Skip to main content

MAFANIKIO HUANZA NA FIKIRA.



                 
                         


MAFANIKIO HUANZA NA FIKIRA
Nimependa kushare nanyi kidogo baada ya kufanya utafiti ambao sio rasmi saana, hasa tukizungumzia mada ya Mafanikio. Watu wengi hasa sisi vijana tumekuwa tukichukulia mafanikio kama tukio....(Success as an event) lakini ukweli ni kwamba mafanikio au Kufanikiwa katika jambo lolote ni Mchakato(a process) ambao unakuwa na Mkakati Fulani/ Maalumu (strategy). Mchakato huo maalumu lazima uanzie akilini kwanza. Tunapoongelea Mafanikio katika chochote ni lazima kwanza kuamini katika kufanikiwa ndipo tuandae mkakati ambao utakusaidia au ambao utakuwa ndio njia ya kukufikisha kwenye Mafanikio. Ukweli ni kwamba Huwezi yafikia Mafanikio Makubwa yoyote halali yenye Thamani Bila Kuamini kwanza katika Mafanikio na kujenga mtazamo Chanya juu ya kile unachokiendea. Lakini Kwa Kumalizia Unaweza kuamini katika Mafanikio na ukawa na Mkakati bila Matendo Nazi (Plan of Action) bado inakuwa haina maana. Lazima kupanga matendo kazi yatakayokupitisha kwenye huo Mkakati ili kuyafikia Mafanikio hayo......Wengi huwa tunaamini kuwa IPO  SIKU nami nitafanikiwa....Kibaya ni pale unapoamini hivyo huku ukiwa huna mkakati wowote, that's wrong(ni mbaya saana, wala sio sahihi). So anza kuamini Kuhusu Mafanikio kisha weka mkakati na Matendo kazi.....Kisha twende tukapige kazi....Always Utakatishwa Tamaa katika mpango huo au Malengo hayo...Don't look back...Fight Fight Fight wengine wanasema. Do it and Do it and Do it and Do it and Do it again and again and again Until the Job get done.....Hapo lazima ukifikie kile unachokitaka. Nawaasa vijana wenzangu twendeni Tukafanye kazi.....Tuache Kuamini kwenye Bahati.

USIPOTEZE NDOTO ZAKO KWA VITU VIDOGO VIDOGO  (TAMAA )

Nirahisi kila mtu kuweka malengo na mipango yake mizuri ndani ya muda fulani,
Lakini kufikia mipango hiyo imekuwa ngumu kwa watu wengi sana na hivyo kujikuta wamesha jipoteza na kupoteza mipango yao.

Kujipoteza na kupoteza mwelekeo kwenye maisha yenye malengo kunatokana na tamaa za muda mfupi hasa unapo kuwa na malengo ya mda mrefu na hapo ndipo akili inakuwa rahisi kuhamia kwenye mambo yaliyo ya kawaida na sio yale mtu alipanga kukamilisha kwa muda alio jipangia.

Tamaa ya vitu vidogo vidogo na vilivyo rahisi kupatikana ndio kizuizi cha watu wengi kufikia malengo yao makubwa,
Mambo madogo madogo ndiyo yanayo ongozwa na hisia za tamaa na hivyo watu kujikuta kupata vitu hivyo badala ya malengo yao yaliyo makubwa.

Malengo Makubwa na ya mda mrefu mala nyingi hayafikiwi kwa sababu ya vitu vidogo ambavyo havikuwepo kwenye mipango yoyote ya awali,
Mfano:Watu wengi wamekuwa na mipango mikubwa na ya mda mrefu lakini wanapo kuwa katikati ya utekelezaji wa mipango hiyo kunajitokeza vitu vidogo vidogo vinavyo kuwa rahisi kuvipata kutokana na urahisi wa kuvipata basi akili huanza kufikiri na kutorokea kwenye vitu hivyo badala ya mipango yao na pindi muda wao unapo kuwa umeisha ambao walijipangia kwenye lengo lao hujikuta wana vitu ambavyo hawa kutegemea wala kupanga na hivyo kuongeza muda wa mipango yao.

Rafiki kuepuka kuathiriwa na tamaa zinazo weza kuwa kuzuizi kwako kufikia mipango yako ni Wewe kutambua umuhimu wa mpango wako,Kujiwekea nidhamu binafsi na kuhakikisha hutoki nje ya mpango wako,Kujikumbusha mala kwa mala na kuona ukubwa wa mpango wako,Uking'ang'anizi  na mengine mengi.

Hakikisha hutoki nje ya chaki au mpango wako huo,
Hakikisha mambo mengine yote yanasimama hasa yanayo hitaji fedha zako hata kama ni kidogo,
Hakikisha usiku na mchana unapata muda wa kutafakari mpango wako na kupanga mbinu zaidi kuufanikisha kwa kila namna.
Mwisho kabisa Epuka kutembea na fedha zisizo kuwa na mpango wowote kwenye ratiba yako ya siku,
Epuka tamaa ya aina yoyote inayo
 chochewa na uwepo wa fedha zako.

 MWISHO KABISA KUMBUKA HIKI :

unapotazama mwenzako kafanikiwa ukamuwekea mashaka, ujue ndivyo hivyo na wenzio wanakuwekea mashaka ya kwanini siyo wewe ufanikiwe??. mungu siku zote hawezi kuelekeza mafanikio kwa watu wenye roho wa kwanini katika maendeleo. ukiona mwenzio kapiga hatua furani katika maisha unapaswa kumpongeza na kumtia moyo kwa sababu baada ya huyo ni zamu yako inayofuata katika kufanikiwa....
 kadiri unavyozidi kujitenga na watu ndivyo hivyo unajitenga  na ujio wa mafanikio , kumbuka kwamba mafanikio yako yako mikononi mwa watu wengine. hata waliofanikiwa walikuwa na watu waliokuwa wanawaunga mkono katika biashara zao kwa kununua bidhaa zao na kama wangesusiwa na wanadamu kamwe wasingefikia mafanikio hayo.Muhimu ni kwamba ishi na watu upate vitu na ukiamua kujitenga na watu shariti uyasahau mafanikio


Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....