Skip to main content

Hekima inayotuongoza Maishani

, Yehova ni Mtawala mwenye hekima? Njia moja yenye kuridhisha ya kujibu swali hilo ni kuchunguza mashauri anayotoa. Je, yanafanya kazi? Je, kuyatumia kunafanya maisha yawe mazuri zaidi na yenye kusudi? Mfalme Sulemani mwenye hekima aliandika mamia ya methali. Methali hizo zinazungumzia nyanja zote za maisha. Fikiria mifano kadhaa.
Kumtegemea Mungu. Ili kuwa na uhusiano mzuri pamoja na Yehova, lazima tumtegemee. Sulemani aliandika: “Mtegemee Yehova kwa moyo wako wote wala usitegemee uelewaji wako mwenyewe. Mtambue yeye katika njia zako zote, naye atanyoosha mapito yako.” (Methali 3:5, 6) Kumtegemea Mungu kwa kufuata mwongozo wake na kumtii hufanya maisha yawe na kusudi. Mtu anayefanya hivyo huufurahisha moyo wa Mungu na kumpa Yehova jibu la masuala yaliyozushwa na mpinzani Wake, Shetani.—Methali 27:11.
Kushughulika na watu wengine kwa hekima. Leo, kuliko wakati mwingine wowote, tunafaidika na shauri la Mungu kwa waume, wake, na watoto. “Ushangilie pamoja na mke wa ujana wako,” Mungu awashauri waume, akiwaagiza wawe waaminifu kwa wake zao. (Methali 5:18-20) Wanawake walioolewa wanaweza kufaidika na ufafanuzi wenye kupendeza ulio katika kitabu cha Methali kuhusu mke mwenye uwezo anayejipatia sifa kutoka kwa mumewe na watoto wake. (Methali, sura ya 31) Nao watoto wanaagizwa wawatii wazazi wao. (Methali 6:20) Kitabu hicho kinaonyesha kwamba urafiki ni muhimu, kwa kuwa kujitenga hutokeza ubinafsi. (Methali 18:1) Marafiki wanaweza kuwa na uvutano mzuri au mbaya, kwa hiyo tunapaswa kuwachagua kwa uangalifu.—Methali 13:20;17:17.
Kujitunza kwa hekima. Kitabu cha Methali kina mashauri mazuri kuhusu kuepuka matumizi yasiyofaa ya vileo, kusitawisha hisia zinazofaa na kuondolea mbali zisizofaa, na kuwa mfanyakazi mwenye bidii. (Methali 6:6; 14:30;20:1) Kitabu hicho kinaonya kwamba kutegemea akili ya mwanadamu na kupuuza shauri la Mungu hutokeza msiba. (Methali 14:12) Kinatuhimiza tumlinde yule mtu wa ndani, moyo wetu, dhidi ya uvutano mbalimbali usiofaa, na kutukumbusha kwamba katika moyo “ndiko zinakotoka chemchemi za uzima.”—Methali 4:23.
Mamilioni ya watu ulimwenguni wamejionea kwamba kuishi kupatana na mashauri hayo hufanya maisha yawe mazuri zaidi. Kwa sababu hiyo, wana sababu nzuri ya kumkubali Yehova kuwa Mtawala wao.
—Inatoka kwenye Kitabu cha Methali.

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....