Mke au binti unayetarajia kuolewa lazima utambue kuwa mume wako anapokuoa pia Ana wazazi wake kama wewe na Ana ndugu zake Kama wewe, imekuwa kawaida kwa mke kutaka au kupenda na kufurahia pale Ambapo mume Wake kama Ana uwezo Kusaidia ndugu zake na wazazi wake lakini linapokuja suala La mume kutaka Kuwasaidia ndugu zake wengi huwa tunakasirika na hapo ndiyo tunaanza wengine kuonyesha rangi zetu halisi na makucha yeti, labda niwaulize kwani Kuna ubaya Gani mume akisaidia ndugu zake au wazazi wake na mbona kwenu mkisaidiwa hukatai na uwezo upo, wengine tunaenda Mbali zaidi mpaka mnachonganisha ndugu na mume wako au mume wako na wazazi wake wakati wewe ndiyo unatakiwa kuwa kiunganishi mzuri kwa ndugu wa mume wako na wazazi tena wakati mwingine hata ukiona mume wako Anajisahau sana na kuwa bize na mambo ya familia tu ni muhimu kumkumbusha kuhusu kuwakumbuka wazazi hata kwa kuwatembelea hata kama wazazi wana uwezo pia wapelekeeni hata zawadi yoyote mtapata Baraka za wazazi pia, hata kama hupendi kukaa nao basi acha hata huko waliko awasaidie basi. Na hao unaowasaidi leo huwezi jua Watakuja kuwa nani na Watakuja kufanyika vipi kuwa msaada kwako au kwa watoto wako Maisha ni Mzunguko leo wewe unacho kesho hauna leo upo kesho haupo duniani. Yule ambaye leo hii unamfukuza hapo kwako au unamnyanyasa kesho ataweza kuwa mtu mwingine kabisa.
Kumbuka unapokuwa na roho mbaya kwa ndugu na hata wazazi wa mume wako Kuna mbegu mbaya Ambayo wewe kwa kujua au kutokujua unaipanda taratibu na itaota Ambayo itakuja kukugharimu siku moja kama sio kwako mwenyewe basi kwa watoto wako mwenyewe,
Na Ikumbukwe kuwa hata kama mtasaidia hao ndugu ni kwa muda tu na itakoma hata kama wanakaa hapo kwenu hawatakaa hapo milele Kuna kipindi nao Watakuwa na Maisha yao na nyumba zao na hata nyinyi hamtapungukiwa na kitu chochote kwakuwa hukuna lisilo na mwisho, kwa kuwa wakati mwingine Mungu analeta Baraka Ili uzitumie na watu wengine pia kwa kufanya hivyo unakuwa unazuia mkondo wa Baraka kwenye nyumba yako na wengine baadaye mnashindwa hata kuwaendea hao ndugu kwa kuona aibu wanapokuwa wamefanikiwa mambo yanapowaendea kombo baadaye kwa sababu mkikumbuka mlivyowanyanyasa hao ndugu wa mume na kuwafanyia Roho mbaya lakini kwakuwa Mungu alikuwa na mpango mzuri na huyo ndugu hakukwama, Usifikiri wewe ukiacha Kumsaidia huyo mtu atakufa au ndio itakuwa mwisho wake hapana Mungu atamuinulia mtu mwingine wa kumfikisha kwenye kanani yake. na wewe baadaye ikakuwia ngumu kwakuwa hukuwa umepanda mbegu njema.
Mimi mwenyewe hapa ni ushuhuda pia wa ninachokiongea Japo sitapenda kuongelea hapa na nimepitia hayo pia hivyo naelewa ilifika mahali nilikuwa napewa msaada kwa ajili ya Shule na familia moja kwa kificho Ili mke asijue nilikuwa ni lazima niende kazini kwa huyo baba au nikutane naye sehemu au akipata muda aje nyumbani kwetu kimya kimya Ili anipe hela ya ada au nauli na kwakuwa kipindi hicho tulikuwa kwenye Mazingira magumu ya kuhitaji msaada, maana mke akijua amani itatoweka nyumbani kwake kwa Kusaidia ndugu zake, na haya mambo bado kwenye nyumba zingine yanatokea hivyo tubadilike Wanawake Ili tupande mbegu njema na pia tujifunze katoka kwa wengine
Kumbuka unapokuwa na roho mbaya kwa ndugu na hata wazazi wa mume wako Kuna mbegu mbaya Ambayo wewe kwa kujua au kutokujua unaipanda taratibu na itaota Ambayo itakuja kukugharimu siku moja kama sio kwako mwenyewe basi kwa watoto wako mwenyewe,
Na Ikumbukwe kuwa hata kama mtasaidia hao ndugu ni kwa muda tu na itakoma hata kama wanakaa hapo kwenu hawatakaa hapo milele Kuna kipindi nao Watakuwa na Maisha yao na nyumba zao na hata nyinyi hamtapungukiwa na kitu chochote kwakuwa hukuna lisilo na mwisho, kwa kuwa wakati mwingine Mungu analeta Baraka Ili uzitumie na watu wengine pia kwa kufanya hivyo unakuwa unazuia mkondo wa Baraka kwenye nyumba yako na wengine baadaye mnashindwa hata kuwaendea hao ndugu kwa kuona aibu wanapokuwa wamefanikiwa mambo yanapowaendea kombo baadaye kwa sababu mkikumbuka mlivyowanyanyasa hao ndugu wa mume na kuwafanyia Roho mbaya lakini kwakuwa Mungu alikuwa na mpango mzuri na huyo ndugu hakukwama, Usifikiri wewe ukiacha Kumsaidia huyo mtu atakufa au ndio itakuwa mwisho wake hapana Mungu atamuinulia mtu mwingine wa kumfikisha kwenye kanani yake. na wewe baadaye ikakuwia ngumu kwakuwa hukuwa umepanda mbegu njema.
Mimi mwenyewe hapa ni ushuhuda pia wa ninachokiongea Japo sitapenda kuongelea hapa na nimepitia hayo pia hivyo naelewa ilifika mahali nilikuwa napewa msaada kwa ajili ya Shule na familia moja kwa kificho Ili mke asijue nilikuwa ni lazima niende kazini kwa huyo baba au nikutane naye sehemu au akipata muda aje nyumbani kwetu kimya kimya Ili anipe hela ya ada au nauli na kwakuwa kipindi hicho tulikuwa kwenye Mazingira magumu ya kuhitaji msaada, maana mke akijua amani itatoweka nyumbani kwake kwa Kusaidia ndugu zake, na haya mambo bado kwenye nyumba zingine yanatokea hivyo tubadilike Wanawake Ili tupande mbegu njema na pia tujifunze katoka kwa wengine
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza