Katika maisha unapaswa kukubaliana na mapungufu
amabayo unayo katika nyakati amabazo unapiatia kwenye maisha yako. Wapo watu
mbalimbali ambao wanakumbana na changamoto nyingi sana katka maisha yao
kutokana na kushindwa kukubaliana na mpungufu ama yake binafsi au ya watu wanao
mzunguka. Jifunze kuwa mwepesi wa kukubaliana na vitu kama hivyo kwenye maisha
yako na baada ya hapo uchukue hatua mapema kukabiliana na hiyo hali. Kuendelea kulaumu
hakukupi wewe daraja la kuvukia kuelekea kwenye nafasi ya wateule wanaokubali
kushindana na changamoto katika maisha yao na sio kusindwa kizembe na
chanagamoto.
Ikunbukwe kwamba mtu pekee mwenye dhamana ya kunusuru
malengo yako ni wewe mwenyewe. Unapaswa kujibidisha katika kufikiria mambo
yalio chanya na kuachana na vitu hasi kama vile kuendelea kushindana na watu
ambao wana mapungufu yalio kinyume kabisa na mlengo yako.
Jijengee mfumo wa kusamehe, kuikubali na kukbaliana na
mapungufu yako pamoja na mapungufu ya wenzio, jisamehe mwenyewe pale unapokuwa
umekosea kwa sababu huwa tunasema kwamba hakuna mwanadamu aliye kamilika katika
maisha yake. Kadili unavyozidi kuwaza mabaya uliokwisha kuyafanya huko nyuma
ndivyo Dhahiri unazidi kujipunguzia utimizaji wa malengo yako.
Unapaswa kuamini kwamba yakale yote yamekwisaha kupita
na sasa umefanyika kiumbe kipya na umesamehewa dhambi zako zote.
MSINGI WA MANENO HAYA
1. Wekeza katika leo yako ili uweze kuitazamia kesho
iliyo njema
2. Epuka kuwa mwepesi wa kugairi mambo yako pasipo sababu
maalum
3. Chunga sana maneno ya ulimi wako yanaweza kuwa kikwazo
kwako
4. Lazimika kusamehe ili kuipa nafasi nafsi kuwaza mema
kwa ajili yako
5. Usiwe mugumu wa kukubaliana na mapungufu yako na yaw
wenzio
6. Jenga utamaduni wa kujiheshimu mwenyewe kabla ya kudai
heshima
7. Chagua kujifunza vitu vipya amabavyo vitakuwa muhimu
kwako.
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza