Skip to main content

Posts

Showing posts from November, 2018

TAMBUA HILI MWANAMKE KATIKA NDOA YAKO

Wewe ni mwanamke mkuu wa familia yako. Uwe na hekima na uweledi. Panga vizuri matumizi yako. Panga bajeti ya matumizi yako kwa njia ambayo haitasababisha hasara kwa utajiri na hekima yako. Usishindane na wengine na uwaonee wivu. Kama unaona nguo nzuri imevaliwa na mwanamke, au kama unavutiwa na fanicha na vyombo ambavyo umeviona kwenye nyumba ya rafiki, usimlazimishe mumeo kununua vitu kama hivyo ambavyo vinazidi uwezo wake wa kifedha na pengine atalazimika kukopa. Je, si vema zaidi kungoja hadi hapo ambapo hali ya kipato itaruhusu au itakapopatikana akiba ya ziada ya kuwezesha kununua vitu visivyo vya muhimu? Mara nyingi ni wale wanawake wajinga na wanaojipendelea ambao hushindwa, na kuwa wabadhirifu na kutaka kushindana. Wanawake wa aina hii huwalazimisha waume zao kuingia kwenye madeni na huchoshwa na kukasirishwa na kujaribu kuridhisha matakwa yao yasiyo weza kutoshelezwa. Wakati mwingine, ufumbuzi wa aina moja tu uliopo kwa wanaume wa kutatua matatizo haya ni uamuzi wa kumtaliki ...

UMUHIMU WA KUSOMA VITABU

Ni watu wachache sana ndiyo wanaopenda na wanafahamu umuhimu wa kusoma vitabu. Watu wengi hasa waafrika hawapendi kusoma vitabu ikiwa hakuna kinachowalazimisha kufanya hivyo kama vile mtihani, kazi, n.k. Kwa hakika kuna maarifa mengi yaliyofichwa kwenye vitabu; hii ndiyo sababu  husoma au hata kuandika vitabu. Ikiwa unataka kupata maarifa na kuboresha maisha yako kwa njia ya kusoma vitabu, basi fahamu faida 15 za kusoma vitabu. 1. Hukuongezea marifa mapya Lengo kubwa linalowafanya waandishi wa vitabu kuandika vitabu ni kuweka maarifa yao kwenye maandishi. Hivyo kwa kusoma vitabu unapata maarifa mbalimbali yaliyowekwa kwenye kitabu husika. Hivi leo kuna vitabu vinavyohusu takriban kila kitu; kwa hiyo maarifa yoyote unayoyahitaji unaweza kuyapata kwenye vitabu. 2. Hukuwezesha kufikiri kwa kina Kwa hakika vitabu huongeza sana uwezo wa kufikiri. Unaposoma vitabu unafahamu mambo ambayo yatakufanya ufikiri zaidi; mara nyingine kitabu kitakuacha na maswali ambayo yatak...

JINSI IMANI YA ELIMU INAVYO WATIA WATU UMASIKINI

Ukichunguza katika jamii, utabaini kuwa sehemu kubwa ya matajiri ni wale ambao wana elimu ndogo ama hawakusoma kabisa. Katika miji na maeneo yote; wenye majengo ya maana, wenye makampuni makubwa, wenye utitiri wa malori na mabasi, wenye maduka makubwa ni wale wa "darasa la saba” au wale ambao hawakuingia darasani kabisa. 📚 Wasomi wengi wana maisha ya kawaida yaani yale ya kiwango cha kubadilisha mboga, wakijitahidi sana wanaishia kujenga nyumba za kuishi 🏡 na 🚗 magari mawili ya kutembelea (tena kwa mikopo!). Wapo wasomi wengi tu wanaoishi kimasikini, kwa lugha ya kistaarabu tunasema wana maisha ya kuungaunga. Kiukweli idadi ya wasomi walio matajiri ni ndogo sana. Lakini Umasikini wa wasomi wengi umeanzia huko shuleni na vyuoni wanakopatia usomi wao. Madarasani kuna mambo mawili wanafundishwa wasomi ambayo ndio yanayowaroga. 1.Wameelimishwa na kuaminishwa kwamba yule anaepata maswali yote kwa usahihi ndio anaonekana amefaulu. Ukikosea unahesabika kuwa u mjinga na wenyewe...

