asilimia kubwa yatu tupenda kujiwekea uhakika wa kile ambacho wanakitarajia kutoka kwa watu wengine lakini kila siku nimekuwa nikisema jambo hili kwenye makala zangu za kila siku kuwa jambo hilo limewatesa wengi sana hasa pale wanapokuwa wameshindwa kupata msaada juu ya kile ambacho walitarajia. kwa mfano kuna watu wanatumia pesa vibaya kwa sababu tu kuna sehemu wameahidiwa kuwa watapata kiwango chochote cha fedha kitakachowasaidia kutimiza yale ambayo wangependa yatimie katika mipango yao. hatima ya kujiaminisha siku zote ni fedheha kwni mambo yanabadilika na maisha ya watu yanabadilika pia. kwa hiyo unashauriwa kuwa na uhakika na kile ambacho unacho mkononi kwako na siyo kilichopo kwa mtu mwingine. haijarishi ni ndugu yako , jamaa yako, rafiki nk . epuka sana kuamini kauli zao juun ya upande wa fedha ama mambo ambayo unaona kabisa wamba kutimia kwako ni vigum .
Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza – Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17 ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza