MAGWEIGA POULTRY INVESTMENT(wajasiriamali wa kuku na bidhaa zake)
MAMBO YANAYOKWAMISHA WAFUGAJI WENGI.
Ufugaji ni rahisi ukitumia faida za mezani na kushuhudia watu wanafanya. Hali hi inaweza ikawa tofauti ukianza wewe mwenyewe kwa vitendo. Ni jambo gumu kiasi chake endapo mfugaji atapuza kanuni bora za Ufugaji.
Hapa mfugaji mpya anapaswa kujitathimini na kujipima kama anaweza kutoboa na kufikia matamanio yake kiufugaji.
Ufugaji ni kazi ngumu lakni imejawa na mafanikio kabambe na pia ni miongoni mwa furusa ambazo zipo wazi. Ila vigezo na mashariti kuzingatiwa.
kinacho kwamisha ufugaji kwa asilimia kubwa ni mambo yafuatayo . Mfugaji asipo yavalia njuga ataishia kwenye msongo wa mawazo na kujipa magonjwa ya moyo. Magweiga poultry investment
1. Magonjwa . Kipengele hiki kimekuwa changamoto kubwa sana kwa sisi wafugaji. Yapo magonjwa changizwa ambayo ni mfugaji mwenyewe anakubaliana na ugonjwa husika kutokea
✔️ Typhoid
✔️Mafua
✔️ coccidiosis
✔️kipindu pindu cha kuku
Haya yote ni magonjwa ni magonjwa ambayo yanamlengo wa kimazingira. Ni magonjwa ambayo husababishwa na
✔️ uchafu wa mabanda,
✔️vyombo vya maji,
✔️️mabanda kuwa mabichi muda mrefu,
✔️Uchanganywaji wa kuku wasio endana umri, ✔️Mzunguko hafifu wa hewa bandani,
✔️chakula kuwa kichafu na kilicho chini ya kiwango,
✔️Kutokuwa na vitendea kazi maalum kwa banda husika,
✔️usimamizi usiokuwa endelevu,
✔️Matumizi ya dozi yasioweza kupona kwa kuku jambo ambalo hupelekea kudumu kwa magonjwa muda mrefu bandani na hatimaye kupelekea vifo,
✔️ Kuchelewa kubaini ugonjwa ukiwa kwenye stage za mwanzo.
Pia yapo magonjwa yenye mlengo wa chanjo kama vile
Newcastle disease, gumboro,
marekes,
IB nk. Haya ni magonjwa ambayo mfugaji anapaswa kutumia chanjo kuwakinga kuku wake.
Hapa napo kumekuwepo na changamoto kuwa ya Nani amfunge paka kengere?* magonjwa Haya yakitokea huwa kuna kusingiziana Kati ya muuzaji na mfugaji.
Mfugaji anasema chanjo aliwapa labda aliponunua ndio kuna kasoro lakini pia muuzaji hutetea kwa nguvu zote ubora wa chanjo zake.
Anayepata hasara kubwa ni mfugaji. Utakuta kapoteza kuku *1000* kwa magonjwa Haya yenye mlengo wa chanjo.
Hapa ni kuhakikisha unazingatia mambo muhimu wakati wa kutoa chanjo, kabla na baada ya chanjo. Chagua chanzo sahihi cha uchukuaji wa chanjo.
2 .Tamaa. ni miongoni mwa mambo yanayo kwamisha wafugaji wengi na kujikuta wanapata hasara kuwa. Unakuta mfugaji mtaji wake ni kuhudumia kuku 100 ndani ya miezi 5 alafu mfugaji huyo anaingiza vifaranga 500. Kinachotokea hapa ni mtaji kukatika na kujikuta umeingia kwenye janga la kudumaza kuku.
Wingi si hoja. Unaweza ukawa na kuku 500 dhaifu, hawana afya, wamekonda na hata kuwauza ni changamoto. Lakini mwanzako akawa na kuku 200 wenye kiwango na afya nzuri. Huwezi kumfikia hata kidogo.
0757472165
NB: Maisha ni kupanga na kupanga ni kuchagua
Fuga unachokimudu na utaifurahia kazi hi ya ufugaji. Utapata matokeo mazuri na ya kufurahisha.
0786155188
Ili tufanye vyema kwenye miradi yetu na kupata matokeo lazima Tuzingatie
✔️ Usafi wa mabanda
✔️Usafi wa vyombo
✔️Chanjo
✔️ Chakula bora . Epuka kujichanganyia hovyo chakula. Tumia formula zinazoleta matokeo chanya. Usiwe mwepesi wa kuchakachua chakula ukidhani unakwepa garama. Watakudai huko mbeleni.
✔️ Vitamin +minerals
✔️Mbegu bora . Chagua Mbegu inayoweza kukua kwa haraka na kupata mwitikio +++
✔️Bajeti sahihi . Usiweke kuku ambao haujui namna ya kufika nao kwenye lengo.
✔️ Usimamizi binafsi . Fuatilia kwa ukaribu kwani wewe ndio uliyebeba maono ya miradi yako. Fuatilia kujua kama pesa yako itarejea au laa!
✔️ Nia ya kufanya
✔️Elimu ya ufugaji. Usiache kuendelea kujifunza, . Hakuna aliyewahi kumaliza kusoma
By Magweiga
Magweiga poultry investment
Wauzaji wa vifaranga, kuku, mayai nk. .
📞+255786155188
📞+255757472165
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza