MAHITAJI MUHIMU KABLA YA KUWEKA VIFARANGA BANDANI :
Unapotaka kuanza ufugaji wowote wa kuku lazima uwe na mahitaji muhimu ya kusaidia muradi wako ukuwe vyema na kuepukana na changamoto.
Miongoni mwa mambo muhimu ni kama vile.
1. Banda kulingana na idadi ya vifaranga unavyotaka kuweka. Usizidishe vifaranga katika banda moja ili kuepusha ukuaji hafifu na matatizo mengine kama vile kudonoana. Hakikisha banda limezingatia kanuni zote za ujenzi ikiwemo
✔️uelekeo wa upepo
✔️upauwaji wa paa
✔️uelekeo wa maji yani lisiwe katika mkondo wa maji
✔️Hewa iingie na kutoka kwa usahihi ili kuzuia mambukizi zaidi ya magonjwa pale yanapokuwa yametokea.
2. Vyombo vya chakula na maji kulingana na Idadi sahihi ya vifaranga. Kwa mfano vifaranga 100 wanahitaji Vyombo 3 vya maji na vitatu vya chakula ndani ya siku 30 mpaka 45
3. Vyungu joto au taa za umeme za kulelea vifaranga
4. vitaru vya kulelea vifaranga endapo banda ni kubwa. Unaweza kutengeneza buruda ili kusaidia kuzuia upotevu wa joto bandani na usambaaji wake.
5.Dawa za kuanzishia ( Neoxchick )
6. Glucose . endapo vifaranga watakuwa wametoka umbali mrefu wanatakiwa kupewa glucose kwa masaa 3 ili kuwaongezea nguvu na kuchangamka kwajili ya kuanza kula.
Katika mchanganuo huu hakuna sehemu nimetaja madawa yenye mlengo wa kutibu magonjwa. Sio rahisi kuzungumzia madawa kwa sababu huwezi kufahamu vifaranga wataumwa nini na watatumia dawa zipi na watapona baada ya muda gani.
Kuna wakati vifaranga wanaumwa na kujikuta wametumia dawa zaidi ya 3 kwenye ugonjwa mmoja kulingana na ukubwa wa tatizo.
Jambo la muhimu ni usimamzi bora na kufuata sharia zote za ufugaji.
Pia Elimu dhidi ya utambuzi wa magonjwa na kinga dhidi ya magonjwa ni muhimu zaidi kuwa nayo.
Jenga utaratibu wa kukagua maendeleo ya vifaranga wako Mara kwa Mara ili ubaini changamoto zikiwa katika hali ya kawaida ambayo Unaweza kukabiliana nayo.
Niwatakie ufugaji mwema na siku njema.
By Bahati magweiga.
Wasiliana Nami kwa huduma zetu za vifaranga wa siku 1 aina ya kroila.
0757472165
0786155188
E-mail bahatichacha698@gmail.com
Pia Tunatoa mafunzo ya kutotolesha vifaranga kwa kutumia mabox ambayo huduma hiyo hufanyika online kwa garama nafuu kabisa. Tupo kibaha pwani.
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza