Skip to main content

MANENO YA MUNGU NA TUJENGANE MEDIA

“Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; nao waupendao watakula matunda yake.” (Mith.18:21)
Naomba kuwasilisha ujumbe maalum kuhusu matumizi ya vinywa vyetu kwa nia ya kujifunza faida na athari zake. Ni muhimu kutambua ya kwamba maneno yatokayo katika vinywa vyetu ya nguvu. Maneno mazuri yana “nguvu za uumbaji” na maneno mabaya ni kama “silaha za maangamizi”.
Maandiko tuliyosoma hapa juu yanatujulisha jinsi ambavyo, nguvu za ulimi zimebeba mauti na uzima. Hebu tujihoji kwa kifupi hapa. Hivi kweli maneno yanayotoka vinywani mwetu yanazalisha matunda gani? Je! tunatumia maneno ya ndimi zetu kujenga au kuangamiza wengine?
Maneno yatokayo vinywani mwetu ni ya namna gani? Yamejaa sumu ya chuki au ladha ya upendo? Yamejaa sumu ya uchungu au dawa ya baraka? Ni maneno ya lawama au kutia moyo? Ni maneno yanayotabiri ushindi au kushindwa?
Maneno ni kama vifaa vya matumizi ya kutusaidia kufikia malengo ya kimaendeleo au kushusha moyo na kusababisha mkandamizo wa moyo na msongo wa mawazo.
WEMA NA UBAYA WETU HUJULIKANA KWA MANENO YETU
Kwa mujibu wa maneno ya Yesu, maneno ya vinywa vyetu ni akiba mbovu iliyomo katika mioyo yetu.
“Enyi wazao wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake. Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya.” (Matt.12:34-35)
Kifungu hiki kinatujulisha jinsi ambavyo ubaya wa mtu unathibitishwa na maneno ya kinywa chake. Huwezi kujitangaza kuwa mwema wakati kinywa chako kinatema sumu yenye kunajisi na kuharibu maisha ya wengine. Na mtu mwema hata kama sura yake sio ya kuvutia, lakini kwa maneno mema ya kinywa chake huutambulisha uzuri na wema wake.
Kiashiria cha mabadiliko ya kitabia kwa mtu aliyekutana na nguvu za wokovu wa Yesu Kristo, ni maneno yatokayo katika kinywa chake. Haiwezekani mtu mwenye kutangaza hadharani kuwa “ameokoka” au “amezaliwa upya” halafu bado akabaki na kinywa chenye kutema maneno yenye sumu iliyooza kama mpagani asiyemjua Mungu hata kidogo! Yesu anasema mtu wa jinsi hii bado ni wa “uzao wa nyoka”!
Kwa uzoefu wangu katika huduma za kiroho, dalili mojawapo ya mtu aliyejawa na pepo wachafu ni maneno yanayotoka kinywani mwake. Kumbuka ya kwamba, pepo wachafu ndio chimbuko la maneno machafu pia.
Ukijikuta kila mara unatokwa na maneno machafu hata kama hupendi kuyasema lakini yanakutoka tu bila kujizuia, hizo ni dalili za pepo wachafu ndani yako, na njia pekee ni maombezi ya kufunguliwa kwa pepo hao kukemewa kwa mamlaka ya jina la Yesu yatoke upate kuwa huru! Ubishi na kujihami kwingi kwa visingizo vya madai ya ujasiri wa kuonya na kukemea wengine sio leseni ya kutokwa na maneno machafu yaliyooza! “Two wrongs does not make one right”
MANENO YETU YANA ASILI YA UMILELE
Maneno yetu sio kwamba yana nguvu za kusababisha mauti au uzima katika dunia hii, bali hata katika ulimwengu ujao ambao ni wa milele.
“Basi, nawambia, kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu. Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.” (Matt.12:36-37)
Hivi ndivyo maneno tusemayo kila siku yalivyo na nguvu za umilele. Tutakutana nayo siku ya hukumu. Na hakuna hata mmoja wetu ambaye hatakutana na Mungu siku ya hukumu. Kiburi chetu ni kifupi mno huwa kinayeyuka ghafla tunapofikwa na mauti. Na hata wengine wanaodai hawaogopi kifo mawazo yao hubadilika ghafla pale kifo kinapowafika na wakati huo tayari wamechelewa kwani huwa hawaweze kubadilisha kitu.
MAONYO KUHUSU KINYWA CHA MCHAJI MUNGU
“Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia.” (Efe.4:29)
Kifungu hiki hapa juu Paulo anachambua kuhusu “wema dhidi ya uovu” kuhusu “maneno chanya” dhidi ya “maneno hasi” Msamiati wa kiyunani uliotumika wa neno “ovu” maana yake ni “uozo”! Lilitumika kutaja matunda au mboga zilizooza. Hali kadhalika, kuna maneno mengi “yaliyooza” yakitoka vinywani “yananuka” uchafu na kunajisi masikio na mioyo ya watu. Maneno ya jinsi hii hayapaswi kutoka kwenye kinywa cha mwenye kujitambulisha kuwa mtu wa Mungu, au mchaji Mungu.
Msisitizo wa Paulo kwa wacha Mungu ni kutumia vinywa vyetu kuachilia maneno yenye msaada wa kuwajenga wahitaji. Katika ulimwengu huu mahitaji siyo fedha au mali au vitu peke yake, bali hata “maneno yenye kujenga” ni bidhaa adimu katika jamii ya leo. Haya maneno mazuri ya kuwafaa wengine yametajwa tena katika waraka kama ifuatavyo:
“Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua iwapasavyo kumjibu kila mtu.” (Kol.4:6)

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....