Skip to main content

USHAURI KWA MABINTI

Moja  ya taswira ya kutambua kesho ya mwanamke yeyote katika ndoa yake ni kutambua msimamo wa awali. wapo mabinti ambao  wamepoteza waenzi wao kwa kushindwa kuwa na msimamo katika mahusiano yao. kwa maana nyingine tunasema wanavumishwa na wimbi la watu wakupita na ambao hwana mpango wowote wa kukuaa nao kimahusiano. tathimini inaonyesha kwamba asilimia kubwa ya wanawake ambao hawajaolewa na hawatarajii kuolewa wamekumbwa na tatizo hilo kutokana na kukoswa msimamo kipindi cha ubinti wao. 
  Jambo la kutambua ni kwamba unaposhindwa kuwa na msimamo lazima hadhi yako itashuka na kujikuta unakuwa mtu wakimatumizi katika upande wa wanaume. ipo haja ya kubadilika kama watoto wakike ili kuweza kutoa taswira chanya ya kesho. wanaume wanachohitaji kwa sasa ni umakini na msimamo wa mwanamke na siyo urembo wa mwanamke. japo kwa sasa wamebakia wanaume wachache wanaotumia kauli ya kwamba sura ndio kila kitu. 
kuna misingi maalumu amabayo unatakiwa kuitambua kama binti ili kujitengenezea mazingira mazuri ya kuwa mwanamke mwenye maono na mwenye kuonyesha taswira ya badaye.

TAZAMA HAPA KAMA UNA SIFA ZIFUATAZO  BASI UTAKUWA MKE MWEMA WA  BADAYE.

MKE MWEMA HUJAWA NA HEKIMA.

Wanawake wengi hawajui kuutumia ulimi vizuri – Ukali, maneno ya mikato, matusi, ukaidi n.k. kwao ni mambo ya kawaida. Wengi wanatawaliwa na HASIRA na WIVU, akiona mwanaume anaempenda anacheka na mwanamke ni Kosa la jinai, mwanamke anafura wala hata hawezi kuongea, hali ya hewa inabadilika hata mpaka marafiki wanatambua kuwa hali ni mbaya. Mwanamke anaepiga kelele na mgomvi bibilia imemwita mwanamke mpumbavu. “Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu.” (MIT. 9:13)
Ni vizuri kutofanya jambo kwa hasira na kuiruhusu hekima kukutawala
UVIVU SIO SEHEMU YA MAISHA YAKE.
Kuna wanawake ambao ni wavivu kupita kiasi hawawezi fanya jambo lolote wenyewe lazima kumtegemea dada wa kazi. Kila kitu huwa wanakua na sababu utasikia sipigi deki sababu kiuno kina mshituko, sifui nguo kucha zangu ni laini zinakatika, neno la Mungu linasemaje juu ya wanawake wa namna hii?
“Mtu mvivu husema, Simba yuko nje; Nitauawa katika njia kuu.” (MIT. 22:13)
Hawakosi sababu kwa kile wanachotakiwa kufanya,ili uwe mwanamke/mke mwema jifunze kujibiidisha na uache uvivu.

NI MSAFI, ANAYEJUA KUPANGILIA MAVAZI YAKE

Kuna wanawake ambao wanaamini wanaume wanaangalia tabia tuu. Sio kweli. Lazima avutiwe na wewe kwanza maana tabia haionekani kwa nje ni kitu cha ndani,so mwonekano wako ndio unaoweza kumfanya kutaka kujua tabia yako. Mwanamke/mke mwema anajua avae nini kwa wakati gani na anajua namna yakupangilia rangi za mavazi yake ili kuonekana akiwa na mvuto, Mwanaume anapomwangalia mwanamke anapata picha hata ya watoto wake watakavokua wanavalishwa. Sio tu mavazi hata mwili- ni vizuri kuwa msafi wa mwili sio kijasho cha hatari au harufu isiyo kuwa ya kawaida, kumbuka Mungu ndo anaangalia moyo ila mwanadamu anaangalia nje kwanza moyo badae kwa hiyo usafi wa mazingira na mwili ni jambo muhimu. “Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.”(1 TIM. 4:12)

ANATIMIZA MAHITAJI YA NDOA KWA MUME WAKE

Sulemani anasema mwanamke mwema “Taa yake haizimiki usiku.” Kuna wanawake wavivu kwa swala hili, pia kuna wanaopenda kulipiza visasi kwa kuwanyima waume zao huduma, utakuta wiki nzima mama anapanda kitandani huku amevaa “KOMBATI” utafikiri ni askari anaenda vitani. Wanaume ni sawa na mbuzi ambao hawachelewi kukata kamba wakikosa majani walipofungiwa. Fanya makosa yote, lakini usijefanya ujinga wa kumkomoa mume kwa kumnyima huduma ya ndoa, hilo ni kosa la Jinai. Hakikisha huduma hizo zinaboreshwa, nenda na wakati ili mradi isiwe kinyume na taratibu za Mungu.

ANAJUA KUPIKA CHAKULA KITAMU CHENYE KUFURAHIWA NA FAMILIA.

Wanawake wengi hasa wa siku hizi hawajui kupika, ndio maana utakuta wanaume wengi wanaishia kula hotelini au kwa mama ntilie, kama umetoka bara basi usione aibu kujifunza kwa watu wa pwani namna ya kuunga NAZI kwenye chakula. Akina mama ni wajibu wao kujifunza Mapishi, Mchicha peke yake unaweza kuwa na mapishi zaidi ya 10, wanaume wanapenda chakula chenye ladha “Taste”, mfanye mume akumbuke chakula cha nyumbani. Ni hatari mwanamke kuwaza ndoa wakati hata chai ukipika unaunguza

ANATAMBUA KUWA WIVU NA HISIA MBAYA NI ADUI WA NDOA YAKE.

Usitoe siri za ndoa yenu kwa mashoga au ndugu zako. Muda wote muombe Mungu akupatie hekima ya kuongea pindi tatizo linapotokea, Muombee mume wako ili Mungu amsaidie pia awe na Hekima ya kutunza ndoa kwa uadilifu na upendo, sio unaita watu nakuanza kusimulia madhaifu ya mumemo. “Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu. Hukaa mlangoni pa nyumba yake, Juu ya kiti mahali pa mjini palipoinuka, Apate kuwaita wapitao njiani, Waendao moja kwa moja katika njia zao. Kila aliye mjinga na aingie humu. Tena amwambia mtu aliyepungukiwa na akili,” (MIT. 9:13-16)

ANA HOFU YA MUNGU SIYO YA MUME

Ni hatari sana kuwa na mwanamke mwenye hofu ya mwanaume na siyo ya Mungu. Hofu ya Mungu itamfanya asifanye vitu kwa kificho maana anauhakika Mungu anaona kila sehemu, Mwanamke mwenye hofu ya Mwanaume ni janga maana machoni kwa mwanaume ni mwema kama kondoo akitoka hapo ni mbuzi mwenye pembe kali. Wakati mwingine wanaume wamekua wakijitia moyo watawabadilisha hao wanawake. Kama hakubadilika mkiwa rafiki usitegemee atabadilika ndoani.Mke akiwa mcharuko uwezekano mkubwa wa watoto kuwa kama mama ni mkubwa maana ndo anakuwa nao muda mrefu

MWENYE MATUMIZI MAZURI YA PESA

Hili ni jambo la msingi sana na wanawake wengi huwa hawajui wanaume wengi huwatega katika huu mtego na kuwapima. Siku zote usitake kukomoa kwasababu anaekununulia ni mwingine na sio wewe, mtu katolewa labda chakula cha jioni ataanza kuagiza vitu alivyokua anaviona kwa tv bila hata kujua bei yake mradi halipi yeye, au kama ni shoping atahakikisha kanunua kila kitu alichokuwaga anawaza maishani bila kujali gharama kwa alie mtoa. Lakini pia hata kama ni kwa hela yako mwenyewe jifunze kuwa na akiba. Ni aibu sana mwanamke/msichana mwenye zaidi ya miaka 20 kutokua na akaunti/fedha ya akiba.

HUJISHUSHA NA KUOMBA MSAMAHA

Ugomvi mwingi kati ya mwanaume na mwanamke au mume na mke mara nyingi hutokana na wote kutaka kua juu hakuna aliyetayari kushuka. Kumbuka mwanamke ndio mlinzi wa ndoa. Wakati mwingine kushuka kwako ndio kunaweza pelekea mume/mwanaume naye kuona makosa yake lakini kutojishusha mara nyingi huleta magomvi ambayo mwishowe huleta aibu “Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu; Bali hekima hukaa na wanyenyekevu.” (MIT. 11:2)

MWENYE MAWAZO YA KUENDELEZA FAMILIA.

Mwanamke mwenye upeo mpana wa kufikiri sio yule anaewaza namna ya kubadilisha ma dera, mwanamke mwema ni yule mwenye kukaa na kushauriana na mumewe juu ya mipango ya maendeleo na kumtia moyo mumewe juu ya mipango aliyonayo na sio kuwa kikwazo kwake na kumuonyesha kuwa hawezi kufikia malengo yake.



Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....