Skip to main content

NGUVU ZA VITA YA KIMAWAZO


Leo ningependa tuangalie kidogo kuhusu vita ya kimawazo
Siku moja nikiwa nimelala, naliota ufalme wa Mungu na ule wa Shetani upo katika vita. Kila upande ulikuwa unafanya bidii kuhakikisha mawazo/matakwa yake yanatekelezwa kupitia mtu. Naam niliota kuna kitu Mungu anataka kizaliwe duniani kupitia mtu na Shetani naye akawa akipinga kile cha Mungu kwa kuleta cha kwake kizaliwe kupitia mtu huyo huyo. Baada ya kutafakari ndoto ile ndipo nikapata ujumbe huu, sasa endelea kujifunza.
Kwanza ni vizuri ukafahamu kwamba, ikiwa Mungu ana mawazo ya amani juu yako(Yeremia 29:11), basi, Shetani pia ana mawazo ya uharibifu juu yako. Na hii ina maana kila siku mwanadamu atakutana na vita ya nini atekeleze katika ufahamu wake, naam hii ndiyo vita ya mawazo. Mungu atapigana kuhakikisha mawazo yake juu yako yanafanikiwa na Shetani naye atapigana kuhakikisha mawazo yake kupitia wewe yanafanikiwa.
Kumbuka kwamba Mungu anapotaka kufanya jambo lolote chini ya jua anatumia njia ya kuweka wazo ndani ya mtu. Wakati huo huo Shetani naye akijua kwamba  wazo la Mungu litaleta uharibifu kwenye ufalme wake, atahakikisha analeta wazo lake, kwa lengo la kuondoa wazo la Mungu ndani yako,  ili kuleta uharibifu kwenye ufalme wa Mungu.
Jambo hili ndilo lilitokea kwa Adam na Eva pale bustanini, Shetani alipoleta wazo la uharibifu kwenye ufahamu wa Eva na kisha Eva akakubaliana na lile wazo la uharibifu, akawa ameharibu mpango wa Mungu juu ya maisha yao. Naam nafsi/akili ya mtu ni kiungo au uwanja wa vita vya mawazo ya upande wa Mungu na upande wa Shetani.
Kumbuka kwamba Vita vya kiroho, ni vita ambayo inapigwa katika ulimwengu wa roho, kwa jinsi ya rohoni baina ya ufalme wa Mungu na wa Shetani kupitia watendaji wao kwa lengo la kumpata mwanadamu, ili kila ufalme umtumie kutekeleza au kufanikisha makusudi yake ya ulimwengu wa roho kwenye ulimwengu wa mwili ambao mwanadamu mwenye mwili wa damu na nyama anaishi.
Vita vya kiroho ni kile ambacho mimi nakiita vita ya matakwa (a war of wills). Kila ufalme katika ulimwengu wa roho, una mambo yake ambayo unataka kuhakikisha yanatimia katika ulimwengu wa mwili, naam ulimwengu ambao roho yenye mwili ndio inayotawala. Viumbe walioko kwenye ulimwengu wa roho hawana mwili wa damu na nyama kama vile sisi tulivyo. Kwa hiyo wanapotaka kutawala kwenye ulimwengu huu, hawana namna ya kufanya zaidi ya kumtumia mwanadamu.
Kwa hiyo mwanadamu anakuwa kiungo muhimu sana kati ya ulimwengu wa roho na huu wa mwili. Na kwa sababu hiyo kila ufalme unafanya jitihada ya kuhakikisha unachukua utawala kwenye nafsi ya mwanadamu ili umtumie kwa kazi yake hapa duniani. Naam huo ndio mwanzo wa vita vya kiroho kati ya Mungu na Shetani, nia yao ikiwa ni kuhakikisha matakwa yao yanafanikiwa kupitia mtu. Na ndio maana, kwa Mungu, mtu ni wa muhimu sana (Zaburi 8:4-8).
Na kwa sababu hii unapaswa kuwa makini kwa habari ya nini unairuhusu nafsi yako ikitafakari, ukijua kwamba vita kubwa ya Mungu na Shetani ni kuwa na utwala wa nafsi yako ili kuongoza mawazo yako na maamuzi yako. Fahamu kwamba Mungu akiongoza nafsi yako ataongoza maamuzi yako pia. Vivyo Shetani akikamata nafsi yako amekamata maamuzi yako na future yako. Hivyo hakikisha unaenenda kwa roho na kuyatafakari mambo ya rohoni ili kuyafanya mapenzi ya Mungu ukikumbuka kwamba siku zote yeye anakuwazia mawazo ya amani. 
Bwana Mungu akubariki na akupe ushindi katika kila vita ya mawazo unayoikabili.
Advertisements

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YANAYO KWAMISHA UFUGAJI

MAGWEIGA POULTRY INVESTMENT(wajasiriamali wa kuku na bidhaa zake) MAMBO YANAYOKWAMISHA WAFUGAJI WENGI.  Ufugaji ni rahisi ukitumia faida za mezani na kushuhudia watu wanafanya.  Hali hi inaweza ikawa tofauti ukianza wewe mwenyewe kwa vitendo.  Ni jambo gumu kiasi chake endapo mfugaji atapuza kanuni bora za Ufugaji.  Hapa mfugaji mpya anapaswa kujitathimini na kujipima kama anaweza kutoboa na kufikia matamanio yake kiufugaji.     Ufugaji ni kazi ngumu lakni imejawa na mafanikio kabambe na pia ni miongoni mwa furusa ambazo zipo wazi.  Ila vigezo na mashariti kuzingatiwa. kinacho kwamisha ufugaji kwa asilimia kubwa ni mambo yafuatayo . Mfugaji asipo yavalia njuga ataishia kwenye msongo wa mawazo na kujipa magonjwa ya moyo. Magweiga poultry investment 1. Magonjwa . Kipengele hiki kimekuwa changamoto kubwa sana kwa sisi wafugaji.  Yapo magonjwa changizwa  ambayo ni mfugaji mwenyewe anakubaliana na ugonjwa husika kutokea  ✔️ Typhoid...

KUWA NA MSIMAMO KWENYE MAISHA YAKO

Ulishawahi kujiuliza ni  kwanini watu wachache wanafanikiwa katika maisha huku wengi wakibakia masikini?  Ukweli ni kwamba sio kuwa wao wanasiri nyingi za kufanikiwa kuliko wewe bali ni misimamo thabiti waliojiwekea ili kuendana na ukuaji wa changamoto za maisha. Ni watu ambao wanafikiria vitu na mambo makubwa na kufanya vitu hivyo kwa msimamo bila kukubali kushindwa.  James William  (Harvard University ) aliwahi kusema kwamba " A human being can alter their lives by altering their attitude of mind" akiwa anamanisha kwamba binadamu yeyote anaweza kupunguza maisha yake kwa kupunguza musimamo wa fikira zake. Duniani kote utafiti unaonyesha kwamba rasirimali watu ndio nyenzo muhimu sana katika biashara yoyote yenye mulengo wa mafanikio.  Ila rasilimali hiyo ndio imekuwa ikipotea kila siku kutokana na watu kukoswa msimamo  (atttitude) Watu wanaweza kuwa asset kubwa sana katika maisha yako. Mafanikio yoyote hayapimwi kwa kipato ulichonacho bali pia ...

USIWE NA TAMAA KATIKA UFUGAJI.

  MADHARA YA TAMAA KATIKA UFUGAJI  Mfugaji yoyote ili aweze kuona faida ya ufugaji wake lazima aweke Tamaa pembeni.  Kuna utofauti kati ya Mfugaji mwenye Malengo na Mfugaji mwenye Tamaa.  Mfugaji mwenye Malengo hufanya muradi wake kwa uchache na kwa ufanisi, pia huweka ukomo wa kumiliki kuku kwa kiwango ambacho huweza kuwamudu na kumletea faida  Mfugaji mwenye Tamaa yeye kwake ukienda utakuta ana kuku 500 wa rika tofauti tofauti ambao hata kuwalisha ni mtihani kwake ila shida yake aonekane anamiliki kuku wengi japo faida yake ni 0%% Mfano : umeweka kuku 100 kroila  na umewakuza kwa shida hadi kufikia kutaga . Wanapoanza kutaga ni muda wa kuvuna mayai ili kurudisha garama zako.  Cha ajabu hapa utakuta Mfugaji anakurupuka kuingiza vifaranga wapya 200 kwa kutegemea hawa kuku 100 wahudumie vifaranga 200  hadi kufikia kutaga.   Pia hao kuku 100 wajiendeshe wao wenyewe kupitia mayai.  pia kuku 100 wahudumie familia. Ukweli ni kwamba itafi...