MSAADA UTOKAO KWA MUNGU JUU NA ALIYE HAI

MIAKA 2,000 hivi iliyopita, Paulo, mwandikaji wa Biblia alimfafanua Yehova kuwa “Mungu anayetoa uvumilivu na faraja.” ( Waroma 15:5 ) Kwa kuwa Biblia inatuhakikishia kwamba Yehova habadiliki kadiri wakati unavyopita, tunaweza kuwa na hakika kwamba bado Mungu anawafariji wale wanaomtumikia. ( Yakobo 1:17 ) Kwa kweli, Biblia inafunua kwamba Yehova anawafariji kwa njia mbalimbali wale walio na uhitaji. Ni njia gani hizo? Mungu anawatia nguvu wale wanaomwomba msaada kupitia sala. Pia, Mungu anawachochea Wakristo wa kweli kuwafariji waamini wenzao. Na Yehova ameweka katika Neno lake, Biblia, masimulizi yenye kutia moyo ambayo yanawatia nguvu hasa wale wanaoomboleza kifo cha mtoto. Acheni tuchunguze aina hizo tatu za faraja, moja baada ya nyingine. “Yehova Mwenyewe Akasikia” Mfalme Daudi aliandika hivi kuhusu Muumba wetu, Yehova: “Mtegemeeni nyakati zote. Mimineni moyo wenu mbele zake. Mungu ni kimbilio letu.” ( Zaburi 62:8 ) Kwa nini Daudi alikuwa na uhakika huo katika Yehova? Daudi alia...

USICHUKULIE CHUKI KWA KILA MTU

Ikiwa jamii inayokuzunguka itajinua na kukuongelea wewe katika maeneo tofauti na mienendo tofauti , ni lazima uchukue nafasi ya kujitathimini upya na kufanya toba za kila wakati juu ya hayo. wanadamu wakati mwingine huwa na taarifa za ishara ya kuharibikiwa kwako pia  mungu huwatumia wao kukufikishia ujumbe juu ya kukutaka ubadilike na uendane na kile ambacho yeye alikusudia ufanye hapa duniani. sio kwamba kila mwanadamu nayekwandama kutokna na mienendo yako anakutakia mabaya bali wengine huwa na nia njema. hupaswi kuchukia badala yake unapaswa kujielimisha juu ya hayo na kuwatumia kama wajuzaji wako.          ...................................        

JIFUNZE HILO

Katika maisha yako usikubali kufumbia macho mambo madogo madogo ukiamini kwamba yanaweza kupata ufumbuzi siku yoyote.  Hasa unapokuwa kwenye mahusiano kati yako na mwenzi wako.  Ikumbukwe kwamba jinsi unavyozidi kufuga hali hiyo ndivyo unajiweka kwenye nafasi kubwa ya kushindwa huko mbeleni.  Penda kuwa mtu wa kumaliza vitu muda huohuo ili kuipa nafasi akili yako na nafsi yako kuhifadhi mambo mapya na makubwa kwenye Safari ya kuelekea kwenye kutimiza ndoto zako.  Ukiwa mtu wa kulimbikiza mambo siku zote lazima utavuruga hasa unapofikia wakati wa mamzi. Epuka sana kumuweka mwenzi wako kwenye mabano huku ukimtegea arudie kosa ili uyaunganishe na kuyafanyia kazi kwa pamoja. Hata hivyo asilimia kubwa ya watu huchukua matatizo hayo kuwa sehemu ya maisha yao kwa sababu ya kutoelewa hilo.  Tumia muda wako vizuri na uwekeze kwenye kujielimisha zaidi juu ya hayo.  Pia unapo fanya hivyo kwa upande mwingine unakuwa unatoa nafasi kubwa kwa shetani kujipenyeza na kuk...