Skip to main content

MAMBO YANAYO CHUKIZA WANAUME KATIKA FAMILIA

Moja ya vitu ambavyo vinakera wanaume wengi ni kurudi nyumbani, unataka kuingia ndani unakuta mlangoni kumejaa wanawake, sijui majirani sijui mashoga zake mkeo wanapiga stori.

Wengine wametandika na mkeka kabisa wanaongea kana bila wasiwasi wowote. Yaani ili kuingia ndani nilazima upite katikati yao. Unaingia ndani, labda mke alikupokea au hata hakukupokea lakini anatoka nnje kuendeleea na mazungumzo.

Lakini pia umewahi kurudi nyumbani, umeamua ukapumzike mara hodi, mara sijui naomba hiki, mara kile mara kile. Hamkai mkapumua washakuja kuangalia TV, sijui kuna tamthilia.

TV yako lakini huwezi hata kuangalia kwa uhuru, shoga yake kashikilia romoti. Mwisho wa wiki ndiyo kabisa, rafiki zake ni kujazana hapo nyumbani, wengine washenzi kabisa wanaingia na jikoni kupika.

Yaani wanajifanya kupendana sana (Wale ambao wanashona na sare kabisa) wanakuja wanakaa wanapiga stori, kupika na kucheka kila saa! Mwanaume unaamua tu kulala ndani au kujifanya una ubize kzaini.

Ndiyo hicho kitu kinakera sana, mwanamke punguza marafiki wa namna hiyo, utawapunguza kwa wewe kuacha kwenda kwao mara kwa mara, utawapunguza kwa wewe kutowaendekeza kuzoea nyumba yako.
Wao ni majirani tu, si sehemu ya ndoa yako, acha kuwafanya kama sehemu ya nyumba yako, mumeo anakwazika, labda hajawahi kukuambia anajifanya kufurahia lakini anachukia na inamkera sana. Sasa ni wajibu wako kuhakikisha kua hilo halitokei!
Hembu waambie marafiki zako, huu ni muda wa mume wangu, weekend ni kwaajili ya mume. Mume akufurahie afurahie kuwa na wewe awe na muda wa kuongea na wewe na si marafiki zako.
Sasa wewe waendekleze hao marafiki, siku mume akikuchoka na hata kumchukua mmmoja woa ndiyo unaanza kulialia wakati ulishatengeneza mwenyewe mazingira ya kuibiwa. Weka mipaka kati yako na marafiki zako!
www.tujenganemedia.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YANAYO KWAMISHA UFUGAJI

MAGWEIGA POULTRY INVESTMENT(wajasiriamali wa kuku na bidhaa zake) MAMBO YANAYOKWAMISHA WAFUGAJI WENGI.  Ufugaji ni rahisi ukitumia faida za mezani na kushuhudia watu wanafanya.  Hali hi inaweza ikawa tofauti ukianza wewe mwenyewe kwa vitendo.  Ni jambo gumu kiasi chake endapo mfugaji atapuza kanuni bora za Ufugaji.  Hapa mfugaji mpya anapaswa kujitathimini na kujipima kama anaweza kutoboa na kufikia matamanio yake kiufugaji.     Ufugaji ni kazi ngumu lakni imejawa na mafanikio kabambe na pia ni miongoni mwa furusa ambazo zipo wazi.  Ila vigezo na mashariti kuzingatiwa. kinacho kwamisha ufugaji kwa asilimia kubwa ni mambo yafuatayo . Mfugaji asipo yavalia njuga ataishia kwenye msongo wa mawazo na kujipa magonjwa ya moyo. Magweiga poultry investment 1. Magonjwa . Kipengele hiki kimekuwa changamoto kubwa sana kwa sisi wafugaji.  Yapo magonjwa changizwa  ambayo ni mfugaji mwenyewe anakubaliana na ugonjwa husika kutokea  ✔️ Typhoid...

KUWA NA MSIMAMO KWENYE MAISHA YAKO

Ulishawahi kujiuliza ni  kwanini watu wachache wanafanikiwa katika maisha huku wengi wakibakia masikini?  Ukweli ni kwamba sio kuwa wao wanasiri nyingi za kufanikiwa kuliko wewe bali ni misimamo thabiti waliojiwekea ili kuendana na ukuaji wa changamoto za maisha. Ni watu ambao wanafikiria vitu na mambo makubwa na kufanya vitu hivyo kwa msimamo bila kukubali kushindwa.  James William  (Harvard University ) aliwahi kusema kwamba " A human being can alter their lives by altering their attitude of mind" akiwa anamanisha kwamba binadamu yeyote anaweza kupunguza maisha yake kwa kupunguza musimamo wa fikira zake. Duniani kote utafiti unaonyesha kwamba rasirimali watu ndio nyenzo muhimu sana katika biashara yoyote yenye mulengo wa mafanikio.  Ila rasilimali hiyo ndio imekuwa ikipotea kila siku kutokana na watu kukoswa msimamo  (atttitude) Watu wanaweza kuwa asset kubwa sana katika maisha yako. Mafanikio yoyote hayapimwi kwa kipato ulichonacho bali pia ...

USIWE NA TAMAA KATIKA UFUGAJI.

  MADHARA YA TAMAA KATIKA UFUGAJI  Mfugaji yoyote ili aweze kuona faida ya ufugaji wake lazima aweke Tamaa pembeni.  Kuna utofauti kati ya Mfugaji mwenye Malengo na Mfugaji mwenye Tamaa.  Mfugaji mwenye Malengo hufanya muradi wake kwa uchache na kwa ufanisi, pia huweka ukomo wa kumiliki kuku kwa kiwango ambacho huweza kuwamudu na kumletea faida  Mfugaji mwenye Tamaa yeye kwake ukienda utakuta ana kuku 500 wa rika tofauti tofauti ambao hata kuwalisha ni mtihani kwake ila shida yake aonekane anamiliki kuku wengi japo faida yake ni 0%% Mfano : umeweka kuku 100 kroila  na umewakuza kwa shida hadi kufikia kutaga . Wanapoanza kutaga ni muda wa kuvuna mayai ili kurudisha garama zako.  Cha ajabu hapa utakuta Mfugaji anakurupuka kuingiza vifaranga wapya 200 kwa kutegemea hawa kuku 100 wahudumie vifaranga 200  hadi kufikia kutaga.   Pia hao kuku 100 wajiendeshe wao wenyewe kupitia mayai.  pia kuku 100 wahudumie familia. Ukweli ni kwamba itafi...