Skip to main content
Mke au binti unayetarajia kuolewa lazima utambue kuwa mume wako anapokuoa pia Ana wazazi wake kama wewe na Ana ndugu zake Kama wewe, imekuwa kawaida kwa mke kutaka au kupenda na kufurahia pale Ambapo mume Wake kama Ana uwezo Kusaidia ndugu zake na wazazi wake lakini linapokuja suala La mume kutaka Kuwasaidia ndugu zake wengi huwa tunakasirika na hapo ndiyo tunaanza wengine kuonyesha rangi zetu halisi na makucha yeti, labda niwaulize kwani Kuna ubaya Gani mume akisaidia ndugu zake au wazazi wake na mbona kwenu mkisaidiwa hukatai na uwezo upo, wengine tunaenda Mbali zaidi mpaka mnachonganisha ndugu na mume wako au mume wako na wazazi wake wakati wewe ndiyo unatakiwa kuwa kiunganishi mzuri kwa ndugu wa mume wako  na wazazi tena wakati mwingine hata ukiona mume wako Anajisahau sana na kuwa bize na mambo ya familia tu ni muhimu kumkumbusha kuhusu kuwakumbuka wazazi hata kwa kuwatembelea hata kama wazazi wana uwezo pia wapelekeeni hata zawadi yoyote mtapata Baraka za wazazi pia, hata kama hupendi kukaa nao basi acha hata huko waliko awasaidie basi. Na hao unaowasaidi leo huwezi jua Watakuja kuwa nani na Watakuja kufanyika vipi kuwa msaada kwako au kwa watoto wako Maisha ni Mzunguko leo wewe unacho kesho hauna leo upo kesho haupo duniani. Yule ambaye leo hii unamfukuza hapo kwako au unamnyanyasa kesho ataweza kuwa mtu mwingine kabisa.

Kumbuka unapokuwa na roho mbaya kwa ndugu na hata wazazi wa mume wako Kuna mbegu mbaya Ambayo wewe kwa kujua au kutokujua unaipanda taratibu na itaota Ambayo itakuja kukugharimu siku moja kama sio kwako mwenyewe basi kwa watoto wako mwenyewe,

Na Ikumbukwe kuwa hata kama mtasaidia hao ndugu ni kwa muda tu na itakoma hata kama wanakaa hapo kwenu hawatakaa hapo milele Kuna kipindi nao Watakuwa na Maisha yao na nyumba zao na hata nyinyi hamtapungukiwa na kitu chochote kwakuwa hukuna lisilo na mwisho, kwa kuwa wakati mwingine Mungu analeta Baraka Ili uzitumie  na watu wengine pia kwa kufanya hivyo unakuwa unazuia mkondo wa Baraka kwenye nyumba yako na wengine baadaye mnashindwa hata kuwaendea hao ndugu kwa kuona aibu wanapokuwa wamefanikiwa mambo yanapowaendea kombo baadaye kwa sababu mkikumbuka mlivyowanyanyasa hao ndugu wa mume na kuwafanyia Roho mbaya lakini kwakuwa Mungu alikuwa na mpango mzuri na huyo ndugu hakukwama,  Usifikiri wewe ukiacha Kumsaidia huyo mtu atakufa au ndio itakuwa mwisho wake hapana Mungu atamuinulia mtu mwingine wa kumfikisha kwenye kanani yake. na wewe baadaye ikakuwia ngumu kwakuwa hukuwa umepanda mbegu njema.

Mimi mwenyewe hapa ni ushuhuda pia wa ninachokiongea Japo sitapenda kuongelea  hapa na nimepitia hayo pia hivyo naelewa  ilifika mahali nilikuwa napewa msaada kwa ajili ya Shule  na familia moja kwa kificho Ili mke asijue  nilikuwa ni lazima niende kazini kwa huyo baba au nikutane naye sehemu  au  akipata muda aje nyumbani kwetu kimya kimya Ili anipe hela ya ada au nauli  na kwakuwa kipindi hicho tulikuwa kwenye Mazingira magumu ya kuhitaji msaada, maana mke akijua  amani itatoweka nyumbani kwake kwa Kusaidia ndugu zake, na haya mambo bado kwenye nyumba zingine yanatokea hivyo tubadilike Wanawake Ili tupande mbegu njema na pia tujifunze katoka kwa wengine

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....