DALILI ZA MTU ANAYETAKA KUKUACHA.
.
Sio kila mtu ana uwezo wa kukufata au kukupigia simu na kukuambia live kuwa hakutaki, muachane, wengi hawawezi kuwa kauzu hivyo na kuamua kutumia njia zingine ambazo kwa kiasi kikubwa zitakuumiza, kutesa, au kusababisha malalamiko/ugomvi unaoweza mpa sababu ya kuachana na wewe.
Zifuatazo ni dalili za mahusiano yanayokaribia kufa.
.
1: MABADILIKO YA TABIA: Mara nyingi mtu anapokua amekuchoka huwa anaanza kujenga tabia za ajabu ajabu, ambazo zitakufanya ukose usingizi, ukose raha ya maisha au hata kusababisha mitafaruku ya mara kwa mara. Mfano: Usaliti wa mara kwa mara na muda mwingine ni wa wazi wazi, gubu, kisirani, kukosoa kosoa bila sababu, kuchelewa kurudi, jeuri, dharau*kejeli, kukupiga mara kwa mara.
.
2: KUPUNGUZA MAWASILIANO: Hii ndo huwa jambo kubwa hasa kwa wenye mahusiano yaliyo nje ya ndoa na ndani ya ndoa. Mlizoeana kuchat asubuhi mpaka usiku, kupigiana simu mara kwa mara. Lakini ghafla unaona ile kasi inapungua, story, ushauri, vichekesho, alivyokuwa akikupa wakati wa maongezi yenu unashangaa vinakufa ghafla. Message mbili anakuaga, hakuna kuchekeshana, wala kushauriana.
.
3: KUTOKUPA KIPAUMBELE: Hiki ndo kipindi ambacho utampigia mara 10, utapokelewa mara moja. Utatuma message WhatsApp hata kama yuko online, hatojibu kwa wakati. Usishangae kukawa na party, na usialikwe.
.
4: KUONGEZEKA KWA VISINGIZIO: Mara nyingi mtu anapokuchoka huwa anakosa hamu ya kuongea, kuchat, kuonana, kula, hata kukaa na wewe. Usishangae sana mumeo kuanza kila akirudi nyumbani kukwambia "Anh nimeshiba", "Nimechelewa kurudi, kazi nyingi", au mpenzi wako "Baby sijaja mama alinituma sehemu ", "Dah mishe zinabana ndomana sijakutafuta".
.
5: KUTOKUJALI TENA: Hiki ndo kipindi ambacho unaongea na mkeo, yeye anakupa mgongo. Ule usile, utosheke chumbani usitosheke, ulale usilale, uumwe usiumwe, wala hana muda na wewe.
.
6: KUFA KWA UPENDO&MAHABA: Utaanza kuona mabadiliko, zile nakupenda, kusifiana, kucheza pamoja, kulishana, mabusu motomoto, kubebana, kudekezana, kutoka wote pamoja, kucheka pamoja, kula pamoja, mechi za kufa mtu, vyote utaona vinapungua kimoja baada ya kingine.
.
7: MABADILIKO KWENYE TENDO LA NDOA: Mara nyingi mtu anapoanza kujenga chuki dhidi yako, huwa anaanza kukosa hamu/hisia juu yako. Hivyo hata kama hana michepuko, huwa anakosa ile hamu ya kufanya na wewe tena. Lakini kama anayo michepuko, huwa anamaliza hamu zake huko huko, wewe unawekwa kando, au hata mkifanya inakuwa kama kajilazimisha kufanya, hivyo anaweza akaishia njiani kutokana na uchovu alionao baada ya kuhudumia michepuko, au kutokana na kukosa hamu ya kufanya na wewe.
.
Tutaendelea na uchambuzi. .......
.
Sio kila mtu ana uwezo wa kukufata au kukupigia simu na kukuambia live kuwa hakutaki, muachane, wengi hawawezi kuwa kauzu hivyo na kuamua kutumia njia zingine ambazo kwa kiasi kikubwa zitakuumiza, kutesa, au kusababisha malalamiko/ugomvi unaoweza mpa sababu ya kuachana na wewe.
Zifuatazo ni dalili za mahusiano yanayokaribia kufa.
.
1: MABADILIKO YA TABIA: Mara nyingi mtu anapokua amekuchoka huwa anaanza kujenga tabia za ajabu ajabu, ambazo zitakufanya ukose usingizi, ukose raha ya maisha au hata kusababisha mitafaruku ya mara kwa mara. Mfano: Usaliti wa mara kwa mara na muda mwingine ni wa wazi wazi, gubu, kisirani, kukosoa kosoa bila sababu, kuchelewa kurudi, jeuri, dharau*kejeli, kukupiga mara kwa mara.
.
2: KUPUNGUZA MAWASILIANO: Hii ndo huwa jambo kubwa hasa kwa wenye mahusiano yaliyo nje ya ndoa na ndani ya ndoa. Mlizoeana kuchat asubuhi mpaka usiku, kupigiana simu mara kwa mara. Lakini ghafla unaona ile kasi inapungua, story, ushauri, vichekesho, alivyokuwa akikupa wakati wa maongezi yenu unashangaa vinakufa ghafla. Message mbili anakuaga, hakuna kuchekeshana, wala kushauriana.
.
3: KUTOKUPA KIPAUMBELE: Hiki ndo kipindi ambacho utampigia mara 10, utapokelewa mara moja. Utatuma message WhatsApp hata kama yuko online, hatojibu kwa wakati. Usishangae kukawa na party, na usialikwe.
.
4: KUONGEZEKA KWA VISINGIZIO: Mara nyingi mtu anapokuchoka huwa anakosa hamu ya kuongea, kuchat, kuonana, kula, hata kukaa na wewe. Usishangae sana mumeo kuanza kila akirudi nyumbani kukwambia "Anh nimeshiba", "Nimechelewa kurudi, kazi nyingi", au mpenzi wako "Baby sijaja mama alinituma sehemu ", "Dah mishe zinabana ndomana sijakutafuta".
.
5: KUTOKUJALI TENA: Hiki ndo kipindi ambacho unaongea na mkeo, yeye anakupa mgongo. Ule usile, utosheke chumbani usitosheke, ulale usilale, uumwe usiumwe, wala hana muda na wewe.
.
6: KUFA KWA UPENDO&MAHABA: Utaanza kuona mabadiliko, zile nakupenda, kusifiana, kucheza pamoja, kulishana, mabusu motomoto, kubebana, kudekezana, kutoka wote pamoja, kucheka pamoja, kula pamoja, mechi za kufa mtu, vyote utaona vinapungua kimoja baada ya kingine.
.
7: MABADILIKO KWENYE TENDO LA NDOA: Mara nyingi mtu anapoanza kujenga chuki dhidi yako, huwa anaanza kukosa hamu/hisia juu yako. Hivyo hata kama hana michepuko, huwa anakosa ile hamu ya kufanya na wewe tena. Lakini kama anayo michepuko, huwa anamaliza hamu zake huko huko, wewe unawekwa kando, au hata mkifanya inakuwa kama kajilazimisha kufanya, hivyo anaweza akaishia njiani kutokana na uchovu alionao baada ya kuhudumia michepuko, au kutokana na kukosa hamu ya kufanya na wewe.
.
Tutaendelea na uchambuzi. .......
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza