Ndugu zangu, nimeongea kuhusu baraka na heri ya kuwa na mwanamke wa pekee pia ni vizuri kwa wakina dada na wanawake kutambua kuwa nao wanatamani sana kuwa na mume wa namna hii. Hii pia ni namna moja ya sisi wanaume kujidai katika ndoa zetu. Mke huyu ana heri anapompata mume wa namna hii:
1️⃣ Mume anayemjua Mungu na anaishi maisha ya kumpendaza Mungu.
2️⃣ Mume anayetambua kuwa yeye ni baba wa familia, mume wa ndoa na mlinzi wa familia.
3️⃣ Mume anayejua kuwa mke wake anatakiwa kusikiliza na siyo kukaripia na kugombezwa kama mtoto na wakati mwengine kutamkiwa maneno makali mbele ya watoto.
4️⃣ Mume ambaye ana uwezo wa kujishusa pale anapofanya kosa, anapoumiza hisia za mke wake.
5️⃣ Mume ambaye anatambua ulimwengu wa mwanamke na anatambua mahitaji ya mke wake.
6️⃣ Mume ambaye anashirikisha mambo ya familia na ndoa kwa mke wake na wanapanga mipango mbalimbali ya familia kwa pamoja.
7️⃣ Mume ambaye anatambua kuwa ni wajibu wake kuwa na muda wa pekee wa kuwa na mke wake, kama vile outing au wenye uwezo basi mtoko wa kwenda mahali na kupumzika angalau hata mara moja kwa miezi kadhaa au kwa mwaka.
8️⃣ Mume ambaye anakumbuka siku maalum za mke wake na kumuenzi, kumpetipeti mke wake kama mtoto au "baby". hili ni la muhimu sana kwa wanawake.
9️⃣ Mume anayetambua kuwa ana wajibu wa kumsaidia mke wake hata kazi ndogo-ndogo za nyumbani muda unaporuhusu.
🔟 Mume ambaye anatambua malezi siyo kazi ya mke wake peke yake, bali kwa pamoja wanasimama imara kulea watoto.
1️⃣1️⃣ Mume ambaye anajivuania kuwa na mke wake na siyo kuona hata shida kumtambulisha au kuongozana naye.
1️⃣2️⃣ Mume ambaye ana nia ya maendeleo na katika maendeleo anajua mke wake ni nguzo muhimu ya wao kufikia malengo ya familia.
1️⃣3️⃣ Mume ambaye habadiliki kutokana na pesa nyingi anazopata, bado ni mwaminifu kwa mke wake na muwazi kwa kila jambo.
1️⃣4️⃣ Mume ambaye anampenda mke wake akiwa ni maskini na hata kama ni tajiri anatambua yote hayo ni baraka zao pamoja.
1️⃣5️⃣ Mume ambaye anafurahia mafanikio ya mke wake na pia kumtia moyo mke wake anapokutana na changamoto, zinakuwa zao wote.
1️⃣6️⃣ Mume ambaye kipato chake siyo siri yake, hana account za siri, kw sabau chochote anachopata anafahamu ni kwa ajili yao kwa pamoja katika familia.
1️⃣7️⃣ Mume anayetambua kuwa mapenzi na mahaba katika ndoa yanahitaji maandalizi mazuri hasa kumwanadaa mkewe na siyo kukurupuka na kumrukia na akimaliza shida zake anageuka pembeni kulala.
1️⃣8️⃣ Mume ambaye anatambua kuwa anaweza kujifunza na kuelemisha mambo mbalimbali na mke wake, siyo kumdharua kwa kila jambo. Mume ambaye anaona mazuri kwa mke wake, na pia kumsifia mke wake. Wanawake wanapenda kusifiwa na kutambuliwa
Mungu nijaalie mke mwema.
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza