Binti yoyote utambue kuwa kuna tofauti ya kuolewa na kujioa mwenyewe, sasa usiwe na haraka mpaka ukafikia hatua ya kuamua kujioa maana huko ndani Jasho litakutoka, Mungu Anaweza asikupe ndizi moja Leo lakini kesho akakupa mkungu mzima wa ndizi hivyo kikubwa ni kuwa na subira na imani kwa Mungu, mfano kuchangia mahari au kujilipia mahari sio jukumu lako, kuolewa na mtu asiye na Kazi au shughuli ya kufanya halafu weee ndio umhudumie kwa kuwa una kipato na umri unaenda na wenzio wameolewa Hilo pia hapana Hilo sio jukumu lako pia wewe ndio wa kuhudumiwa na kutunzwa pale msaada wako unapohitajika sawa ndio maana ukaitwa msaidizi na sio kichwa, kuolewa tu ilimradi na wewe umetoa gundu kuwa na mimi niliwahi Vaa shera kama wengine mnavyosema hata kama unajua kuwa mwanaume hakupendi ila una mimba yake na wazazi wamelazimisha ili usiwatie aibu Nyumbani wakati unajua kabisa ndoa yako itakuwa na mtikisiko mana mume hana upendo na wewe hivyo yajayo unayajua hilo pia sio kwakuwa kuna watu walipata mimba lakini baadaye wakaja kuolewa na mtu mwingine mwenye upendo hivyo sio Mwisho wa maisha , na vitu vingine utajiongeza, kuna mtu atakuwa kanielewa hapo, maana 2019 hiyo inakuja usiseme sikukuambia Japo vijana wengi wa mteremko hawataipenda hii najua ila ndio ukweli wenyewe huo
MAGWEIGA POULTRY INVESTMENT(wajasiriamali wa kuku na bidhaa zake) MAMBO YANAYOKWAMISHA WAFUGAJI WENGI. Ufugaji ni rahisi ukitumia faida za mezani na kushuhudia watu wanafanya. Hali hi inaweza ikawa tofauti ukianza wewe mwenyewe kwa vitendo. Ni jambo gumu kiasi chake endapo mfugaji atapuza kanuni bora za Ufugaji. Hapa mfugaji mpya anapaswa kujitathimini na kujipima kama anaweza kutoboa na kufikia matamanio yake kiufugaji. Ufugaji ni kazi ngumu lakni imejawa na mafanikio kabambe na pia ni miongoni mwa furusa ambazo zipo wazi. Ila vigezo na mashariti kuzingatiwa. kinacho kwamisha ufugaji kwa asilimia kubwa ni mambo yafuatayo . Mfugaji asipo yavalia njuga ataishia kwenye msongo wa mawazo na kujipa magonjwa ya moyo. Magweiga poultry investment 1. Magonjwa . Kipengele hiki kimekuwa changamoto kubwa sana kwa sisi wafugaji. Yapo magonjwa changizwa ambayo ni mfugaji mwenyewe anakubaliana na ugonjwa husika kutokea ✔️ Typhoid...
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza