Skip to main content

HAKUNA NDOA ILIYOKAMILIKA ASILIMIA 1000%

Nataka kukuambia kuwa hakuna ndoa iliyo kamili yaani perfect, na kama kuna mtu Anakwambia kuwa ndoa yake ipo perfect ujue huyo ni muongo mkubwa vinginevyo kama hao watu waliooana ni mazombi kwa maana nyingine siyo Binadamu, hata kama ni ya mchungaji wako, shehe wako au hata askofu wako wa jimbo . hata hao mnaoona wanatupia mapicha picha na wake zao au waume zao kuonyesha kuwa wapo happy Haimaanishi kuwa ndio Muda wote asubuhi mpaka jioni,jumatatu mpaka jumapili, January mpaka December wao ni kucheka tu  hapana kiasi Kwamba ukaona kuwa ndoa yako haifai kabisa au upo kwenye Shimo, Kwenye ndoa watu kuna kukwazana, kupishana, hata kugombana kabisa wakati mwingine lakini  kikubwa tunachotofautiana wengi ni namna ya kushughulikia hayo matatizo yanapojitokeza na kuishia kuharibu ndoa zetu wenyewe



Katikati ya ndoa yenu nani mumemweka kama mhimili wenu ni Mungu au nani,? Wanaume kujaa ufahari kuwa mimi mwanaume Bwana siwezi omba msamaha, wanawake na wao husema Kwamba atanionaje huyu mimi labda nikimuanza kumuongelesha wakati yeye ndio Mwenye makosa,na wengi kutokuwa wakweli na kuamua kuyaongea matatizo yao hivyo kubaki na Vinyongo Moyoni mpaka kushindwa kusamehe. Tuachane na ujinga na tabia zinazohatarisha ndoa zetu, kumuanza mwenzio hata kama wewe sio mwenye makosa au kujipendekeza kwake ilimradi tu kunusuru na kuifanya ndoa Iendelee mbele  na  kuleta amani siyo Dhambi na siyo ujinga bali ni ujasiri na kujitambua zaidi.
   
      Bahati Magweiga
       Whatsapp : 0757472165
          Tigo           0659991953

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....