Nataka kukuambia kuwa hakuna ndoa iliyo kamili yaani perfect, na kama kuna mtu Anakwambia kuwa ndoa yake ipo perfect ujue huyo ni muongo mkubwa vinginevyo kama hao watu waliooana ni mazombi kwa maana nyingine siyo Binadamu, hata kama ni ya mchungaji wako, shehe wako au hata askofu wako wa jimbo . hata hao mnaoona wanatupia mapicha picha na wake zao au waume zao kuonyesha kuwa wapo happy Haimaanishi kuwa ndio Muda wote asubuhi mpaka jioni,jumatatu mpaka jumapili, January mpaka December wao ni kucheka tu hapana kiasi Kwamba ukaona kuwa ndoa yako haifai kabisa au upo kwenye Shimo, Kwenye ndoa watu kuna kukwazana, kupishana, hata kugombana kabisa wakati mwingine lakini kikubwa tunachotofautiana wengi ni namna ya kushughulikia hayo matatizo yanapojitokeza na kuishia kuharibu ndoa zetu wenyewe
Katikati ya ndoa yenu nani mumemweka kama mhimili wenu ni Mungu au nani,? Wanaume kujaa ufahari kuwa mimi mwanaume Bwana siwezi omba msamaha, wanawake na wao husema Kwamba atanionaje huyu mimi labda nikimuanza kumuongelesha wakati yeye ndio Mwenye makosa,na wengi kutokuwa wakweli na kuamua kuyaongea matatizo yao hivyo kubaki na Vinyongo Moyoni mpaka kushindwa kusamehe. Tuachane na ujinga na tabia zinazohatarisha ndoa zetu, kumuanza mwenzio hata kama wewe sio mwenye makosa au kujipendekeza kwake ilimradi tu kunusuru na kuifanya ndoa Iendelee mbele na kuleta amani siyo Dhambi na siyo ujinga bali ni ujasiri na kujitambua zaidi.
Bahati Magweiga
Whatsapp : 0757472165
Tigo 0659991953
Bahati Magweiga
Whatsapp : 0757472165
Tigo 0659991953
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza