Skip to main content

sulemani mwana wa daudi

    Methali za Sulemani+ mwana wa Daudi,+ mfalme wa Israeli:+  Ili mtu ajifunze* hekima+ na nidhamu;Ili aelewe maneno ya hekima;  Ili apate nidhamu+ inayoleta ufahamu,Uadilifu,+ busara,*+ na unyoofu;*  Ili kumfanya mjinga awe mwerevu;+Ili kumpa kijana ujuzi na uwezo wa kufikiri.+  Mtu mwenye hekima husikiliza na kujifunza zaidi;+Mtu mwenye uelewaji hupata mwelekezo stadi*+  Ili kuelewa methali na fumbo,*Maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao.+  Kumwogopa* Yehova ndio mwanzo wa ujuzi.+Ni wapumbavu tu wanaodharau hekima na nidhamu.+  Mwanangu, sikiliza nidhamu ya baba yako,+Wala usiyaache mafundisho* ya mama yako.+  Ni shada linalovutia kwenye kichwa chako+Na pambo maridadi shingoni mwako.+10  Mwanangu, watenda dhambi wakijaribu kukushawishi, usikubali.+11  Wakisema: “Njoo twende.Acha tuvizie ili kumwaga damu.Tutajificha na kuwashambulia bila sababu watu wasio na hatia.12  Tutawameza wakiwa hai kama Kaburi*linavyomeza,Wazima-wazima, kama wale wanaoshuka shimoni.13  Na tunyakue mali zao zote zenye thamani;Nyumba zetu tutazijaza nyara.14  Unapaswa kujiunga nasi,*Nasi sote tutagawana sawasawa vitu tunavyoiba.”*15  Mwanangu, usiwafuate.Iepushe miguu yako na njia yao.+16  Kwa maana miguu yao hukimbilia kutenda uovu;Wanaenda haraka kumwaga damu.+17  Kwa kweli ni kazi bure kutandaza wavu huku ndege akitazama.18  Ndio sababu wanavizia ili kumwaga damu;Wanajificha ili wawaue* wengine.19  Hizo ndizo njia za wale wanaotafuta faida isiyo ya haki,Ambayo itawaangamiza wale wanaoipata.+20  Hekima ya kweli+ hupaza sauti kubwa barabarani.+Huendelea kuinua sauti yake katika viwanja vya jiji.+21  Hupaza sauti kwenye makutano ya barabara zenye watu wengi.Nayo husema hivi kwenye malango ya jiji:+22  “Ninyi wajinga mtaendelea kuupenda ujinga mpaka lini?Nanyi wadhihaki mtaendelea kufurahia dhihaka mpaka lini?Nanyi wapumbavu mtaendelea kuchukia ujuzi mpaka lini?+23  Sikilizeni karipio langu.*+Ndipo nitakapowamiminia roho yangu;Nitawajulisha maneno yangu.+24  Kwa sababu niliwaita, lakini mkaendelea kukataa,Niliunyoosha mkono wangu, lakini hakuna yeyote aliyejali,+25  Mliendelea kupuuza ushauri wangu woteNa kukataa karipio langu,26  Mimi pia nitawacheka mtakapopatwa na msiba;Nitawadhihaki jambo mnaloogopa litakapokuja,+27  Jambo mnaloogopa litakapokuja kama dhoruba,Na msiba wenu utakapofika kama upepo wa dhoruba,Wakati dhiki na taabu zitakapowapata.28  Wakati huo wataendelea kuniita, lakini sitajibu;Watanitafuta kwa bidii, lakini hawatanipata,+29  Kwa sababu walichukia ujuzi,+Nao hawakuchagua kumwogopa Yehova.+30  Walikataa ushauri wangu;Waliyadharau makaripio yangu yote.31  Basi watapata matokeo* ya njia yao,+Nao watashiba kabisa mashauri yao* wenyewe.32  Kwa maana upotovu wa wajinga utawaua,Na kutojali kwa wapumbavu kutawaangamiza.33  Lakini yule anayenisikiliza ataishi kwa usalama+Naye hatahangaishwa na woga wa msiba.”+

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....