Skip to main content

SIRI KADHAA ZA KUFANIKIWA :



   
Mafanikio ni haki ya kila mmoja wetu na ni kitu ambacho kinawezekana kwa kila mmoja.  Watu wamekuwa wakichukuria neno mafanikio kama ajari (accident ) . Ila ukweli mafanikio siyo ajari bali ni matokeo ya misimamo yetu na misimamo yetu ni munganiko wa uchaguzi wa mambo ambayo tunayamini kuwa ndio sahihi.  Kwa maana nyingine Tunasema kwamba mafanikio ni mamzi (choice ) na siyo  nafasi.  Katika maandiko tunasema mafanikio ni neema ambayo kila mmoja wetu anakeremiwa na mungu kwa kadri anavyotumikia na kuifanyia kazi neema hiyo.  Na kila mmoja wetu amejaliwa neema hiyo na mungu hata kabla hajamuleta hapa duniani.
Kabla ya kuendelea mbele hebu tuangalie kwanza utofauti kati ya mtu mwenye kiu ya mafanikio na ambaye amekata tamaa za kufanikiwa.  Kwa maana nyingine Tunasema WINNERS  VS  LOSERS. 

1. Mshindi muda wote anakuwa ni mtatuzi wa matatizo  ( problem solver and answers  finder)  . Watu washindi na wa pambanaji katika kufikia mafanikio yao muda wote huwa ni sehemu ya kutafuta majibu na kutatua matatizo yanayowakabili.  Ila kwa mtu ambaye amekata tamaa  (losers ) wao huwa ni sehemu ya kutengeneza matatizo katika jamii. 

2. Mshindi siku zote anaongoza maisha yake kwa malengo  (plan )  Ila washindwa hubaki kuwa watu wa kugairigairi mipango yao.  Kwa maana nyingine ni watu wa siyo weza kusimamia mipango yao wenyewe.  Au kwa upande mwingine tunasema ni watu amabao wanajiongoza kwa kufuata mkumbo wa watu wengine. 

3. Mshindi katika maisha siku zote hupenda kufanya kitu kwa ajili ya watu wengine  ila walioshindwa hupenda kukatisha tamaa juu ya mambo mazuri yanayofanywa na watu wanaotumikia neema zao ipasavyo. 
Kwa maana nyingine hutumia neno kwamba hiyo siyo kazi yangu.

4.mshindi (winner) muda wote huona majibu ya matatizo wakati huo mshindwa  (losers ) yeye huona matatizo pekee. 

5.  Washindi siku zote huwa ni wale amabao wanasamehe na kusamehe wenyewe juu ya mlolongo mzima wa maisha yao. Kwa maana nyingine tunasema ni watu wasiyoweza kabisa kukaa na mambo mabaya nafsini mwao.  Washindwa  (losers ) huamini kwamba visasi ndio njia pekee ya kufikia mafanikio yao. Hawa ni watu amabao hutunza vitu ambavyo vimekwisha kupita nyuma. Kwa maana nyingine Tunasema kwamba hawa ni watu ambao kwao hawana tabia ya kusamehe na kujivika yalio mema. 

6. Mshindi siku zote  huchagua kile wanacho Sema kwa upande mwingine tunasema huchanganua . Wakati huo mshindwa husema kile walichochagua bila kuchanganua. 

7. Mshindi yeye jambo hili ni gumu lkn litawezekana wakati huo mshindwa  ( losers ) yeye anasema jambo hili linawezekana ila ni gumu.

8. Mshindi siku zote hufanya kitu ili kitokee na mshindwa husubiri kitu kitokee. Kwa namna nyingine ni mtu anayesubiri miujuza itokee ili afanikiwe katika maisha yake.  

Hiyo ni badhi ya tofauti chache ambazo pia zitakusaidia kujiPima upo katika kundilipi hasa katika upande wa kupigania ndoto zako.
Ili uweze kufanikiwa katika maisha yako kuna siri kadhaa za kupitia na ambazo zitakufanya uwe tofauti katika jamii. 
1. Jiamini kuwa unaweza kufikia malengo yako.  Kujiamini na kuamini ni moja ya siri kubwa katika kufikia mafanikio yako. Usipokuwa na ujasiri pamoja na Imani huwezi kufikia mafanikio yako kamwe.

2. Chagua marafiki wenye maono. Jambo ambalo watu wengi hukosea ni kwenye uchaguzi wa marafiki katika maisha yao. Rafiki ana msukumo mkubwa katika kubomoa ndoto zako au kukusogeza mbele kimafanikio.   
Kwa mfano unachagua marafiki ambao hutumia muda mwingi kujadili anasa  kwamwe hawawezi kukusaidia katika kufika kule ulikokusudia. 

3. Tengeneza mipango sahihi  (plan). Huwezi kufanikiwa kwa kutaka kufanya mambo yote kwa wakati mmoja.  Maana ya kuweka mipango ni kukusaidia kuweka kipaumbele katika mambo ya msingi.  Ukisema uendeshe maisha bila mipango lazima uataona kipato chako ni kidogo na hakitoshi kukufikisha u endapo. 

4. Jifunze kuheshimu fedha.  Kwa maana nyingine Tunasema lazima uwe na nidham ya kuitumia pesa.  Kuna watu ambao kwao pesa hazikai kwenye akaunti zao . Hawa ni watu ambao wanapenda starehe ambazo majuto yake ni makubwa kwa badaye.
5. Jenga ukomavu wa fikira 
Fikira chanya ni nyenzo thabiti katika kufikia mafanikio yako.  Kuwa mtu wa kutafuta maarifa na ujuzi uliosahihi kupitia kusoma vitabu au njia yoyote iliosahihi.

Hizo ni badhi ya siri kadhaa za mafanikio  japo zipo nyingine nyingi.  
Ili kuendelea kupata makala nyinginezo,  endelea kuifanya blog hii kuwa sehemu yako ya maarifa. 
Share makala hii katika marafiki zako kwenye mitandao yote ya kijamii ili na wao tuweze kwenda sambamba

Watu wasiyo kuwa na malengo mara nyingi hupenda sana kutumia maneno haya

1)Sina mtaji
2)Sina Connection
3)Nitaanza rasmi kesho
4)Mimi ni wa hivihivi tu
5)Mifumo mibovu ya Serikali ndiyo inayonirudisha nyuma
6) Mke/mme/ndugu zangu Ndiyo walioniangusha/kunitenda/kikwazo
7)Kupata ni majaliwa
8)Usilazimishe mambo
9)Kuna watu special siyo mimi.
10)Sina bahati
11) kupata si uhodari nami nitapata tu.
12) Mimi ni fungu la kukosa tu.
13) muda wangu bado nitapata tu
14) mungu hajapanga hata vidole mkononi havilingani.
15) wapo waliopangiwa sisi wasindikizaji
16) Familia yetu hakuna tajiri nianze mimi?
17) hata wanaotafuta mbona wapo vilevile...fulani namjua mbona yupo tu kama mimi au namzidi.
18)Rais anabana sana

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....