Skip to main content

MAMBO YANAYO KWAMISHA UFUGAJI

MAGWEIGA POULTRY INVESTMENT(wajasiriamali wa kuku na bidhaa zake)

MAMBO YANAYOKWAMISHA WAFUGAJI WENGI. 

Ufugaji ni rahisi ukitumia faida za mezani na kushuhudia watu wanafanya.  Hali hi inaweza ikawa tofauti ukianza wewe mwenyewe kwa vitendo.  Ni jambo gumu kiasi chake endapo mfugaji atapuza kanuni bora za Ufugaji. 

Hapa mfugaji mpya anapaswa kujitathimini na kujipima kama anaweza kutoboa na kufikia matamanio yake kiufugaji.  

 Ufugaji ni kazi ngumu lakni imejawa na mafanikio kabambe na pia ni miongoni mwa furusa ambazo zipo wazi.  Ila vigezo na mashariti kuzingatiwa.

kinacho kwamisha ufugaji kwa asilimia kubwa ni mambo yafuatayo . Mfugaji asipo yavalia njuga ataishia kwenye msongo wa mawazo na kujipa magonjwa ya moyo. Magweiga poultry investment

1. Magonjwa . Kipengele hiki kimekuwa changamoto kubwa sana kwa sisi wafugaji.  Yapo magonjwa changizwa  ambayo ni mfugaji mwenyewe anakubaliana na ugonjwa husika kutokea 

✔️ Typhoid 

✔️Mafua 

✔️ coccidiosis 

✔️kipindu pindu cha kuku

 Haya yote ni magonjwa ni magonjwa ambayo yanamlengo wa kimazingira. Ni magonjwa ambayo husababishwa na

✔️ uchafu wa mabanda, 

✔️vyombo vya maji, 

✔️️mabanda kuwa mabichi muda mrefu,  

✔️Uchanganywaji wa kuku wasio endana umri,  ✔️Mzunguko hafifu wa hewa bandani, 

✔️chakula kuwa kichafu na kilicho chini ya kiwango,  

✔️Kutokuwa na vitendea kazi maalum kwa banda husika,  

✔️usimamizi usiokuwa endelevu,  

✔️Matumizi ya dozi yasioweza kupona kwa kuku jambo ambalo hupelekea kudumu kwa magonjwa muda mrefu bandani na hatimaye kupelekea vifo, 

✔️ Kuchelewa kubaini ugonjwa ukiwa kwenye stage za mwanzo. 

Pia yapo magonjwa yenye mlengo wa chanjo kama vile  

Newcastle disease,  gumboro, 

marekes,  

IB  nk.  Haya ni magonjwa ambayo mfugaji anapaswa kutumia chanjo kuwakinga kuku wake. 

 Hapa napo kumekuwepo na changamoto kuwa ya Nani amfunge paka kengere?* magonjwa Haya yakitokea huwa kuna kusingiziana  Kati ya muuzaji na mfugaji.  

Mfugaji anasema chanjo aliwapa labda aliponunua ndio kuna kasoro lakini pia muuzaji hutetea kwa nguvu zote  ubora wa chanjo zake. 

Anayepata hasara kubwa ni mfugaji.  Utakuta kapoteza kuku *1000*  kwa magonjwa Haya yenye mlengo wa chanjo.  

Hapa ni kuhakikisha unazingatia mambo muhimu wakati wa kutoa chanjo,  kabla na baada ya chanjo.   Chagua chanzo sahihi cha  uchukuaji wa chanjo. 

 2 .Tamaa. ni miongoni mwa mambo yanayo kwamisha wafugaji wengi na kujikuta wanapata hasara kuwa.  Unakuta mfugaji mtaji wake ni kuhudumia kuku 100 ndani ya miezi 5 alafu mfugaji huyo anaingiza vifaranga 500.  Kinachotokea hapa ni mtaji kukatika na kujikuta umeingia kwenye janga la kudumaza kuku. 

Wingi si hoja. Unaweza ukawa na kuku 500  dhaifu,  hawana afya,  wamekonda na hata kuwauza ni changamoto. Lakini mwanzako akawa na kuku 200 wenye kiwango na afya nzuri.  Huwezi kumfikia hata kidogo.  

0757472165

NB: Maisha ni kupanga  na kupanga ni kuchagua

Fuga unachokimudu na utaifurahia kazi hi ya ufugaji.  Utapata matokeo mazuri na ya kufurahisha.   

0786155188

Ili tufanye vyema kwenye miradi yetu na kupata matokeo lazima Tuzingatie 

✔️ Usafi wa mabanda 

✔️Usafi wa vyombo 

✔️Chanjo 

✔️ Chakula bora . Epuka kujichanganyia hovyo chakula.  Tumia formula zinazoleta matokeo chanya.  Usiwe mwepesi wa kuchakachua chakula ukidhani unakwepa garama.  Watakudai huko mbeleni. 

✔️ Vitamin +minerals 

✔️Mbegu bora . Chagua Mbegu inayoweza kukua kwa haraka na kupata mwitikio +++

✔️Bajeti sahihi . Usiweke kuku ambao haujui namna ya kufika nao kwenye lengo.  

✔️ Usimamizi binafsi . Fuatilia kwa ukaribu kwani wewe ndio uliyebeba maono ya miradi yako.  Fuatilia kujua kama pesa yako itarejea au laa! 

✔️ Nia ya kufanya 

✔️Elimu ya ufugaji.  Usiache kuendelea kujifunza, . Hakuna aliyewahi  kumaliza kusoma 

 By Magweiga

 Magweiga poultry investment

Wauzaji wa vifaranga, kuku, mayai nk. . 

📞+255786155188

📞+255757472165


Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....