Skip to main content
UJUMBE MUHIMU KWA WANAUME.

Utamsikia mwanaume anajisifia kabisa “Mke wangu yeye hapendi hayo mambo, muelewa sana yule mwanamke, hivyo vitu anajinunulia mwenyewe, yeye alimradi chakula kiwepo mezani na watoto waende shule basi!”
Ndugu yangu labda kama umeoa Mbuzi na si hawa wanawake ninaowajua mimi. Hakuna mwanamke ambaye hapendi kudekezwa, hapendi umnunulie vizawadi, hapendi umtoe out siku moja moja, hapendi umsifie na kumsuprise kimapenzi mapenzi.
Wewe kuleta ugali mezani ni majukumu yako kama mwanaume, lakini kumtoa hata kula chips mtaani ni mapenzi, kumpelekea maua ni mapenzi. Kumpa hela ya kununua nguo ni majukumu, lakini kumnunulia nguo, ukamuambia ajaribishe, ukamsifia alivyopendeza ni ni mapenzi.
Utasikia mwanaume anasema “Mimi siwezi kuchagua nampa pesa achague mwenyewe..” Ndugu yangu raha ya zawadi ni kununuliwa na si kujinunulia. Ukimpa pesa akanunue maua yanakua maua ya mezani ila ukimnunulia wewe na kumpa yanageuka kuwa zawadi ya maua hata kama hayana harufu utaona anachekacheka na kuyanusa nusa…!
Ukimpa pesa akanunue chips mtaani inakuwa ni chakula ila ukimtoa sehemu mkaenda kukaa na akaagiza chips inakuwa ni mtoko ‘outing’ na atawasimulia na marafiki zake wote kuwa umlimtoa. “Au ulifikiri mkitoka out ndiyi anaenda kuagiza kuku wa mbinguni?”
Unajifanya hujui kuchagua, yaani hata kwenda dukani kununua dazeni za underwear na kumpelekea huwezi au hujui hata saizi ya kiuno chake! Ukimpa hela ya kununulia nguo anaweza akanunua hata kumi na zinakua nguo tu, lakini ukamletea nguo moja inageuka na kuwa zawadi na atawasimulia rafiki zake wote.
Badilika ndugu yangu, vitu vidogo vidogo ambavyo havigharimu chochote kwa mwanamke ndiyo mapenzi lakini vile vikubwa vinaitwa majukumu.  Mkeo hata anajifanya hapendi kwakuwa ashakusoma anaona humjali hivyo ili tu kulinda ndoa na asiumie hujifanya kutokupenda.
Lakini hata kama angekuwa Raisi bado angetamani umuite Baby, umsuprise na maua ya elfu mbili na hata kacheni kampoja kakuoshea. Narudia labda kama umeoa Mbuzi si wanawake hawa ambao ninawafahamu!


Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YANAYO KWAMISHA UFUGAJI

MAGWEIGA POULTRY INVESTMENT(wajasiriamali wa kuku na bidhaa zake) MAMBO YANAYOKWAMISHA WAFUGAJI WENGI.  Ufugaji ni rahisi ukitumia faida za mezani na kushuhudia watu wanafanya.  Hali hi inaweza ikawa tofauti ukianza wewe mwenyewe kwa vitendo.  Ni jambo gumu kiasi chake endapo mfugaji atapuza kanuni bora za Ufugaji.  Hapa mfugaji mpya anapaswa kujitathimini na kujipima kama anaweza kutoboa na kufikia matamanio yake kiufugaji.     Ufugaji ni kazi ngumu lakni imejawa na mafanikio kabambe na pia ni miongoni mwa furusa ambazo zipo wazi.  Ila vigezo na mashariti kuzingatiwa. kinacho kwamisha ufugaji kwa asilimia kubwa ni mambo yafuatayo . Mfugaji asipo yavalia njuga ataishia kwenye msongo wa mawazo na kujipa magonjwa ya moyo. Magweiga poultry investment 1. Magonjwa . Kipengele hiki kimekuwa changamoto kubwa sana kwa sisi wafugaji.  Yapo magonjwa changizwa  ambayo ni mfugaji mwenyewe anakubaliana na ugonjwa husika kutokea  ✔️ Typhoid...

KUWA NA MSIMAMO KWENYE MAISHA YAKO

Ulishawahi kujiuliza ni  kwanini watu wachache wanafanikiwa katika maisha huku wengi wakibakia masikini?  Ukweli ni kwamba sio kuwa wao wanasiri nyingi za kufanikiwa kuliko wewe bali ni misimamo thabiti waliojiwekea ili kuendana na ukuaji wa changamoto za maisha. Ni watu ambao wanafikiria vitu na mambo makubwa na kufanya vitu hivyo kwa msimamo bila kukubali kushindwa.  James William  (Harvard University ) aliwahi kusema kwamba " A human being can alter their lives by altering their attitude of mind" akiwa anamanisha kwamba binadamu yeyote anaweza kupunguza maisha yake kwa kupunguza musimamo wa fikira zake. Duniani kote utafiti unaonyesha kwamba rasirimali watu ndio nyenzo muhimu sana katika biashara yoyote yenye mulengo wa mafanikio.  Ila rasilimali hiyo ndio imekuwa ikipotea kila siku kutokana na watu kukoswa msimamo  (atttitude) Watu wanaweza kuwa asset kubwa sana katika maisha yako. Mafanikio yoyote hayapimwi kwa kipato ulichonacho bali pia ...

USIWE NA TAMAA KATIKA UFUGAJI.

  MADHARA YA TAMAA KATIKA UFUGAJI  Mfugaji yoyote ili aweze kuona faida ya ufugaji wake lazima aweke Tamaa pembeni.  Kuna utofauti kati ya Mfugaji mwenye Malengo na Mfugaji mwenye Tamaa.  Mfugaji mwenye Malengo hufanya muradi wake kwa uchache na kwa ufanisi, pia huweka ukomo wa kumiliki kuku kwa kiwango ambacho huweza kuwamudu na kumletea faida  Mfugaji mwenye Tamaa yeye kwake ukienda utakuta ana kuku 500 wa rika tofauti tofauti ambao hata kuwalisha ni mtihani kwake ila shida yake aonekane anamiliki kuku wengi japo faida yake ni 0%% Mfano : umeweka kuku 100 kroila  na umewakuza kwa shida hadi kufikia kutaga . Wanapoanza kutaga ni muda wa kuvuna mayai ili kurudisha garama zako.  Cha ajabu hapa utakuta Mfugaji anakurupuka kuingiza vifaranga wapya 200 kwa kutegemea hawa kuku 100 wahudumie vifaranga 200  hadi kufikia kutaga.   Pia hao kuku 100 wajiendeshe wao wenyewe kupitia mayai.  pia kuku 100 wahudumie familia. Ukweli ni kwamba itafi...