Skip to main content

MANENO YA LEO NA TUJENGANE MEDIA 2018



Katika maisha unapaswa kukubaliana na mapungufu amabayo unayo katika nyakati amabazo unapiatia kwenye maisha yako. Wapo watu mbalimbali ambao wanakumbana na changamoto nyingi sana katka maisha yao kutokana na kushindwa kukubaliana na mpungufu ama yake binafsi au ya watu wanao mzunguka. Jifunze kuwa mwepesi wa kukubaliana na vitu kama hivyo kwenye maisha yako na baada ya hapo uchukue hatua mapema kukabiliana na hiyo hali. Kuendelea kulaumu hakukupi wewe daraja la kuvukia kuelekea kwenye nafasi ya wateule wanaokubali kushindana na changamoto katika maisha yao na sio kusindwa kizembe na chanagamoto.
Ikunbukwe kwamba mtu pekee mwenye dhamana ya kunusuru malengo yako ni wewe mwenyewe. Unapaswa kujibidisha katika kufikiria mambo yalio chanya na kuachana na vitu hasi kama vile kuendelea kushindana na watu ambao wana mapungufu yalio kinyume kabisa na mlengo yako.
Jijengee mfumo wa kusamehe, kuikubali na kukbaliana na mapungufu yako pamoja na mapungufu ya wenzio, jisamehe mwenyewe pale unapokuwa umekosea kwa sababu huwa tunasema kwamba hakuna mwanadamu aliye kamilika katika maisha yake. Kadili unavyozidi kuwaza mabaya uliokwisha kuyafanya huko nyuma ndivyo Dhahiri unazidi kujipunguzia utimizaji wa malengo yako.
Unapaswa kuamini kwamba yakale yote yamekwisaha kupita na sasa umefanyika kiumbe kipya na umesamehewa dhambi zako zote.
                 MSINGI WA MANENO HAYA
1.   Wekeza katika leo yako ili uweze kuitazamia kesho iliyo njema
2.   Epuka kuwa mwepesi wa kugairi mambo yako pasipo sababu maalum
3.   Chunga sana maneno ya ulimi wako yanaweza kuwa kikwazo kwako
4.   Lazimika kusamehe ili kuipa nafasi nafsi kuwaza mema kwa ajili yako
5.   Usiwe mugumu wa kukubaliana na mapungufu yako na yaw wenzio
6.   Jenga utamaduni wa kujiheshimu mwenyewe kabla ya kudai heshima
7.   Chagua kujifunza vitu vipya amabavyo vitakuwa muhimu kwako.

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YANAYO KWAMISHA UFUGAJI

MAGWEIGA POULTRY INVESTMENT(wajasiriamali wa kuku na bidhaa zake) MAMBO YANAYOKWAMISHA WAFUGAJI WENGI.  Ufugaji ni rahisi ukitumia faida za mezani na kushuhudia watu wanafanya.  Hali hi inaweza ikawa tofauti ukianza wewe mwenyewe kwa vitendo.  Ni jambo gumu kiasi chake endapo mfugaji atapuza kanuni bora za Ufugaji.  Hapa mfugaji mpya anapaswa kujitathimini na kujipima kama anaweza kutoboa na kufikia matamanio yake kiufugaji.     Ufugaji ni kazi ngumu lakni imejawa na mafanikio kabambe na pia ni miongoni mwa furusa ambazo zipo wazi.  Ila vigezo na mashariti kuzingatiwa. kinacho kwamisha ufugaji kwa asilimia kubwa ni mambo yafuatayo . Mfugaji asipo yavalia njuga ataishia kwenye msongo wa mawazo na kujipa magonjwa ya moyo. Magweiga poultry investment 1. Magonjwa . Kipengele hiki kimekuwa changamoto kubwa sana kwa sisi wafugaji.  Yapo magonjwa changizwa  ambayo ni mfugaji mwenyewe anakubaliana na ugonjwa husika kutokea  ✔️ Typhoid...

KUWA NA MSIMAMO KWENYE MAISHA YAKO

Ulishawahi kujiuliza ni  kwanini watu wachache wanafanikiwa katika maisha huku wengi wakibakia masikini?  Ukweli ni kwamba sio kuwa wao wanasiri nyingi za kufanikiwa kuliko wewe bali ni misimamo thabiti waliojiwekea ili kuendana na ukuaji wa changamoto za maisha. Ni watu ambao wanafikiria vitu na mambo makubwa na kufanya vitu hivyo kwa msimamo bila kukubali kushindwa.  James William  (Harvard University ) aliwahi kusema kwamba " A human being can alter their lives by altering their attitude of mind" akiwa anamanisha kwamba binadamu yeyote anaweza kupunguza maisha yake kwa kupunguza musimamo wa fikira zake. Duniani kote utafiti unaonyesha kwamba rasirimali watu ndio nyenzo muhimu sana katika biashara yoyote yenye mulengo wa mafanikio.  Ila rasilimali hiyo ndio imekuwa ikipotea kila siku kutokana na watu kukoswa msimamo  (atttitude) Watu wanaweza kuwa asset kubwa sana katika maisha yako. Mafanikio yoyote hayapimwi kwa kipato ulichonacho bali pia ...

USIWE NA TAMAA KATIKA UFUGAJI.

  MADHARA YA TAMAA KATIKA UFUGAJI  Mfugaji yoyote ili aweze kuona faida ya ufugaji wake lazima aweke Tamaa pembeni.  Kuna utofauti kati ya Mfugaji mwenye Malengo na Mfugaji mwenye Tamaa.  Mfugaji mwenye Malengo hufanya muradi wake kwa uchache na kwa ufanisi, pia huweka ukomo wa kumiliki kuku kwa kiwango ambacho huweza kuwamudu na kumletea faida  Mfugaji mwenye Tamaa yeye kwake ukienda utakuta ana kuku 500 wa rika tofauti tofauti ambao hata kuwalisha ni mtihani kwake ila shida yake aonekane anamiliki kuku wengi japo faida yake ni 0%% Mfano : umeweka kuku 100 kroila  na umewakuza kwa shida hadi kufikia kutaga . Wanapoanza kutaga ni muda wa kuvuna mayai ili kurudisha garama zako.  Cha ajabu hapa utakuta Mfugaji anakurupuka kuingiza vifaranga wapya 200 kwa kutegemea hawa kuku 100 wahudumie vifaranga 200  hadi kufikia kutaga.   Pia hao kuku 100 wajiendeshe wao wenyewe kupitia mayai.  pia kuku 100 wahudumie familia. Ukweli ni kwamba itafi...