Binti yoyote utambue kuwa kuna tofauti ya kuolewa na kujioa mwenyewe, sasa usiwe na haraka mpaka ukafikia hatua ya kuamua kujioa maana huko ndani Jasho litakutoka, Mungu Anaweza asikupe ndizi moja Leo lakini kesho akakupa mkungu mzima wa ndizi hivyo kikubwa ni kuwa na subira na imani kwa Mungu, mfano kuchangia mahari au kujilipia mahari sio jukumu lako, kuolewa na mtu asiye na Kazi au shughuli ya kufanya halafu weee ndio umhudumie kwa kuwa una kipato na umri unaenda na wenzio wameolewa Hilo pia hapana Hilo sio jukumu lako pia wewe ndio wa kuhudumiwa na kutunzwa pale msaada wako unapohitajika sawa ndio maana ukaitwa msaidizi na sio kichwa, kuolewa tu ilimradi na wewe umetoa gundu kuwa na mimi niliwahi Vaa shera kama wengine mnavyosema hata kama unajua kuwa mwanaume hakupendi ila una mimba yake na wazazi wamelazimisha ili usiwatie aibu Nyumbani wakati unajua kabisa ndoa yako itakuwa na mtikisiko mana mume hana upendo na wewe hivyo yajayo unayajua hilo pia sio kwakuwa kuna watu walipata mimba lakini baadaye wakaja kuolewa na mtu mwingine mwenye upendo hivyo sio Mwisho wa maisha , na vitu vingine utajiongeza, kuna mtu atakuwa kanielewa hapo, maana 2019 hiyo inakuja usiseme sikukuambia Japo vijana wengi wa mteremko hawataipenda hii najua ila ndio ukweli wenyewe huo
Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza – Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17 ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza