Skip to main content

WANAWAKE WENGI HUFUNGA NA KUOMBA WANAUME WA NAMNA HII.



Ndugu zangu, nimeongea kuhusu baraka na heri ya kuwa na mwanamke wa pekee pia ni vizuri kwa wakina dada na wanawake kutambua kuwa nao wanatamani sana kuwa na mume wa namna hii. Hii pia ni namna moja ya sisi wanaume kujidai katika ndoa zetu. Mke huyu ana heri anapompata mume wa namna hii:
1️⃣ Mume anayemjua Mungu na anaishi maisha ya kumpendaza Mungu.
2️⃣ Mume anayetambua kuwa yeye ni baba wa familia, mume wa ndoa na mlinzi wa familia.
3️⃣ Mume anayejua kuwa mke wake anatakiwa kusikiliza na siyo kukaripia na kugombezwa kama mtoto na wakati mwengine kutamkiwa maneno makali mbele ya watoto.
4️⃣ Mume ambaye ana uwezo wa kujishusa pale anapofanya kosa, anapoumiza hisia za mke wake.
5️⃣ Mume ambaye anatambua ulimwengu wa mwanamke na anatambua mahitaji ya mke wake.
6️⃣ Mume ambaye anashirikisha mambo ya familia na ndoa kwa mke wake na wanapanga mipango mbalimbali ya familia kwa pamoja.
7️⃣ Mume ambaye anatambua kuwa ni wajibu wake kuwa na muda wa pekee wa kuwa na mke wake, kama vile outing au wenye uwezo basi mtoko wa kwenda mahali na kupumzika angalau hata mara moja kwa miezi kadhaa au kwa mwaka.
8️⃣ Mume ambaye anakumbuka siku maalum za mke wake na kumuenzi, kumpetipeti mke wake kama mtoto au "baby". hili ni la muhimu sana kwa wanawake.
9️⃣ Mume anayetambua kuwa ana wajibu wa kumsaidia mke wake hata kazi ndogo-ndogo za nyumbani muda unaporuhusu.
🔟 Mume ambaye anatambua malezi siyo kazi ya mke wake peke yake, bali kwa pamoja wanasimama imara kulea watoto.
1️⃣1️⃣ Mume ambaye anajivuania kuwa na mke wake na siyo kuona hata shida kumtambulisha au kuongozana naye.
1️⃣2️⃣ Mume ambaye ana nia ya maendeleo na katika maendeleo anajua mke wake ni nguzo muhimu ya wao kufikia malengo ya familia.
1️⃣3️⃣ Mume ambaye habadiliki kutokana na pesa nyingi anazopata, bado ni mwaminifu kwa mke wake na muwazi kwa kila jambo.
1️⃣4️⃣ Mume ambaye anampenda mke wake akiwa ni maskini na hata kama ni tajiri anatambua yote hayo ni baraka zao pamoja.
1️⃣5️⃣ Mume ambaye anafurahia mafanikio ya mke wake na pia kumtia moyo mke wake anapokutana na changamoto, zinakuwa zao wote.
1️⃣6️⃣ Mume ambaye kipato chake siyo siri yake, hana account za siri, kw sabau chochote anachopata anafahamu ni kwa ajili yao kwa pamoja katika familia.
1️⃣7️⃣ Mume anayetambua kuwa mapenzi na mahaba katika ndoa yanahitaji maandalizi mazuri hasa kumwanadaa mkewe na siyo kukurupuka na kumrukia na akimaliza shida zake anageuka pembeni kulala.
1️⃣8️⃣ Mume ambaye anatambua kuwa anaweza kujifunza na kuelemisha mambo mbalimbali na mke wake, siyo kumdharua kwa kila jambo. Mume ambaye anaona mazuri kwa mke wake, na pia kumsifia mke wake. Wanawake wanapenda kusifiwa na kutambuliwa

Mungu nijaalie mke mwema.

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....