Skip to main content
UJUMBE MUHIMU KWA WANAUME.

Utamsikia mwanaume anajisifia kabisa “Mke wangu yeye hapendi hayo mambo, muelewa sana yule mwanamke, hivyo vitu anajinunulia mwenyewe, yeye alimradi chakula kiwepo mezani na watoto waende shule basi!”
Ndugu yangu labda kama umeoa Mbuzi na si hawa wanawake ninaowajua mimi. Hakuna mwanamke ambaye hapendi kudekezwa, hapendi umnunulie vizawadi, hapendi umtoe out siku moja moja, hapendi umsifie na kumsuprise kimapenzi mapenzi.
Wewe kuleta ugali mezani ni majukumu yako kama mwanaume, lakini kumtoa hata kula chips mtaani ni mapenzi, kumpelekea maua ni mapenzi. Kumpa hela ya kununua nguo ni majukumu, lakini kumnunulia nguo, ukamuambia ajaribishe, ukamsifia alivyopendeza ni ni mapenzi.
Utasikia mwanaume anasema “Mimi siwezi kuchagua nampa pesa achague mwenyewe..” Ndugu yangu raha ya zawadi ni kununuliwa na si kujinunulia. Ukimpa pesa akanunue maua yanakua maua ya mezani ila ukimnunulia wewe na kumpa yanageuka kuwa zawadi ya maua hata kama hayana harufu utaona anachekacheka na kuyanusa nusa…!
Ukimpa pesa akanunue chips mtaani inakuwa ni chakula ila ukimtoa sehemu mkaenda kukaa na akaagiza chips inakuwa ni mtoko ‘outing’ na atawasimulia na marafiki zake wote kuwa umlimtoa. “Au ulifikiri mkitoka out ndiyi anaenda kuagiza kuku wa mbinguni?”
Unajifanya hujui kuchagua, yaani hata kwenda dukani kununua dazeni za underwear na kumpelekea huwezi au hujui hata saizi ya kiuno chake! Ukimpa hela ya kununulia nguo anaweza akanunua hata kumi na zinakua nguo tu, lakini ukamletea nguo moja inageuka na kuwa zawadi na atawasimulia rafiki zake wote.
Badilika ndugu yangu, vitu vidogo vidogo ambavyo havigharimu chochote kwa mwanamke ndiyo mapenzi lakini vile vikubwa vinaitwa majukumu.  Mkeo hata anajifanya hapendi kwakuwa ashakusoma anaona humjali hivyo ili tu kulinda ndoa na asiumie hujifanya kutokupenda.
Lakini hata kama angekuwa Raisi bado angetamani umuite Baby, umsuprise na maua ya elfu mbili na hata kacheni kampoja kakuoshea. Narudia labda kama umeoa Mbuzi si wanawake hawa ambao ninawafahamu!


Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....