Skip to main content

Posts

Showing posts from December 4, 2018

HAKUNA NDOA ILIYOKAMILIKA ASILIMIA 1000%

Nataka kukuambia kuwa hakuna ndoa iliyo kamili yaani perfect, na kama kuna mtu Anakwambia kuwa ndoa yake ipo perfect ujue huyo ni muongo mkubwa vinginevyo kama hao watu waliooana ni mazombi kwa maana nyingine siyo Binadamu, hata kama ni ya mchungaji wako, shehe wako au hata askofu wako wa jimbo . hata hao mnaoona wanatupia mapicha picha na wake zao au waume zao kuonyesha kuwa wapo happy Haimaanishi kuwa ndio Muda wote asubuhi mpaka jioni,jumatatu mpaka jumapili, January mpaka December wao ni kucheka tu  hapana kiasi Kwamba ukaona kuwa ndoa yako haifai kabisa au upo kwenye Shimo, Kwenye ndoa watu kuna kukwazana, kupishana, hata kugombana kabisa wakati mwingine lakini  kikubwa tunachotofautiana wengi ni namna ya kushughulikia hayo matatizo yanapojitokeza na kuishia kuharibu ndoa zetu wenyewe Katikati ya ndoa yenu nani mumemweka kama mhimili wenu ni Mungu au nani,? Wanaume kujaa ufahari kuwa mimi mwanaume Bwana siwezi omba msamaha, wanawake na wao husema Kwamba atanionaje ...

HII NI MAALUMU KWA WANAUME

Wanaume wengi wanafikilia kuwa mwanamke anachohitaji kwenye maisha ni hela, magari na mijizawadi ya kumdanganyia,  lakini ukweli ni kwamba mwanamke sahihi kwako au mke wako hahitaji hivyo vyote kwani kwake hivyo ni matokeo tu katika maisha ila anachojali zaidi ni Muda wako kwake, upendo wako kwake, Kujali kwako, ukweli wako kwake, uaminifu wako kwako,  na Tabasamu, na wewe kumfanya yeye ndio kipaumbele chako na zaidi ya vyote uwe na hofu ya Mungu. Hela, magari na zawadi ni Kazi bure kama hivyo vyote vingine havioni ndani ya Nyumba kwa kuwa kwako hajafata hivyo wengine hata kwao hela zilikuwepo na hata pia hayo magari yalikuwepo na bado yapo, na walikuwa wanavitumia ila kwako kuna vya ziada alivyofata ambavyo ni muhimu zaidi kuliko hayo magari na hela. Zingatia sana kujali familia yako kwani upendo wako ni wa thamani sana kwao Kumbuka ndoa yoyote Iliyodumu au mahusiano yoyote yaliyodumu maana yake kuna mmoja Kati yao Alikuwa anajishusha, Walikuwa wanasameheana pale walipokose...

EPUKA KUJIAMINISHA JUU YA KILE AMBACHO UMEHIDIWA

asilimia kubwa yatu tupenda kujiwekea uhakika wa  kile ambacho wanakitarajia kutoka kwa watu wengine lakini kila siku nimekuwa nikisema jambo hili kwenye makala zangu za kila siku kuwa jambo hilo limewatesa wengi sana hasa pale wanapokuwa wameshindwa kupata msaada juu ya kile ambacho walitarajia. kwa mfano kuna watu wanatumia pesa vibaya kwa sababu tu kuna sehemu wameahidiwa kuwa watapata kiwango chochote cha fedha kitakachowasaidia kutimiza yale ambayo wangependa yatimie katika mipango yao. hatima ya kujiaminisha siku zote ni fedheha kwni mambo yanabadilika na maisha ya watu yanabadilika pia. kwa hiyo unashauriwa kuwa na uhakika na kile ambacho unacho mkononi kwako na siyo kilichopo kwa mtu mwingine. haijarishi ni ndugu yako , jamaa yako, rafiki nk . epuka sana kuamini kauli zao juun ya upande wa fedha ama mambo ambayo unaona kabisa wamba kutimia  kwako ni vigum .