Skip to main content

KUJITAMBUA KATIKA WAKATI SAHIHI

Kujitambua katika maisha ni moja ya hatua kubwa ambayo humtofautisha mtu na mtu katika swala zima la mafanikio.
Nini maana ya kujitambua?
Ukizungumzia neno kujitambua kwa mtu yeyote ni  kuwa mtu sahihi, mahali sahihi, kwa muda sahihi.   Kuwa mtu sahihi maana yake ni kuwa mtu ambaye unajisimamia na kutekeleza kile ambacho unatakiwa kufanya wewe kama mwanadamu.
Mahali sahihi inamanisha kwamba upo kwenye kiwango ambacho ulistahiri kuwepo kimaisha kwa maana ya kwamba kiuchumi, kijamii na hata kisiasa.
 Asilimia kubwa ya vijana waliowengi hupoteza uelekeo wao wa maisha kwa kushindwa kujitambua katika umuri nyeti ambao bado vijana hawa wanakuwepo na nguvu za kutosha za kuwawezesha kushughulika na ndoto zao katika maisha.
 Tunapaswa kujitambua na kutambua kwamba chochote ambacho kinaonekana sasa katika Macho yetu ni mamzi mugumu yaliofanywa na watu kama sisi.  Vijana wengi tumekuwa na tabia furani ya kuiambia dunia tunachokifahamu badala ya kuonyesha Dunia unacho kifahamu kwa vitendo.
Maneno pekee hayawezi kukusukuma mbele katika kufikia ndoto zako. Unapaswa kujielekeza katika vitendo zaidi juu ya kile unachozungumzia kuliko nadharia.
Ili kugundua kwamba umejitambua lazima uwe na uwezo wa kujibu haya maswali
1. Kwanini upo hapa duniani?
2. Wewe ni nani hapa Duniani?
3. Kwanini upo katika hali hiyo ulionayo kimaisha?
4. Ni nani anapaswa kulaumiwa katika wewe kuwa hivyo ulivyo kimaisha?
5. Ni nani anathirika kupitia wewe kuwa hivyo?
6. Je anawajibu wowote wa kukutoa katika hali hiyo kwa sasa?
7. Akishindwa kukutoa katika hapo ulipomtegea kuchukua mamzi mugumu kuna madhara yoyote ya moja kwa moja yatakayompata?
8. Kwa nini afikirie kwa ajili ya maisha yako
9. Ikitokea leo akasimamisha tabia ya kufikiri kwa niaba yako utaweza kujimudu?
 Majibu yatakayotokana na kujiuliza hayo maswali yatakusaidia kujijenga na kuchukua jukumu la kufanya mamzi magumu kuyatumikia maisha yako.

UMUHIMU WA KUJITAMBUA KAMA KIJANA.

kujitambua kama kijana katika muda sahihi,  mazingira sahihi na umuri sahihi kuna faida na umuhimu mkubwa katika kubadili maisha yako.  Hakuna aliefanikiwa na kutimiza ndoto zake pasipo kujitambua.  Hiyo ndio mbegu pekee ambayo ilipandwa na watu ambao sasahivi tumekuwa tukiwa shabikia kwa manufaa binafsi.
1.kujitambua husaidia mtu kuwa tofauti na kufikiria vitu chanya ambavyo ni tofauti kabisa na wengine katika jamii inayo mzunguka.  Kumbuka kwamba huwezi kuwa mtu tofauti katika jamii kwa kufikiria vitu sawia na wengine.
2. Husaidia kufikia ndoto zako kirahisi
3. Husaidia kujenga uaminifu na watu katika jamii.  Ikumbukwe kwamba mafanikio yoyote huletwa na watu wanao kuzunguka katika muda sahihi.
4. Husaidia kujenga saikolojia

MAMBO YANAYOWEZA KUSADIA KUJITAMBUA KWA HARAKA NA KUWA MTU SAHIHI KATIKA MAISHA YAKO:

1: Kwepa mazingira hasi
2: Wekeza kwenye utafutaji wa maarifa sahihi na endelevu
3: penda kujitegemea hata kwa kidogo ulicho nacho
4: Jifunze kuwa mtu sahihi muda wote katika maisha yako.
4: fuatilia na kuyajua mapungufu ili uweze kuwepuka kurudia rudia udhaifu muda mwingi.
5: Chagua mahali sahihi pa kuelekeza maisha yako  ( Driven power )
6: Epuka ukusanyaji wa taarifa zisizo za lazima.  Chagua taarifa sahihi na zifanyie utafiti kabla hujaruhusu zianze kuendesha maisha yako.
7: Tathimini mamzi unayofanya kabla ya matumizi yake katika maisha.
8: Chagua mtu sahihi wa kukuongoza katika kufikia unakotaka kufika kimafanikio.
9: Jenga tabia ya kushinda mambo hasi
10. Jenga utamaduni wa kujisemesha semesha katika mtazamo chanya ili ukae kichwani mwako. ... nk

Makala hii itaendelea hapo badaye  . Tunakushauri usiwe mbali na tujenganemedia.

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....