Imeandikwa na mwanamke ambaye ameachika kwa mume wake na sasa anaishi peke yake na kulea mtoto
Nimeandika kwenu ili muweze kuelewa kuwa wakati mwingine ni vema kuwathamini Wenza wetu.
Nina miaka 32, Mimi na mume wangu tulikuwa kwenye mahusiano kwa Muda wa miaka 6 na tulikuwa marafiki kabla hatujaoana, nilimsubiri mume wangu mpaka alipomaliza chuo, baadaye wazazi wakafahamiana na sisi tukafunga ndoa na sasa tuna mtoto wa miaka 7.mume wangu Alikuwa ni mtu wa kukasirika haraka lakini hayo yote yalianza baada ya mimi mwenyewe kutaka kumuonyesha kuwa hawezi kunitawala. Kila mara tulipogombana kidogo tu nilichukua mizigo yangu na kwenda kwetu kuelezea,dada yangu anachukua simu na kuanza kumpigia simu mume wangu na kumgombeza, na nilikuwa nikimtishia kuwa kama vipi nipe talaka yangu, huku Moyoni kiukweli simaanishi kweli kutaka talaka, nilikuwa naleta tu ufahari na kutaka kutoonekana nimeshindwa au Nina shida naye sana, siku moja kwa matendo yangu nilisababisha mpaka akanipiga sana na kunifungia nje, nikaenda kwetu kama kawaida na familia yangu wakampeleka polisi, na kila wakati ilikuwa inaonekana kama mimi ndio ninaonewa na kuteswa na mume wangu ila ukweli mimi ndio niliyekuwa namnyanyasa mume wangu kihisia.wakamkamata na kumuweka ndani na mimi nikaambwa sana na ndugu Zake kuwa nifute kesi aachiwe. Baadaye nikajifikiria kuwa mm ndio Nina makosa mume wangu hakuwa mgomvi kabisa nilimsukumia mume wangu ukutani mpaka akaanguka Chini na bado aliamka na kuomba msamaha. Nikafuta kesi na tukayamaliza, baada ya miezi 3 Nikafunga vilago vyangu na kuondoka tena sababu ya kitu kidogo tu ambacho tungeweza kukimaliza na kumuacha peke yake, baada ya siku 2 nilipata simu kuwa mume wangu yupo hospitali, familia yangu ikaniambia kuwa nisiende kumuona itaonekana kama nambembelezaa na dada zangu wakahisi anajifanyisha ugonjwa, na wakati wote huo watu walikuwa wananionea Huruma kama vile ninateseka kwenye ndoa yangu, alikaa hospitali wiki nzima na baada ya kutoka nilipokea barua ya kutaka kuachana, nilitaka kukata ila sababu ya kiburi changu kitakatifu nikajua atabadili mawazo tu na kunibembeleza, nikampigia simu na kusema bora tuachane maana hata mimi naona kama niko Jehanamu.
Tulipokutana mahakamani nikataka kumkomesha nikaiambia mahakama kuwa nataka tugawane kila kitu tulichochuma wote na kwa mshangao wa Ajabu na yeye akaiambia mahakama kuwa chochote ninachotaka nipewe tu anachotaka yeye ni kuachana tu . tuliachana mwaka 2009 mwezi wa 6, sasa hivi mume wangu ameoa mwanamke mwingine na mimi nipo tu nimeharibikiwa na ndugu zangu wamenigeuka na kunicheka na sasa ninaishi kwa kutegemea hela za mtoto za matumizi anazopewa mwanangu na baba yake, najua nimepoteza ndoa yangu mwenyewe,
Nipo hapa kukuambia wewe mwanamke uliyeolewa kuwa makini sana na ushauri unaopewa, usiruhusu ndugu au wazazi hata marafiki waingilie ndoa yako, sasa hivi hata wadogo zangu ndio Wanaheshimika zaidi kuliko mimi, wote waliokuwa wananipa moyo niachane na mume wangu walikuwa wananijaza upepo kinafiki na sasa Wamenikimbia na kuniacha peke yangu naangaika.
