
Watu wengi hukosea katika mahusiano kwa kutokuwa wavumilivu pale wanapoachwa au kusaritiwa. Wengi huwahi sana kuingia kwenye mahusiano ikiwezekana siku moja baada ya kuachwa na mpenzi wake. Ukweli ni kwamba huwezi kupatia katika mahusiano kama hujafanyia kazi sababu na changamoto zilizo mfanya huyo mwanaume au mwanamke akukimbie .wengi husema lengo ni kuziba magepu na kupunguza stresi lakini ukweli ni kwamba baada ya mchungu kuisha utarudia makosa yale yale ya mwanzo. Unachotakiwa kufanya baada ya kusaritiwa au kukataliwa na mpenzi wako ni........
1. Jitathimini kwanza
2. Jifikirie kwa kina sana ili kubaini ukweli wa kusaritiwa au kukataliwa kwako.
3. Punguza jaziba na hasira zako kwani zinaweza kukufanya ukaumia zaid pale unapo ongea na aliyekusariti.
4. Punguza kumwambia kila mtu juu ya kuumizwa kwako
5. Jitahidi kusahau .
Ukizingatia hayo itakuwa rahisi sana kufika mbali kimahusiano na kufanya chaguo sahihi la mwenzi wako. Ukiendelea kuingia kwenye mahusiano kwa lengo la kuziba magepu au kupunguza stress huwezi kufikia malengo yako kimahusiano.
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza