Jilazimishe kusamehe ili iwe rahisi kwako kusamehewa mbele za mungu. Kuna badhi ya watu wanashindwa kusamehe kabisa hata pale wenzao wanapojishusha kwa kuwaomba msamaha . Jambo la kujiuliza ni moja, Ni kwanini wao wasisamehe kama yesu mwenyewe awasamehe? . Lazima tubadilike na kuyafuata maandiko matakatifu.
Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza – Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17 ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza