MAANDALIZI KWAJILI YA VIFARANGA NA MAMBO MUHIMU SIKU 30 ZA MWANZO.
By Magweiga bahati
bahatichacha698@gmail.com
📞+255757472165
📞+255786155188
ukitaka kuwa mfugaji mzuri na mwenye kujenga uzoefu mzuri katika ufugaji huna budi kuanza na vifaranga. Changamoto mbalimbali za uleaji wa vifaranga ndio uhalisia wa kuku katika magonjwa, ukuaji na mambo mengine yanayo mhusu. Upo utofauti mkubwa wa uelewa kati ya mtu ambaye ameanza kumfuga kuku tangu kufaranga hadi kutaga kisha kuuzwa na yule ambaye ameuziwa kuku wakiwa wakubwa.
Aliyeuziwa kuku wakubwa anakuwa na changamoto chache za kutatua kuliko yule mkuzaji wa huyo kuku tangu kufaranga. Hata katika uchambuzi wa changamoto zinazohusiana na kuku Anakuwa na uwanja mdogo wa kuzungumzia kuku kiundani.
Asilimia kubwa ya watu hupenda kuwa wafugaji lakini hawataki kupita katika mchakato wa kulea vifaranga. Wengi huamini kukuza vifaranga ni kazi ngumu bora kununua wakubwa. Dhana hi kitaalamu tunaita upungufu wa maarifa /kukosa uvumilivu au uhitaji wa maendeleo ya haraka yasio na tija.
Sasa Tuangazie mambo muhimu katika maandalizi ya kuwapokea vifaranga.
- Hakikisha banda limejengwa kwa kufuata kanuni bora za ujenzi wa mabanda kama vile uelekeo wa upepo, mkondo wa maji au lisiwe katika sehemu yanakopita maji, uwezekaji sahihi wa paa, nk.
- Hakikisha unaweka oda kulingana na idadi sahihi ya vifaranga ambao wanatakiwa kukaa kwenye banda hilo kulingana na square meters pendekezwa. Epuka kauli za kusema kwamba naagiza 250 kisha unajianda kwamba hata wakifa 50 utabaki na 200. Ukweli ni kwamba siku wakianza kufa utabaki na 50. Agiza vifaranga ukiwa na imani kwamba wote watakuwa vyema. Usijipangie idadi ya vifoo kabla hata ya kuanza kufuga. ( Mungu wetu halali wala hasinzii )
- Kama banda ni kubwa tengeneza bruda ndani yake ili kuzuia upotevu wa joto bandani au kuchukua muda mrefu joto kusambaa bandani . Kitendo hiki kitawafanya vifaranga wakue taratibu na pia ulaji hautakuwa sawia kwa sababu hutumia muda mrefu kujikunyata . Joto ni muhimu sana Kwa vifaranga ndani ya siku 30 za mwanzo. Huwasaidia vifaranga kuota manyoa Kwa haraka na kukua vyema. Zingatia kiwango cha joto kulingana na majuma sahihi ya vifaranga. Joto hupunguzwa kadiri majuma yanavyo ongezeka pamoja na ukuaji wa vifaranga. Epuka mkaa unaotoa moshi kwani huongeza hewa chafu bandani.
- baada ya kuandaa vitaru na kuviwekea vyanzo vya joto, hatua inayofuata ni kuandaa vyombo vya maji kwa idadi sahihi ya vifaranga. Kagua vyombo na kuvisafisha kwa maji na sabuni hata kama vipya. Hakikisha vyombo vya chakula na Maji vina vibanio ili kuepusha kumwaga maji bandani.
- wape vifaranga maji ya dawa ya kufunga vitovu neoxychic formula baada ya kuwapokea. Ikiwa vifaranga wametoka umbali mrefu wapewe glucose kwa masaa mawili kisha waendelee na maji ya dawa. Epuka kujichanganyia dawa hovyo kama vile Neochick na oxyfarm nk.
- Hakikisha wewe mwenyewe upo safi wakati wa kupokea vifaranga. Epuka kutumia nguo za kuhudumia kuku wakubwa au ulizokuwa ulizunguka nazo wakati wa kuwapokea vifaranga. Wakague vifaranga vizur na kuwaingiza bandani.
- Mabokisi yaliotumika kubeba vifaranga yasiingizwe bandani bali yaishie njee kwani yanaweza kukuachia vimelea bandani na kukuletea magonjwa. Kadharika usiruhusu aliyekuletea vifaranga kuingia bandani kwako hata kama unamfahamu
Siku 1-5.... Neochick
Siku 6……maji ya kawaida
Siku ya 7..... Chanjo ya Newcastle
siku ya 8 ….maji ya kawaida
Siku ya 9-12… Maji yenye vitamini
Siku ya 13 maji ya kawaida
Siku ya 14 . Chanjo ya gombolo
Siku ya 15 maji ya kawaida
Siku ya 16-19 maji ye Vitamini
Siku ya 21 chanjo ya gombolo
Siku ya 22 maji ya kawaida
Siku ya 23-26 wape vifaranga maji ya vitamini
siku 27 wape maji ya kawaida siku ya 28 wape chanjo ya Newcastle.
