MPANGILIO SAHIHI WA CHANJO KWA VIFARANGA CHOTARA NA KIENYEJI
.............................................
Vifaranga ili wakuwe vyema na kusitawi ni lazima wazingatiwe katika chanjo na chakula bora.
Chanjo humsaidia kifaranga kujikinga na magonjwa hatari ambayo hayana dawa kama vile mdondo, mahebe , Gumboro na ugonjwa wa ndui.
Haya ni magonjwa ambayo yakitokea Katika shamba huweza kuleta vifo na hasara kubwa kwa mfugaji.
Magonjwa haya huwa yana chanjo na sio dawa hivyo mfugaji anapaswa kuzingatia ratiba za chanjo kwa usahihi
*RATIBA ZA CHANJO*
SIKU 1. MAREK'S
SIKU 7. NEWCASTLE
SIKU 14. GUMBORO
SIKU 21 NEWCASTLE
SIKU 28 GUMBORO
SIKU 35 NDUI
Katika hizo chanjo , chanjo mbili hutolewa kwenye bawa ambazo ni chanjo ya marekes na chanjo ya ndui.
Chanjo zilizobakia huchanganywa katika maji Kwa maelekezo sahihi ya kitaalamu.
✔️Chanjo hutakiwa kuhifadhiwa Katika sehemu ya ubaridi na kusiwe na changamoto za ukatikaji wa umeme kwa Muda mrefu zaidi.
✔️Chanjo inatakiwa ikaguliwe tarehe ya kuisha matumizi ili kuwepuka vifo kwa kuku au vifaranga.
✔️Chanjo ifunguliwe vizuri kulingana na maelekezo ya kitaalamu . Epuka chanjo kukutana na mionzi ya jua Kwa muda mrefu kabla ya kuchanganywa na maji.
✔️ chanjo nyingi hutumika kwa muda wa masaa 2 baada ya hapo inatikwa kutupwa mbali na mazingira ya kuku.
✔️ Chanjo zinunuliwe kutoka Kwa wasambazaji wa kuaminika na wenye historia nzuri Katika uuzaji wa madawa na chanjo. Kuna badhi ya wasambazaji hawazingatii sheria za utunzaji wa chanjo na kusababisha hasara kwa wafugaji.
✔️ Kuku wagonjwa / vifaranga wasipewe chanjo badala yake watibiwe kwanza wapone kisha ndio wapewe chanjo.
✔️ chunguza vifaranga kwa makini siku 3 kabla ya chanjo ili kubaini kama kuna ugonjwa wowote.
✔️ vifaranga wasipewe chanjo wakati wa Jua kali. Inapendekezwa asubhi /jioni.
✔️ chanjo ya Newcastle irudiwe kila baada ya miezi 3 . Hakikisha unaandika tarehe uliowapa chanjo na siku ya kurdia. Hi itakusaidia kutovukisha chanjo kwa muda mrefu.
By Mqagweiga
Wasiliana nami kwa uhitaji wa huduma za vifaranga, ushauri, mayai, kuku, ujenzi wa mabanda bora kupitia namba
📞 +255757472165
📞+256786155188
E-mail bahatichacha698@gmailcom
Niwatakie ufugaji mwema
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza