Skip to main content

UTAJUAJE MTU ANAYE KUSARITI?

Kama mtu anachepuka au anakusariti lazima kutakuwa na dalili au viashiria  kadhaa kwake
Dalili za kujua mtu anaekusaliti
1. mwanandoa anayetoka nje ya ndoa hana muda wa kusikiliza familia ina tatizo au furaha gani. Anafafanua kuwa hiyo inatokana na muda wote kufikiria mambo ya familia nyingine hata kama ni ya mtu huko alikoanzisha uhusiano.
2. Kuchukia kushiriki tendo la ndoa
Anasema wengi wao hufanya mapenzi na wenza wao kwa kujilazimisha na wakati mwingine kulazimishwa kwa uwazi kabisa
3. mwenza anayetoka nje ya ndoa muda mwingi anakuwa mtu wa safari za ndani au za nje ya eneo analoishi.
4. anayechepuka anakuwa makini na simu zaidi ya kawaida, yupo radhi aende nayo bafuni, anakuwa makini asikamatwe anayochat kwenye simu.
5. kuchelewa kurudi nyumbani nk.
Tutaendelea kuangazia dalili mbalimbali za mtu anayekusariti
5. Kuongeza upendo ghafla: mwanaume anapoanza kutoka nje yandoa, kama ndoa yake haina vurugu , anaweza kuonesha upendo mkbwa hadi mkewe akashangaa na kujiuliza. Nafsi inamsuta mwanaume anajishtukia
6. Kuona kasoro nyingi za mke : kama mume anaanaza kuona kasoro nyingi za mkewe ambazo hapo nyuma alikuwa hazioni, basi ana lake jambo.
7. Mabadiliko ya kipato: Kuna wakati mabadiliko ya kipato yanaweza kuwa ni kiashirio cha mwanaume kutoka nje ya ndoa. Mwanaume anaweza kuwa na ajira ile ile au shughuli zilezile lakini ikaonekana kwamba kipato hakitoshi.
8 . Alama na harufu mpya: Kama mwanaume siyo makini sana, kupatikana kwa rangi ya mdomo kwenye shati au nguo zake za juu ni rahisi sana. lakini hata kama ni makini, harufu ya pafyumu tofauti na ile anayotumia mkewe inaweza kusikika sana kwenye nguo zake.
9. Mazungumzo ya simu: Kama mwanaume anaanza kuzungumza kwenye simu kwa kukatishakatisha au kusema tu,;nitakupigia baadae,' ama wakati mwingine kuonekana amebabaika baada ya kupokea simu, inaweza kuwa dalili. Kuna wakati anaweza kuwa anakata simu kila ikiita na kubadilika hata usoni kwa tahayari.
10. Mbele ya wanawake wengine: Tafiti nyingi zinaonesha kwamba, wanaume huchukua wanawake ambao wako karibu nao, au wamewazoea kwa njia ya kukutana mara kwa mara. Ni rahisi mwanaume kuwa na hawara ambaye ni jirani, mfanyakazi mwenzie, mshiriki wake kibiashara, rafiki wa familia, au hata mwanafunzi wake.Kwa hiyo mwanamke asijidanganye kwamba, kwa kuwa mwanamke fulani ni rafiki wa familia, ni jirani, ni mwanafunzi wa mumewe, hawezi kuwa na uhusiano naye, hapana. Kwa mwanaume, hao ni mawindo rahisi sana.

Tutaendelea badaye kidogo. Endelea kufuatilia makala zetu kila siku kwa mafunzo mbalimbali ya maisha
©Bahati Magweiga
Mshauri elekezi wa vijana na mahusiano
Simu namba 0757472165

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....