Moja ya kitu ambacho kinakimbiza wateja dukani kwako ni kupokea mteja huku umekaa. Kinaua mood ya wateja wengi sana. Mteja ni kama mgeni,a napokuja dukani kwako uchangamfu wako ndiyo utamfanya kununua. Hembu jiulize umeenda kwa rafiki yako, umefika anakukaribisha anakuacha sebuleni anaenda kupiga stori nnje na watu wengine utaruudi?
Sasa una duka mteja anakuja umekaa, anaulizia kitu flani umekaa unamuonyeshea kwa mkono tu au unamuambia ingia uangalie! Ndugu yangu labda kama unauza Oxygen kwamba nisiponunua nitakufa sirudi. Mteja akija kwako kwanza nyanyuka huku ukimkaribisha, akiulizia nguo flani nenda ishike, hata kama hutaki kuishusha lakini mgeukie muulize ni saizi gani, kama ni sahani muulize unataka rangi gani na chochote kile.
Unaponyanyuka kuna mambo mawili yanatokea, kwanza anahisi unamhehsimu, anaanza kujiona kuwa kumbe na yeye ni wa muhimu anaheshimiwa, lakini pili anaanza kuona aibu, anaona kuwa huyu nisiponunua nitakua nimemsumbua. Lakini pia kuna kitu cha tatu kinatokea na hiki ni chamuhimu zaidi, unaponyanyuka unamlazimisha kukaa dukani kwako kwa muda zaidi ili kuangalia vitu vingine.
Labda nikupe mfano tu, mteja kaja anaulizia una Lotion za Nivea, wewe huna kabisa, sasa kwa mtu ambaye hajui Biashara atasema sina akiwa kakaa anaendelea kuchezea simu yake akifuatilia sijui kama yale magari ni ya Zari au kakodi! Lakini kwa mfanyabiashara anajua kabisa kuwa hana Nivea ila atanyanyuka, ataenda kwenye shelfu la Lotion ataangalia kisha atasmea “Hizo zimetuishia ila tuna Nice and Lovely….”
Anageuka kidogo anamuangalia ngozi yake anauliza “Unapaka ya ngozi kavu au …” hapo mhusika hata kama haitaki lakini lazima akae kujibu lile swali kwakua umeuliza kistaarabu, ataangalia angalia na kutafuta kingine na hata asiponunua siku hiyo atarudi tena kwakua ulimuonyesha ukarimu. I;a mtu anakuja dukani, unakuta lijitu limenuna, au yuko bize na simu utafikiri kachanjiwa unaingia na kutoka hata hageuki halafu unaishia kusema “Huyu si mnunuaji?”
Yaani huwa nashangaa mtu mwingine analalamika wiki hajauza lakini anakuja huyo mtena mmoja anaacha kuweka simu pembeni akamhudumia unaacha kunyanyuka kumhudumia vizuri mpaka atamani kurudi tena! Kusimama mtena anapokuja kuna nguvu kubwa sana katika kumrudisha mteja, usijali ni wa namna gani simama tu hizo dakika tano ataona umemheshimu, fanya hivyo utanishukuru baadaye utakapotengeneza wateja wakudumu!
Sasa una duka mteja anakuja umekaa, anaulizia kitu flani umekaa unamuonyeshea kwa mkono tu au unamuambia ingia uangalie! Ndugu yangu labda kama unauza Oxygen kwamba nisiponunua nitakufa sirudi. Mteja akija kwako kwanza nyanyuka huku ukimkaribisha, akiulizia nguo flani nenda ishike, hata kama hutaki kuishusha lakini mgeukie muulize ni saizi gani, kama ni sahani muulize unataka rangi gani na chochote kile.
Unaponyanyuka kuna mambo mawili yanatokea, kwanza anahisi unamhehsimu, anaanza kujiona kuwa kumbe na yeye ni wa muhimu anaheshimiwa, lakini pili anaanza kuona aibu, anaona kuwa huyu nisiponunua nitakua nimemsumbua. Lakini pia kuna kitu cha tatu kinatokea na hiki ni chamuhimu zaidi, unaponyanyuka unamlazimisha kukaa dukani kwako kwa muda zaidi ili kuangalia vitu vingine.
Labda nikupe mfano tu, mteja kaja anaulizia una Lotion za Nivea, wewe huna kabisa, sasa kwa mtu ambaye hajui Biashara atasema sina akiwa kakaa anaendelea kuchezea simu yake akifuatilia sijui kama yale magari ni ya Zari au kakodi! Lakini kwa mfanyabiashara anajua kabisa kuwa hana Nivea ila atanyanyuka, ataenda kwenye shelfu la Lotion ataangalia kisha atasmea “Hizo zimetuishia ila tuna Nice and Lovely….”
Anageuka kidogo anamuangalia ngozi yake anauliza “Unapaka ya ngozi kavu au …” hapo mhusika hata kama haitaki lakini lazima akae kujibu lile swali kwakua umeuliza kistaarabu, ataangalia angalia na kutafuta kingine na hata asiponunua siku hiyo atarudi tena kwakua ulimuonyesha ukarimu. I;a mtu anakuja dukani, unakuta lijitu limenuna, au yuko bize na simu utafikiri kachanjiwa unaingia na kutoka hata hageuki halafu unaishia kusema “Huyu si mnunuaji?”
Yaani huwa nashangaa mtu mwingine analalamika wiki hajauza lakini anakuja huyo mtena mmoja anaacha kuweka simu pembeni akamhudumia unaacha kunyanyuka kumhudumia vizuri mpaka atamani kurudi tena! Kusimama mtena anapokuja kuna nguvu kubwa sana katika kumrudisha mteja, usijali ni wa namna gani simama tu hizo dakika tano ataona umemheshimu, fanya hivyo utanishukuru baadaye utakapotengeneza wateja wakudumu!
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza