MAFANIKIO HUANZA NA FIKIRA
Nimependa kushare nanyi kidogo baada ya kufanya utafiti ambao sio rasmi saana, hasa tukizungumzia mada ya Mafanikio. Watu wengi hasa sisi vijana tumekuwa tukichukulia mafanikio kama tukio....(Success as an event) lakini ukweli ni kwamba mafanikio au Kufanikiwa katika jambo lolote ni Mchakato(a process) ambao unakuwa na Mkakati Fulani/ Maalumu (strategy). Mchakato huo maalumu lazima uanzie akilini kwanza. Tunapoongelea Mafanikio katika chochote ni lazima kwanza kuamini katika kufanikiwa ndipo tuandae mkakati ambao utakusaidia au ambao utakuwa ndio njia ya kukufikisha kwenye Mafanikio. Ukweli ni kwamba Huwezi yafikia Mafanikio Makubwa yoyote halali yenye Thamani Bila Kuamini kwanza katika Mafanikio na kujenga mtazamo Chanya juu ya kile unachokiendea. Lakini Kwa Kumalizia Unaweza kuamini katika Mafanikio na ukawa na Mkakati bila Matendo Nazi (Plan of Action) bado inakuwa haina maana. Lazima kupanga matendo kazi yatakayokupitisha kwenye huo Mkakati ili kuyafikia Mafanikio hayo......Wengi huwa tunaamini kuwa IPO SIKU nami nitafanikiwa....Kibaya ni pale unapoamini hivyo huku ukiwa huna mkakati wowote, that's wrong(ni mbaya saana, wala sio sahihi). So anza kuamini Kuhusu Mafanikio kisha weka mkakati na Matendo kazi.....Kisha twende tukapige kazi....Always Utakatishwa Tamaa katika mpango huo au Malengo hayo...Don't look back...Fight Fight Fight wengine wanasema. Do it and Do it and Do it and Do it and Do it again and again and again Until the Job get done.....Hapo lazima ukifikie kile unachokitaka. Nawaasa vijana wenzangu twendeni Tukafanye kazi.....Tuache Kuamini kwenye Bahati.
USIPOTEZE NDOTO ZAKO KWA VITU VIDOGO VIDOGO (TAMAA )
Nirahisi kila mtu kuweka malengo na mipango yake mizuri ndani ya muda fulani,
Lakini kufikia mipango hiyo imekuwa ngumu kwa watu wengi sana na hivyo kujikuta wamesha jipoteza na kupoteza mipango yao.
Kujipoteza na kupoteza mwelekeo kwenye maisha yenye malengo kunatokana na tamaa za muda mfupi hasa unapo kuwa na malengo ya mda mrefu na hapo ndipo akili inakuwa rahisi kuhamia kwenye mambo yaliyo ya kawaida na sio yale mtu alipanga kukamilisha kwa muda alio jipangia.
Tamaa ya vitu vidogo vidogo na vilivyo rahisi kupatikana ndio kizuizi cha watu wengi kufikia malengo yao makubwa,
Mambo madogo madogo ndiyo yanayo ongozwa na hisia za tamaa na hivyo watu kujikuta kupata vitu hivyo badala ya malengo yao yaliyo makubwa.
Malengo Makubwa na ya mda mrefu mala nyingi hayafikiwi kwa sababu ya vitu vidogo ambavyo havikuwepo kwenye mipango yoyote ya awali,
Mfano:Watu wengi wamekuwa na mipango mikubwa na ya mda mrefu lakini wanapo kuwa katikati ya utekelezaji wa mipango hiyo kunajitokeza vitu vidogo vidogo vinavyo kuwa rahisi kuvipata kutokana na urahisi wa kuvipata basi akili huanza kufikiri na kutorokea kwenye vitu hivyo badala ya mipango yao na pindi muda wao unapo kuwa umeisha ambao walijipangia kwenye lengo lao hujikuta wana vitu ambavyo hawa kutegemea wala kupanga na hivyo kuongeza muda wa mipango yao.
Rafiki kuepuka kuathiriwa na tamaa zinazo weza kuwa kuzuizi kwako kufikia mipango yako ni Wewe kutambua umuhimu wa mpango wako,Kujiwekea nidhamu binafsi na kuhakikisha hutoki nje ya mpango wako,Kujikumbusha mala kwa mala na kuona ukubwa wa mpango wako,Uking'ang'anizi na mengine mengi.
Hakikisha hutoki nje ya chaki au mpango wako huo,
Hakikisha mambo mengine yote yanasimama hasa yanayo hitaji fedha zako hata kama ni kidogo,
Hakikisha usiku na mchana unapata muda wa kutafakari mpango wako na kupanga mbinu zaidi kuufanikisha kwa kila namna.
Mwisho kabisa Epuka kutembea na fedha zisizo kuwa na mpango wowote kwenye ratiba yako ya siku,
Epuka tamaa ya aina yoyote inayo
chochewa na uwepo wa fedha zako.
MWISHO KABISA KUMBUKA HIKI :
unapotazama mwenzako kafanikiwa ukamuwekea mashaka, ujue ndivyo hivyo na wenzio wanakuwekea mashaka ya kwanini siyo wewe ufanikiwe??. mungu siku zote hawezi kuelekeza mafanikio kwa watu wenye roho wa kwanini katika maendeleo. ukiona mwenzio kapiga hatua furani katika maisha unapaswa kumpongeza na kumtia moyo kwa sababu baada ya huyo ni zamu yako inayofuata katika kufanikiwa....
kadiri unavyozidi kujitenga na watu ndivyo hivyo unajitenga na ujio wa mafanikio , kumbuka kwamba mafanikio yako yako mikononi mwa watu wengine. hata waliofanikiwa walikuwa na watu waliokuwa wanawaunga mkono katika biashara zao kwa kununua bidhaa zao na kama wangesusiwa na wanadamu kamwe wasingefikia mafanikio hayo.Muhimu ni kwamba ishi na watu upate vitu na ukiamua kujitenga na watu shariti uyasahau mafanikio
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza