MITHALI 11:12
Asiye na akili humdharau mwenziwe; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.MITHALI 17:28 Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima; Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu.
Changamoto kubwa tuliyonayo ni kwamba tunataka kuongea kila wakati, tunataka kujibu kila tunachokisikia, kila tunachokiona tunataka kukisemea kitu.
Kuna wakati tunasikia na kukutana na mambo ambayo kiuhalisia moyo unagoma kabisa kunyamaza, unatamani ujibu, unatamani uwaambie watu yale umefanyiwa, unatamani uelezee vile umeumizwa lakini kumbe si kila jambo linatakiwa kuongelewa.Si kila ukionacho unatakiwa kukisemea kitu. Si kila usikiacho/uambiwacho ni lazima ujibu.Si kila ufanyiwacho ni lazima umwambie kila mtu.
MUHUBIRI 3:1 Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;Ipo nguvu katika kunyamazaYapo mambo ambayo tunapaswa kuongea, kusema, lakini yapo mambo ambayo tunapaswa kunyamaza kwa ajili ya usalama wa Roho zetu.
Ni kweli kuna wakati unasemwa sana vibaya, unasingiziwa, unatukanwa nk nk, lakini ni lazima ukumbuke kwamba kuna mazingira ambayo hupaswi kujibizana hata kama umeumia kiasi gani.Unajua ni kwanini?Ukisemwa vibaya, ukitukanwa, ukidharauliwa lazima moyo utaghafilika, moyo ukighafilika lazima utakuwa na hasira na ghadhabu.Ukiwa na hasira katu usitegemee kuwa utajadiliana na mtu kwa hekima.Ukiongea utaongea katika uwepo wa hasira, ukijibu utajibu kulingana na kiwango cha hasira ulichonacho.Sasa jiulize majibu yanayotoka kutokana na msukumo wa hasira huwa yanakuwaje?Mazuri? Ya upole? Ya hekima? Ya unyenyekevu? Namini kabisa jibu ni hapana.Kama jibu ni hapana that means utaongea vitu vibaya ambavyo ni chukizo kwa MUNGU kwa sababu amesema maneno yetu na yakolee munyu (chumvi).Sasa badala ya kuongea upumbavu na ukamkosea MUNGU kwanini usichague kunyamaza?Nimekuwa inspired sana na mwanamke Abigaili, ni kweli mumewe alikuwa na makosa, ni kweli alikuwa mlevi, lakini mwanamke huyu alijua ni wakati gani, na mazingira gani alipaswa kuongea na mumewe na alijua aongee nini. Alipomkuta mumewe yupo katika hali ya ulevi, ALINYAMAZA, alijua kuwa huu sio wakati wa kusema jambo lolote.1 SAMWELI 25:1Ni vyema sisi pia tukajifunza kusoma mazingira na nyakati na hali za watu zilivyo ili tujue ni wakati gani tujibu, tuongee nini na ni wakati gani
ZABURI 19:14 – Bwana na akafanye maneno yetu yakapate kibali mbele zake MUNGU na mbele za wanadamu pia.1 SAMWELI 25:36
kumbuka kwamba yupo mungu mwenye uweza wa kujibu na kuhukumu hapohapo katika maisha. imeandikwa kwamba kila mmoja atapimiwa kwa kiasi kilekile amabacho amewatendea wenzie.
MADHARA MAKUBWA YA KUSHINDWA KUNYAMAZA KATIKA MISHA
kushindwa kunyamaza kumesabisha asilimia kubwa ya migogoro na mafarakano makubwa katika jamii inayo tuzunguka.
Ningependa tujadili kwa mapana madhara hayo tujikita kwenye swala zima la mahusiano.
Hii imekuwa changamoto kubwa katika jamii
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza