kutokuwa na kifua cha kuficha mambo ya nyumbani. [chumbani] 15. Kuto kujali watu wa nyumbani kwako [ndugu,watoto n.k] 16. Kujiamulia kufanya vitu bila ushauri wa pamoja. 17. Kutokuwa na faraja na mwenzi wako [kutokujua jinsi ya kumfariji mwenzi wako] 18. Kutomridhisha mwenzi wako kimapenzi. 19. Kuwa na amri kwa mwenzi wako hata kwa mambo yasiyokuwa na maana au malengo katika                maisha yenu. 20. Ugomvi wa muda mrefu usiok...