MADHARA YA TAMAA KATIKA UFUGAJI
Mfugaji yoyote ili aweze kuona faida ya ufugaji wake lazima aweke Tamaa pembeni. Kuna utofauti kati ya Mfugaji mwenye Malengo na Mfugaji mwenye Tamaa.
Mfugaji mwenye Malengo hufanya muradi wake kwa uchache na kwa ufanisi, pia huweka ukomo wa kumiliki kuku kwa kiwango ambacho huweza kuwamudu na kumletea faida
Mfugaji mwenye Tamaa yeye kwake ukienda utakuta ana kuku 500 wa rika tofauti tofauti ambao hata kuwalisha ni mtihani kwake ila shida yake aonekane anamiliki kuku wengi japo faida yake ni 0%%
Mfano : umeweka kuku 100 kroila na umewakuza kwa shida hadi kufikia kutaga . Wanapoanza kutaga ni muda wa kuvuna mayai ili kurudisha garama zako. Cha ajabu hapa utakuta Mfugaji anakurupuka kuingiza vifaranga wapya 200 kwa kutegemea hawa kuku 100 wahudumie vifaranga 200 hadi kufikia kutaga.
Pia hao kuku 100 wajiendeshe wao wenyewe kupitia mayai. pia kuku 100 wahudumie familia.
Ukweli ni kwamba itafika sehemu utaona kama ufugaji unakuonea vile kumbe sio kweli bali ni matamaa yako tu mfugaji. Kwa hesabu za haraka kuku 100 kroila wakiwa watagaji wazuri na wanao simamiwa vyema watakupa 252,000/= kwa wiki ila usiache kukumbuka kwamba wanaweza kutaga chini ya kiwango.
Kama mfugaji utakuwa unategemea kuku 100 uliowakuza kwa shida ndio waendeshe 200 vipi siku ikitokea wameshindwa kutaga inavyotakiwa? Kuna wakati wanashuka utagaji bila tatizo lolote Jeee! Unaweza kumudu hawa 200? .
Asilimia 99% ya wafugaji wanaofuga kwa Tamaa huwa hatuoni faida kabisa. Kwa sababu Tunaamini Katika wingi na sio Katika ufanisi.
Ukiona kroila nipe
Ukiona sasso nipe
Ukiona tanbro nipe hata 10
Ukiona Malawi unasema nikichukua hata 20 sio mbaya.
Unajikuta mfugaji una aina zote za kuku pale nyumbani japo wachache wachache lakini hawaendani
✔️umri,
✔️ ukuaji tofauti
✔️ulishaji wao tofauti
✔️utagaji wao tofauti
Lengo hapo ni nini kama sio Tamaa?
Kwa nini usitumie hiyo pesa kuendesha kuku wa aina moja ili wakuwe vyema wakuletee matokeo? ????
Wafugaji wenye Malengo huwezi kukuta anafuga mbegu zote za kuku kwa pamoja bali huchagua ilio bora zaidi na kuiboresha ili apate matokeo ya haraka.
Ufugaji mpaka ufikie faida sio jambo jepesi kama wengi tunavyo chukulia. Inahitaji akili, umakini, mtaji na muda.
O786155188
ushauri wangu
✔️ punguza Tamaa na ridhika na ulichonacho kwanza hadi kikuletee matokeo. Kuingiza vifaranga wapya bila mtaji kwa kutegemea kuku 100 wawendeshe ni kutafuta *stress*
✔️Fuga kwa Malengo
✔️Chagua kitu ambacho unataka kuku wakusaidie kutimiza Katika safari ya maisha yako Kisha weka kidogo kidogo kutimiza hicho kitu.
http://www.tujenganemedia.blogspot.com
Inaweza kuwa ni kiwanja au ujenzi wa nyumba nk. Kama kuku watakujengea nyumba, au kukupa kiwanja nk lazima uhamasike kila uwonapo kitu hicho.
✔️jifanyie Tathimini kama unasonga mbele na uchukue hatua zaidi.
✔️Tumia sana watu wanaofanya vitu kwa vitendo zaidi ya wahamasishaji. Hawa wanaweza kukuingiza kwenye mtego ambao mwisho wa siku utakufanya uchukie ndoto zako.
✔️Chagua watu sahihi wa kujifunza kutoka kwao kuhusu ufugaji wako
✔️ kuwa na msimamo Katika kile unachoamini kuhusu ufugaji wako ili muradi kiwe sahihi.
By Magweiga
📞+255757472165
📞+255786155188
bahatimagweiga467@gmail.com
✔️vifaranga
✔️Mayai
✔️kuku
Vyote vinapatikana kwetu 24 hrs. Wasiliana nasi kupitia hizo namba hapo juu.
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza