Skip to main content

UPANGILIO WA CHANJO KWA VIFRANGA.

MPANGILIO SAHIHI WA CHANJO KWA VIFARANGA CHOTARA NA KIENYEJI
.............................................
Vifaranga ili wakuwe vyema na kusitawi ni lazima wazingatiwe katika chanjo na chakula bora.  
Chanjo humsaidia kifaranga kujikinga na magonjwa hatari ambayo hayana dawa kama vile mdondo,  mahebe  ,  Gumboro na ugonjwa wa ndui. 
Haya ni magonjwa ambayo yakitokea Katika shamba huweza kuleta vifo na hasara kubwa kwa mfugaji.  
Magonjwa haya huwa yana chanjo na sio dawa hivyo mfugaji anapaswa kuzingatia ratiba za chanjo kwa usahihi 
   *RATIBA ZA CHANJO* 

SIKU 1.    MAREK'S
SIKU 7.    NEWCASTLE
SIKU 14.    GUMBORO
SIKU 21   NEWCASTLE
SIKU 28   GUMBORO
SIKU 35     NDUI

Katika hizo chanjo , chanjo mbili hutolewa kwenye bawa ambazo ni chanjo ya marekes  na  chanjo ya ndui. 
Chanjo zilizobakia huchanganywa katika maji Kwa maelekezo sahihi ya kitaalamu.  
✔️Chanjo hutakiwa kuhifadhiwa Katika sehemu ya ubaridi na kusiwe na changamoto za ukatikaji wa umeme kwa Muda mrefu zaidi.  
✔️Chanjo inatakiwa ikaguliwe tarehe ya kuisha matumizi ili kuwepuka vifo kwa kuku au vifaranga.  
✔️Chanjo ifunguliwe vizuri kulingana na maelekezo ya kitaalamu . Epuka chanjo kukutana na mionzi ya jua Kwa muda mrefu kabla ya kuchanganywa na maji. 
✔️ chanjo nyingi hutumika kwa muda wa masaa 2 baada ya hapo inatikwa kutupwa mbali na mazingira ya kuku. 
✔️ Chanjo zinunuliwe kutoka Kwa wasambazaji wa kuaminika na wenye historia nzuri Katika uuzaji wa madawa na chanjo.  Kuna badhi ya wasambazaji hawazingatii sheria za utunzaji wa chanjo na kusababisha hasara kwa wafugaji. 
✔️ Kuku wagonjwa / vifaranga wasipewe chanjo badala yake watibiwe kwanza wapone kisha ndio wapewe chanjo. 
✔️ chunguza vifaranga kwa makini siku 3 kabla ya chanjo ili kubaini kama kuna ugonjwa wowote. 
✔️ vifaranga wasipewe chanjo wakati wa Jua kali.  Inapendekezwa asubhi /jioni. 
✔️ chanjo ya Newcastle irudiwe kila baada ya miezi 3 . Hakikisha unaandika tarehe uliowapa chanjo na siku ya kurdia.  Hi itakusaidia kutovukisha chanjo kwa muda mrefu.  
   By Mqagweiga
Wasiliana nami kwa uhitaji wa huduma za vifaranga,  ushauri,  mayai,  kuku,  ujenzi wa mabanda bora kupitia namba 
📞 +255757472165
📞+256786155188
E-mail bahatichacha698@gmailcom
Niwatakie ufugaji mwema

Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....