Ushuhuda wa Yohana Mbatizaji
19 Lk 3:15,16 Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani? 20Mdo 13:25 Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo. 21Kum 18:15,18; Mal 4:5; Mt 17:10; Yn 6:14; 7:40 Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La. 22Basi wakamwambia, U nani? Na tupate jibu la kuwapelekea wale waliotutuma. Wanenaje juu yako mwenyewe? 23Isa 40:3; Mt 3:3; Mk 1:3; Lk 3:4Akasema, Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, Inyosheni njia ya Bwana! Kama vile alivyonena nabii Isaya. 24Nao wale waliotumwa walikuwa wametoka kwa Mafarisayo. 25Mt 21:25 Wakamwuliza, wakamwambia, Mbona basi wabatiza, ikiwa wewe si Kristo, wala Eliya, wala nabii yule? 26Mt 3:11; Mk 1:7,8 Yohana akawajibu akisema, Mimi nabatiza kwa maji. Katikati yenu amesimama yeye msiyemjua ninyi. 27Yn 3:26; Mdo 13:25 Ndiye yule ajaye nyuma yangu, ambaye mimi sistahili kuilegeza kamba ya kiatu chake. 28Mt 3:6,13 Hayo yalifanyika huko Bethania ng'ambo ya Yordani, alikokuwako Yohana akibatiza.
Mwana-kondoo wa Mungu
29 Yn 1:36; Isa 53:7 Kesho yake alimwona Yesu akija kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu! 30Yn 15:27 Huyu ndiye niliyenena habari zake ya kwamba, Yuaja mtu nyuma yangu, ambaye amekuwa mbele yangu; kwa maana alikuwa kabla yangu. 31Wala mimi sikumjua; lakini ili adhihirishwe kwa Israeli ndiyo maana mimi nilikuja nikibatiza kwa maji. 32Mt 3:16; Mk 1:10; Lk 3:22 Tena Yohana akashuhudia akisema, Nimemwona Roho akishuka kama hua kutoka mbinguni; naye akakaa juu yake. 33Lk 3:2; Mt 3:16Wala mimi sikumjua; lakini yeye aliyenituma kubatiza kwa maji, huyo aliniambia, Yeye ambaye utamwona Roho akishuka na kukaa juu yake, huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu. 34Mt 3:17Nami nimeona, tena nimeshuhudia ya kuwa huyu ni Mwana wa Mungu.
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza