Skip to main content

USHAURI WA WADAU WA JUKWAA LETU LA TUJENGANE MEDIA

Imeandikwa na mwanamke ambaye ameachika kwa mume wake na sasa anaishi peke yake na kulea mtoto

Nimeandika kwenu  ili muweze kuelewa kuwa wakati mwingine ni vema kuwathamini Wenza wetu.

Nina miaka 32, Mimi na mume wangu tulikuwa kwenye mahusiano kwa Muda wa miaka 6 na tulikuwa marafiki kabla hatujaoana, nilimsubiri mume wangu mpaka alipomaliza chuo, baadaye wazazi wakafahamiana na sisi tukafunga  ndoa na sasa tuna mtoto wa miaka 7.mume wangu Alikuwa ni mtu wa kukasirika haraka  lakini hayo yote yalianza baada ya mimi mwenyewe kutaka kumuonyesha kuwa hawezi kunitawala. Kila mara tulipogombana kidogo tu nilichukua mizigo yangu na kwenda kwetu kuelezea,dada yangu anachukua simu na kuanza kumpigia simu mume wangu na kumgombeza, na nilikuwa nikimtishia kuwa kama vipi nipe talaka yangu, huku Moyoni kiukweli simaanishi kweli kutaka talaka, nilikuwa naleta tu ufahari na kutaka kutoonekana nimeshindwa au Nina shida naye sana, siku moja kwa matendo yangu nilisababisha mpaka akanipiga sana na kunifungia nje, nikaenda kwetu kama kawaida na familia yangu wakampeleka polisi, na kila wakati ilikuwa inaonekana kama  mimi ndio ninaonewa na kuteswa na mume wangu ila ukweli mimi ndio niliyekuwa namnyanyasa mume wangu kihisia.wakamkamata na kumuweka ndani na mimi nikaambwa sana na ndugu Zake kuwa nifute kesi aachiwe. Baadaye nikajifikiria kuwa mm ndio Nina makosa mume wangu hakuwa mgomvi kabisa nilimsukumia mume wangu ukutani mpaka akaanguka Chini na bado aliamka na kuomba msamaha. Nikafuta kesi na tukayamaliza,  baada ya miezi 3 Nikafunga vilago vyangu na kuondoka tena sababu ya kitu kidogo tu ambacho tungeweza kukimaliza na kumuacha peke yake, baada ya siku 2 nilipata simu kuwa mume wangu yupo hospitali, familia yangu ikaniambia kuwa nisiende kumuona itaonekana kama nambembelezaa na dada zangu wakahisi anajifanyisha ugonjwa, na wakati wote huo watu walikuwa wananionea Huruma kama vile ninateseka kwenye ndoa yangu, alikaa hospitali wiki nzima na baada ya kutoka nilipokea  barua ya kutaka kuachana, nilitaka kukata ila sababu ya kiburi changu kitakatifu nikajua  atabadili mawazo tu na kunibembeleza, nikampigia simu na kusema bora tuachane maana hata mimi naona kama niko Jehanamu.

Tulipokutana mahakamani nikataka kumkomesha nikaiambia mahakama kuwa nataka tugawane kila kitu tulichochuma wote na kwa mshangao wa Ajabu na yeye akaiambia mahakama kuwa chochote ninachotaka nipewe tu anachotaka yeye ni kuachana tu . tuliachana mwaka 2009 mwezi wa 6,  sasa hivi mume wangu ameoa mwanamke mwingine na mimi nipo tu nimeharibikiwa na ndugu zangu wamenigeuka na kunicheka na sasa  ninaishi kwa kutegemea hela za mtoto za matumizi anazopewa mwanangu na baba yake, najua nimepoteza ndoa yangu mwenyewe,

 Nipo hapa kukuambia wewe mwanamke uliyeolewa kuwa makini sana na ushauri unaopewa,  usiruhusu  ndugu au wazazi  hata marafiki  waingilie ndoa yako, sasa hivi hata wadogo zangu ndio Wanaheshimika zaidi kuliko mimi, wote waliokuwa wananipa moyo niachane na mume wangu walikuwa wananijaza upepo kinafiki na sasa Wamenikimbia na kuniacha peke yangu naangaika.

Share ujumbe huu kama umekubariki ili kunusuru ndoa Zingine, Mara nyingine huwa sio makosa ya mwanaume bali ni ujinga wetu na kiburi..hivyo kuna cha kujifunza kama mwanamke

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....