Share ujumbe huu kama umekubariki ili kunusuru ndoa Zingine, Mara nyingine huwa sio makosa ya mwanaume bali ni ujinga wetu na kiburi..hivyo kuna cha kujifunza kama mwanamke
Nimeandika kwenu ili muweze kuelewa kuwa wakati mwingine ni vema kuwathamini Wenza wetu.
Nina miaka 32, Mimi na mume wangu tulikuwa kwenye mahusiano kwa Muda wa miaka 6 na tulikuwa marafiki kabla hatujaoana, nilimsubiri mume wangu mpaka alipomaliza chuo, baadaye wazazi wakafahamiana na sisi tukafunga ndoa na sasa tuna mtoto wa miaka 7.mume wangu Alikuwa ni mtu wa kukasirika haraka lakini hayo yote yalianza baada ya mimi mwenyewe kutaka kumuonyesha kuwa hawezi kunitawala. Kila mara tulipogombana kidogo tu nilichukua mizigo yangu na kwenda kwetu kuelezea,dada yangu anachukua simu na kuanza kumpigia simu mume wangu na kumgombeza, na nilikuwa nikimtishia kuwa kama vipi nipe talaka yangu, huku Moyoni kiukweli simaanishi kweli kutaka talaka, nilikuwa naleta tu ufahari na kutaka kutoonekana nimeshindwa au Nina shida naye sana, siku moja kwa matendo yangu nilisababisha mpaka akanipiga sana na kunifungia nje, nikaenda kwetu kama kawaida na familia yangu wakampeleka polisi, na kila wakati ilikuwa inaonekana kama mimi ndio ninaonewa na kuteswa na mume wangu ila ukweli mimi ndio niliyekuwa namnyanyasa mume wangu kihisia.wakamkamata na kumuweka ndani na mimi nikaambwa sana na ndugu Zake kuwa nifute kesi aachiwe. Baadaye nikajifikiria kuwa mm ndio Nina makosa mume wangu hakuwa mgomvi kabisa nilimsukumia mume wangu ukutani mpaka akaanguka Chini na bado aliamka na kuomba msamaha. Nikafuta kesi na tukayamaliza, baada ya miezi 3 Nikafunga vilago vyangu na kuondoka tena sababu ya kitu kidogo tu ambacho tungeweza kukimaliza na kumuacha peke yake, baada ya siku 2 nilipata simu kuwa mume wangu yupo hospitali, familia yangu ikaniambia kuwa nisiende kumuona itaonekana kama nambembelezaa na dada zangu wakahisi anajifanyisha ugonjwa, na wakati wote huo watu walikuwa wananionea Huruma kama vile ninateseka kwenye ndoa yangu, alikaa hospitali wiki nzima na baada ya kutoka nilipokea barua ya kutaka kuachana, nilitaka kukata ila sababu ya kiburi changu kitakatifu nikajua atabadili mawazo tu na kunibembeleza, nikampigia simu na kusema bora tuachane maana hata mimi naona kama niko Jehanamu.
Tulipokutana mahakamani nikataka kumkomesha nikaiambia mahakama kuwa nataka tugawane kila kitu tulichochuma wote na kwa mshangao wa Ajabu na yeye akaiambia mahakama kuwa chochote ninachotaka nipewe tu anachotaka yeye ni kuachana tu . tuliachana mwaka 2009 mwezi wa 6, sasa hivi mume wangu ameoa mwanamke mwingine na mimi nipo tu nimeharibikiwa na ndugu zangu wamenigeuka na kunicheka na sasa ninaishi kwa kutegemea hela za mtoto za matumizi anazopewa mwanangu na baba yake, najua nimepoteza ndoa yangu mwenyewe,
Nipo hapa kukuambia wewe mwanamke uliyeolewa kuwa makini sana na ushauri unaopewa, usiruhusu ndugu au wazazi hata marafiki waingilie ndoa yako, sasa hivi hata wadogo zangu ndio Wanaheshimika zaidi kuliko mimi, wote waliokuwa wananipa moyo niachane na mume wangu walikuwa wananijaza upepo kinafiki na sasa Wamenikimbia na kuniacha peke yangu naangaika.
Share ujumbe huu kama umekubariki ili kunusuru ndoa Zingine, Mara nyingine huwa sio makosa ya mwanaume bali ni ujinga wetu na kiburi..hivyo kuna cha kujifunza kama mwanamke
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza