Skip to main content

USIWE NA TAMAA KATIKA UFUGAJI.

 MADHARA YA TAMAA KATIKA UFUGAJI 

Mfugaji yoyote ili aweze kuona faida ya ufugaji wake lazima aweke Tamaa pembeni.  Kuna utofauti kati ya Mfugaji mwenye Malengo na Mfugaji mwenye Tamaa. 

Mfugaji mwenye Malengo hufanya muradi wake kwa uchache na kwa ufanisi, pia huweka ukomo wa kumiliki kuku kwa kiwango ambacho huweza kuwamudu na kumletea faida 

Mfugaji mwenye Tamaa yeye kwake ukienda utakuta ana kuku 500 wa rika tofauti tofauti ambao hata kuwalisha ni mtihani kwake ila shida yake aonekane anamiliki kuku wengi japo faida yake ni 0%%

Mfano : umeweka kuku 100 kroila  na umewakuza kwa shida hadi kufikia kutaga . Wanapoanza kutaga ni muda wa kuvuna mayai ili kurudisha garama zako.  Cha ajabu hapa utakuta Mfugaji anakurupuka kuingiza vifaranga wapya 200 kwa kutegemea hawa kuku 100 wahudumie vifaranga 200  hadi kufikia kutaga.  

Pia hao kuku 100 wajiendeshe wao wenyewe kupitia mayai.  pia kuku 100 wahudumie familia.

Ukweli ni kwamba itafika sehemu utaona kama ufugaji unakuonea vile kumbe sio kweli bali ni matamaa yako tu mfugaji.   Kwa hesabu za haraka kuku 100 kroila wakiwa watagaji wazuri na wanao simamiwa vyema watakupa 252,000/=  kwa wiki ila usiache kukumbuka kwamba wanaweza kutaga chini ya kiwango. 

Kama mfugaji utakuwa unategemea kuku 100 uliowakuza kwa shida ndio waendeshe 200  vipi siku ikitokea wameshindwa kutaga inavyotakiwa? Kuna wakati wanashuka utagaji bila tatizo lolote Jeee!  Unaweza kumudu hawa 200? . 

Asilimia 99% ya wafugaji wanaofuga kwa Tamaa  huwa hatuoni faida kabisa.  Kwa sababu Tunaamini Katika wingi na sio Katika ufanisi. 

 Ukiona kroila nipe

Ukiona sasso nipe

Ukiona tanbro  nipe hata 10 

Ukiona Malawi unasema nikichukua hata 20  sio mbaya.

Unajikuta mfugaji una aina zote za kuku pale nyumbani japo wachache wachache lakini hawaendani 

✔️umri, 

✔️ ukuaji tofauti 

✔️ulishaji wao tofauti 

✔️utagaji wao tofauti 

Lengo hapo ni nini kama sio Tamaa? 

Kwa nini usitumie hiyo pesa kuendesha kuku wa aina moja ili wakuwe vyema wakuletee matokeo? ????

Wafugaji wenye Malengo huwezi kukuta anafuga mbegu zote za kuku kwa pamoja bali huchagua ilio bora zaidi na kuiboresha ili apate matokeo ya haraka. 

Ufugaji mpaka ufikie faida sio jambo jepesi kama wengi tunavyo chukulia.  Inahitaji akili, umakini, mtaji na muda.

O786155188

 ushauri wangu

✔️ punguza Tamaa na ridhika na ulichonacho kwanza hadi kikuletee matokeo.  Kuingiza vifaranga wapya bila mtaji kwa kutegemea kuku 100 wawendeshe ni kutafuta *stress* 

✔️Fuga kwa Malengo 

✔️Chagua kitu ambacho unataka kuku wakusaidie kutimiza Katika safari ya maisha yako Kisha weka kidogo kidogo kutimiza hicho kitu. 

http://www.tujenganemedia.blogspot.com

 Inaweza kuwa ni kiwanja au ujenzi wa nyumba nk.  Kama kuku watakujengea nyumba, au kukupa kiwanja nk lazima uhamasike kila uwonapo kitu hicho. 

✔️jifanyie Tathimini kama unasonga mbele na uchukue hatua zaidi.  

✔️Tumia sana watu wanaofanya vitu kwa vitendo zaidi ya wahamasishaji. Hawa wanaweza kukuingiza kwenye mtego ambao mwisho wa siku utakufanya uchukie ndoto zako.  

✔️Chagua watu sahihi wa kujifunza kutoka kwao kuhusu ufugaji wako 

✔️ kuwa na msimamo Katika kile unachoamini kuhusu ufugaji wako ili muradi kiwe sahihi. 

By Magweiga 

📞+255757472165

📞+255786155188

bahatimagweiga467@gmail.com 

✔️vifaranga 

✔️Mayai

✔️kuku 

Vyote vinapatikana kwetu 24 hrs.  Wasiliana nasi kupitia hizo namba hapo juu.

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....