Skip to main content

MANENO YA LEO NA TUJENGANE MEDIA 2018



Katika maisha unapaswa kukubaliana na mapungufu amabayo unayo katika nyakati amabazo unapiatia kwenye maisha yako. Wapo watu mbalimbali ambao wanakumbana na changamoto nyingi sana katka maisha yao kutokana na kushindwa kukubaliana na mpungufu ama yake binafsi au ya watu wanao mzunguka. Jifunze kuwa mwepesi wa kukubaliana na vitu kama hivyo kwenye maisha yako na baada ya hapo uchukue hatua mapema kukabiliana na hiyo hali. Kuendelea kulaumu hakukupi wewe daraja la kuvukia kuelekea kwenye nafasi ya wateule wanaokubali kushindana na changamoto katika maisha yao na sio kusindwa kizembe na chanagamoto.
Ikunbukwe kwamba mtu pekee mwenye dhamana ya kunusuru malengo yako ni wewe mwenyewe. Unapaswa kujibidisha katika kufikiria mambo yalio chanya na kuachana na vitu hasi kama vile kuendelea kushindana na watu ambao wana mapungufu yalio kinyume kabisa na mlengo yako.
Jijengee mfumo wa kusamehe, kuikubali na kukbaliana na mapungufu yako pamoja na mapungufu ya wenzio, jisamehe mwenyewe pale unapokuwa umekosea kwa sababu huwa tunasema kwamba hakuna mwanadamu aliye kamilika katika maisha yake. Kadili unavyozidi kuwaza mabaya uliokwisha kuyafanya huko nyuma ndivyo Dhahiri unazidi kujipunguzia utimizaji wa malengo yako.
Unapaswa kuamini kwamba yakale yote yamekwisaha kupita na sasa umefanyika kiumbe kipya na umesamehewa dhambi zako zote.
                 MSINGI WA MANENO HAYA
1.   Wekeza katika leo yako ili uweze kuitazamia kesho iliyo njema
2.   Epuka kuwa mwepesi wa kugairi mambo yako pasipo sababu maalum
3.   Chunga sana maneno ya ulimi wako yanaweza kuwa kikwazo kwako
4.   Lazimika kusamehe ili kuipa nafasi nafsi kuwaza mema kwa ajili yako
5.   Usiwe mugumu wa kukubaliana na mapungufu yako na yaw wenzio
6.   Jenga utamaduni wa kujiheshimu mwenyewe kabla ya kudai heshima
7.   Chagua kujifunza vitu vipya amabavyo vitakuwa muhimu kwako.

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....