Skip to main content

NGUVU ZA VITA YA KIMAWAZO


Leo ningependa tuangalie kidogo kuhusu vita ya kimawazo
Siku moja nikiwa nimelala, naliota ufalme wa Mungu na ule wa Shetani upo katika vita. Kila upande ulikuwa unafanya bidii kuhakikisha mawazo/matakwa yake yanatekelezwa kupitia mtu. Naam niliota kuna kitu Mungu anataka kizaliwe duniani kupitia mtu na Shetani naye akawa akipinga kile cha Mungu kwa kuleta cha kwake kizaliwe kupitia mtu huyo huyo. Baada ya kutafakari ndoto ile ndipo nikapata ujumbe huu, sasa endelea kujifunza.
Kwanza ni vizuri ukafahamu kwamba, ikiwa Mungu ana mawazo ya amani juu yako(Yeremia 29:11), basi, Shetani pia ana mawazo ya uharibifu juu yako. Na hii ina maana kila siku mwanadamu atakutana na vita ya nini atekeleze katika ufahamu wake, naam hii ndiyo vita ya mawazo. Mungu atapigana kuhakikisha mawazo yake juu yako yanafanikiwa na Shetani naye atapigana kuhakikisha mawazo yake kupitia wewe yanafanikiwa.
Kumbuka kwamba Mungu anapotaka kufanya jambo lolote chini ya jua anatumia njia ya kuweka wazo ndani ya mtu. Wakati huo huo Shetani naye akijua kwamba  wazo la Mungu litaleta uharibifu kwenye ufalme wake, atahakikisha analeta wazo lake, kwa lengo la kuondoa wazo la Mungu ndani yako,  ili kuleta uharibifu kwenye ufalme wa Mungu.
Jambo hili ndilo lilitokea kwa Adam na Eva pale bustanini, Shetani alipoleta wazo la uharibifu kwenye ufahamu wa Eva na kisha Eva akakubaliana na lile wazo la uharibifu, akawa ameharibu mpango wa Mungu juu ya maisha yao. Naam nafsi/akili ya mtu ni kiungo au uwanja wa vita vya mawazo ya upande wa Mungu na upande wa Shetani.
Kumbuka kwamba Vita vya kiroho, ni vita ambayo inapigwa katika ulimwengu wa roho, kwa jinsi ya rohoni baina ya ufalme wa Mungu na wa Shetani kupitia watendaji wao kwa lengo la kumpata mwanadamu, ili kila ufalme umtumie kutekeleza au kufanikisha makusudi yake ya ulimwengu wa roho kwenye ulimwengu wa mwili ambao mwanadamu mwenye mwili wa damu na nyama anaishi.
Vita vya kiroho ni kile ambacho mimi nakiita vita ya matakwa (a war of wills). Kila ufalme katika ulimwengu wa roho, una mambo yake ambayo unataka kuhakikisha yanatimia katika ulimwengu wa mwili, naam ulimwengu ambao roho yenye mwili ndio inayotawala. Viumbe walioko kwenye ulimwengu wa roho hawana mwili wa damu na nyama kama vile sisi tulivyo. Kwa hiyo wanapotaka kutawala kwenye ulimwengu huu, hawana namna ya kufanya zaidi ya kumtumia mwanadamu.
Kwa hiyo mwanadamu anakuwa kiungo muhimu sana kati ya ulimwengu wa roho na huu wa mwili. Na kwa sababu hiyo kila ufalme unafanya jitihada ya kuhakikisha unachukua utawala kwenye nafsi ya mwanadamu ili umtumie kwa kazi yake hapa duniani. Naam huo ndio mwanzo wa vita vya kiroho kati ya Mungu na Shetani, nia yao ikiwa ni kuhakikisha matakwa yao yanafanikiwa kupitia mtu. Na ndio maana, kwa Mungu, mtu ni wa muhimu sana (Zaburi 8:4-8).
Na kwa sababu hii unapaswa kuwa makini kwa habari ya nini unairuhusu nafsi yako ikitafakari, ukijua kwamba vita kubwa ya Mungu na Shetani ni kuwa na utwala wa nafsi yako ili kuongoza mawazo yako na maamuzi yako. Fahamu kwamba Mungu akiongoza nafsi yako ataongoza maamuzi yako pia. Vivyo Shetani akikamata nafsi yako amekamata maamuzi yako na future yako. Hivyo hakikisha unaenenda kwa roho na kuyatafakari mambo ya rohoni ili kuyafanya mapenzi ya Mungu ukikumbuka kwamba siku zote yeye anakuwazia mawazo ya amani. 
Bwana Mungu akubariki na akupe ushindi katika kila vita ya mawazo unayoikabili.
Advertisements

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....