Siku ya 35 mpaka 42 wape chanjo ya ndui.
9. Hakikisha unachakula chao cha kutosha ndani ya siku 30. Vifaranga wapewe chakula bora chenye virutubisho ili kuwasaidia kuimarisha mifupa pamoja na Kinga ya mwili kwa haraka ndani ya siku 30. Epuka uchanganyaji holela wa chakula cha vifaranga kwani utakuletea matatizo mkubwa kama vile
✔️ulemavu wa muguu
✔️kudumaa kwa vifaranga
✔️kuvimba macho na kupofuka kabisa
✔️magonjwa ya Mara kwa Mara bandani
✔️kudonoana na kulana hovyo kwa sababu ya upungufu wa vini rishe katika chakula chao. Vifaranga waanze kuchanganyiwa chakula baada ya siku 30 mpaka 60
Fuatilia maendeleo ya vifaranga wako kwa ukaribu ili kubaini kama
✔️ wanakula wote
✔️wanatawanyika na kusambaa vyema katika banda au bruda. Ikiwa wanajikusanya kwenye pembe za banda jua kwamba joto halipo sawia. Hakikisha unauwa hizo kona za banda kwa kutumia kitu chochote kwani asilimia kubwa ya vifaranga hujikusanya kwenye kona na kulalina kisha kukosa hewa na kupelekea vifoo.
✔️ Wana dalili za ugonjwa wowote ili iwe rahisi kwako kutubu mapema kabla haujawa mkubwa.
✔️ Fuatilia sana vinyesi vyao na muonekano wao bandani. Hi itakusaidia kujua kama kuna magonjwa nyemerezi kama vile
Prolium
Salmonella
Coccidiosis
Flow chorela nk
Kukiwa kuna mambukizi yoyote yanayo kutatiza muone dakitar aliopo karibu na wewe kwa msaada na ushauri Zaid.
🍇Hakikisha vifaranga wanapewa chanjo zote kwa wakati. Vifaranga wagonjwa wasipewe chanjo mpaka watakapo kuwa wamepona. Tibu kwanza vifaranga wako wapone ndio uwape chanjo. Hapa inatakiwa umakini sana. Unatakiwa kujiridhisha siku Tatu kabla kuwa vifaranga wako Hawa magonjwa yoyote kisha ndio uchukue hatua ya kuwapa chanjo. Zingatia uhifadhi wa chanjo kutoka dukani hadi kwako . Chanjo dhaifu haifai kwani badaye inaweza kusababisha changamoto kwa vifaranga.
🍇Hakikisha vyombo vya chakula na maji vinatosheleza kwa idadi ya vifaranga. Hii itakusaidia kupata ukuaji ulio sawia( uniform) kwa vifaranga. Vyombo vikiwa vichache kuna badhi ya vifaranga watakula wa mwisho na chakula kichache.
🍇Hakikisha vifaranga ambao wana dalili za magonjwa wanatengwa na wenzao kisha kuhudumiwa wa mwisho. Fuatilia vyema na kubaini aina ya ugonjwa, chanzo chake na tiba sahihi kulingana na ukubwa wa tatizo.
🍇Epuka utoaji dozi kiholela kwa vifaranga kwani badhi ya dawa zinakuwa nzito kwa vifaranga na kupelekea stress pia jambo hili linaweza kusababisha usugu wa madawa katika vifaranga. Onana na dakitari wa mifugo kwa ushauri zaidi.
🍇Unapo changanya dawa mbili hadi Tatu kutibu ugonjwa hakikisha unafahamu kiundani zinatibu nini na chemical concentration zake zinahusiana vipi. pia kuna muhimu wowote kufanya hivyo. Kuna badhi ya dawa hazitakiwi kuchanganywa na yoyote.
Kwa uhitaji wa vifaranga bora vya kroila wasiliana nasi kupitia namba zilizopo katika makala hi. Bei ya kifaranga ni shilingi 1500/=
Tupo kibaha pwani na mikoani tunakufikia kwa uwaminifu mkubwa. 0786155188
Magweight poultry investment. Wafugaji, wazalishaji na wauzaji wa kuku rika tofauti. Pia mayai ya layers na kroila yanapatikana
Asante niwatakie ufugaji mwema
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza