Skip to main content

MAMBO YANAYO CHUKIZA WANAUME KATIKA FAMILIA

Moja ya vitu ambavyo vinakera wanaume wengi ni kurudi nyumbani, unataka kuingia ndani unakuta mlangoni kumejaa wanawake, sijui majirani sijui mashoga zake mkeo wanapiga stori.

Wengine wametandika na mkeka kabisa wanaongea kana bila wasiwasi wowote. Yaani ili kuingia ndani nilazima upite katikati yao. Unaingia ndani, labda mke alikupokea au hata hakukupokea lakini anatoka nnje kuendeleea na mazungumzo.

Lakini pia umewahi kurudi nyumbani, umeamua ukapumzike mara hodi, mara sijui naomba hiki, mara kile mara kile. Hamkai mkapumua washakuja kuangalia TV, sijui kuna tamthilia.

TV yako lakini huwezi hata kuangalia kwa uhuru, shoga yake kashikilia romoti. Mwisho wa wiki ndiyo kabisa, rafiki zake ni kujazana hapo nyumbani, wengine washenzi kabisa wanaingia na jikoni kupika.

Yaani wanajifanya kupendana sana (Wale ambao wanashona na sare kabisa) wanakuja wanakaa wanapiga stori, kupika na kucheka kila saa! Mwanaume unaamua tu kulala ndani au kujifanya una ubize kzaini.

Ndiyo hicho kitu kinakera sana, mwanamke punguza marafiki wa namna hiyo, utawapunguza kwa wewe kuacha kwenda kwao mara kwa mara, utawapunguza kwa wewe kutowaendekeza kuzoea nyumba yako.
Wao ni majirani tu, si sehemu ya ndoa yako, acha kuwafanya kama sehemu ya nyumba yako, mumeo anakwazika, labda hajawahi kukuambia anajifanya kufurahia lakini anachukia na inamkera sana. Sasa ni wajibu wako kuhakikisha kua hilo halitokei!
Hembu waambie marafiki zako, huu ni muda wa mume wangu, weekend ni kwaajili ya mume. Mume akufurahie afurahie kuwa na wewe awe na muda wa kuongea na wewe na si marafiki zako.
Sasa wewe waendekleze hao marafiki, siku mume akikuchoka na hata kumchukua mmmoja woa ndiyo unaanza kulialia wakati ulishatengeneza mwenyewe mazingira ya kuibiwa. Weka mipaka kati yako na marafiki zako!
www.tujenganemedia.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....