Skip to main content

NUKUU YA LEO . 9/12/2018

Kuwa na Elimu kubwa haina maana kwamba unafahamu mambo yote katika ulimwengu tunamoishi.  Asilimia kubwa ya watu wamepotea kimaisha kutokana na falsafa hasi ya kwamba wapo sahihi muda wote kwa sababu tu ya Kiwango cha Elimu alichopata darasani.  Kwa ukweli usiopingika ni kwamba umehitimu Elimu ya darasani ila bado upo wazi au mweupe kabisa kwenye Elimu ya mtaani yani Elimu inayotumika zaidi kwenye maisha.  Elimu ya darasani itakusaidia kwa uchache sana kufanikisha mambo yako ila elimu ya mtaani itakuwezesha zaidi kutimiza ndoto zako kimaisha.  Kwa mfano kuna watu wamesoma na wana elimu kubwa ila bado Elimu hiyo waliopata darasani inazidi kuwatenga mbali na jamii inayowazunguka kwa kushindwa kuchanganua mambo kwa wakati.
Itikadi hii inatokana na kuaminishawa kwamba sehemu pekee itakayo kusaidia wewe kumaliza matatizo yako ni darasani.  Ila ukweli usiopingika ni kwamba darasani pekee hakutoshi kumaliza matatizo yako.  Ispokuwa hata njee ya darasani yani hekima binafsi ya kuzaliwa nayo inawezekana.
Uchunguzi umebaini rasimi kwamba kuna badhi ya watu wana uwezo wa Elimu ya kawaida lakini uchanganuzi wao wa mambo ni mkubwa sana kutokana na matumizi ya hekima waliozaliwa nayo.
Wakati mwingine watu hao wamefanya mambo makubwa sana katika ulimwengu wa mafanikio.

Imeandaliwa na bahati magweiga
Simu namba 0757472165
     Tigo namba 0659991953
E-mail bahatimagweiga467@gmail.com

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....