Skip to main content

NG'AMUA HAYA NA UCHUKUE HATUA KABLA YA YEYE KUFANYA HIVYO

DALILI ZA MTU ANAYETAKA KUKUACHA.
.
Sio kila mtu ana uwezo wa kukufata au kukupigia simu na kukuambia live kuwa hakutaki, muachane, wengi hawawezi kuwa kauzu hivyo na kuamua kutumia njia zingine ambazo kwa kiasi kikubwa zitakuumiza, kutesa, au kusababisha malalamiko/ugomvi unaoweza mpa sababu ya kuachana na wewe.
Zifuatazo ni dalili za mahusiano yanayokaribia kufa.
.
1: MABADILIKO YA TABIA: Mara nyingi mtu anapokua amekuchoka huwa anaanza kujenga tabia za ajabu ajabu, ambazo zitakufanya ukose usingizi, ukose raha ya maisha au hata kusababisha mitafaruku ya mara kwa mara. Mfano: Usaliti wa mara kwa mara na muda mwingine ni wa wazi wazi, gubu, kisirani, kukosoa kosoa bila sababu, kuchelewa kurudi, jeuri, dharau*kejeli, kukupiga mara kwa mara.
.
2: KUPUNGUZA MAWASILIANO: Hii ndo huwa jambo kubwa hasa kwa wenye mahusiano yaliyo nje ya ndoa na ndani ya ndoa. Mlizoeana kuchat asubuhi mpaka usiku, kupigiana simu mara kwa mara. Lakini ghafla unaona ile kasi inapungua, story, ushauri, vichekesho, alivyokuwa akikupa wakati wa maongezi yenu unashangaa vinakufa ghafla. Message mbili anakuaga, hakuna kuchekeshana, wala kushauriana.
.
3: KUTOKUPA KIPAUMBELE: Hiki ndo kipindi ambacho utampigia mara 10, utapokelewa mara moja. Utatuma message WhatsApp hata kama yuko online, hatojibu kwa wakati. Usishangae kukawa na party, na usialikwe.
.
4: KUONGEZEKA KWA VISINGIZIO: Mara nyingi mtu anapokuchoka huwa anakosa hamu ya kuongea, kuchat, kuonana, kula, hata kukaa na wewe. Usishangae sana mumeo kuanza kila akirudi nyumbani kukwambia "Anh nimeshiba", "Nimechelewa kurudi, kazi nyingi", au mpenzi wako "Baby sijaja mama alinituma sehemu ", "Dah mishe zinabana ndomana sijakutafuta".
.
5: KUTOKUJALI TENA: Hiki ndo kipindi ambacho unaongea na mkeo, yeye anakupa mgongo. Ule usile, utosheke chumbani usitosheke, ulale usilale, uumwe usiumwe, wala hana muda na wewe.
.
6: KUFA KWA UPENDO&MAHABA: Utaanza kuona mabadiliko, zile nakupenda, kusifiana, kucheza pamoja, kulishana, mabusu motomoto, kubebana, kudekezana, kutoka wote pamoja, kucheka pamoja, kula pamoja, mechi za kufa mtu, vyote utaona vinapungua kimoja baada ya kingine.
.
7: MABADILIKO KWENYE TENDO LA NDOA: Mara nyingi mtu anapoanza kujenga chuki dhidi yako, huwa anaanza kukosa hamu/hisia juu yako. Hivyo hata kama hana michepuko, huwa anakosa ile hamu ya kufanya na wewe tena. Lakini kama anayo michepuko, huwa anamaliza hamu zake huko huko, wewe unawekwa kando, au hata mkifanya inakuwa kama kajilazimisha kufanya, hivyo anaweza akaishia njiani kutokana na uchovu alionao baada ya kuhudumia michepuko, au kutokana na kukosa hamu ya kufanya na wewe.
.
Tutaendelea na uchambuzi. .......

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....