Skip to main content

Kwa Nini Uichunguze Biblia?

Je, wewe unaifahamu Biblia? Hakuna kitabu kingine chochote katika historia ambacho kimesambazwa sana kama Biblia. Ujumbe wake umewafariji na kuwapa tumaini watu wa tamaduni zote, nao wamefaidika na mashauri yake maishani. Hata hivyo, watu wengi leo hawaijui Biblia vizuri. Iwe wewe ni mfuasi wa dini fulani au sivyo, huenda kuna mambo fulani ambayo ungependa kujua kuhusu Biblia.
KABLA ya kuchukua Biblia na kuanza kuisoma, ingefaa kujua mpangilio wake. Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vitabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo.
Biblia ilitungwa na nani? Hilo ni swali ambalo limewasumbua watu wengi. Ukweli ni kwamba Maandiko hayo yaliandikwa na wanaume wapatao 40 katika kipindi cha miaka 1,600 hivi. Hata hivyo, wanaume hao hawakudai kamwe kuwa watungaji wa Biblia. Mmoja wao aliandika: “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu.” (2 Timotheo 3:16) Mwandikaji mwingine alisema: “Roho ya Yehova ndiyo iliyosema kupitia mimi, na neno lake lilikuwa kwenye ulimi wangu.” (2 Samweli 23:2) Kulingana na waandikaji hao, Yehova Mungu ndiye Mtungaji wa Biblia naye anataka kuwa na uhusiano wa karibu na wanadamu.
Kuna jambo lingine muhimu linalohitajika ili kuielewa Biblia. Biblia ina ujumbe mmoja wa msingi: kutetewa kwa haki ya Mungu ya kuwatawala wanadamu kupitia Ufalme wa mbinguni. Katika broshua hii, utaona jinsi ujumbe huo unavyojitokeza kuanzia kitabu cha Mwanzo mpaka Ufunuo.
Ukiwa na hayo akilini, sasa chunguza ujumbe ulio katika kitabu maarufu zaidi ulimwenguni, Biblia.

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....