Skip to main content

USIMAMIZI WA KUKU WANAO TAGA.

 SABABU ZA KUJIENDESHA KIHASARA KATIKA UFUGAJI

Ufugaji ili ukuletee matokeo chanya inakutaka mfugaji utumie akili nyingi na mbinu sitahiki . Kuliko matumizi mengi ya pesa akili kidogo  ( maarifa )

Nimewahi kusema huko nyuma Kwamba kabla hujaweka pesa zako kwenye tasinia ya ufugaji inakuhitaji kwanza uwekeze kwenye upatikanaji wa Elimu sahihi kuhusu ufugaji.  Kinyume cha hapo ni kuhatarisha mtaji wako.

Wapo watu wanaingia kwenye tasinia hi ya ufugaji kwa sababu wanapesa.  Ukweli usiopingika ni kwamba pesa haiwezi kuzuia kuku kufa isipokuwa maarifa sahihi ya ufugaji ndio yatakusaidia kujua 👇

✔️ Anaumwa nini 

✔️Atumie dawa gani 

✔️Kwa nini Anaumwa 

✔️ dozi sahihi kwa ugonjwa alionao 

✔️Ataweza kupona? 

✔️Anaweza kuambukiza wengine 

✔️Ni magonjwa yatokanayo na ukosefu wa chanjo au mazingira wanayoishi? ?

Ukisema unafuga kwa sababu unapesa itakusaidia kuzuia magonjwa kwa kununua madawa sio kweli kwa sababu kuna kipindi inafikia kuku wanagoma dawa zote za ugonjwa husika.  Mwisho wa siku itabidi wafe kisha kupata hasara.  Tafuta maarifa sahihi kabla ya kuingia huku

Hebu Twende kwenye maada lengwa kuhusu sababu zinazopelekea mfugaji kujiendesha kihasara Bila kupata faida.  Wapo wafugaji wanafurahi kuwa na kuku wengi kwa maana ya Namba Lakini hawampi faida sitahiki 

Kuchakachua chakula.....  hi hupelekea kuku kutaga chini ya kiwango na kusababisha mfugaji kupata mayai ambayo yanatosha kurudisha garama za chakula kwa siku au kwa wiki.   Muda mwingine hata kuku kushindwa kujirisha wenyewe na kupelekea mfugaji kuchukua pesa binafsi kwajili ya kulisha kuku. 

Kuku anapoanza kutaga inabidi mfugaji kuwa makini kuona kama kuku wako wanakupa faida.  

 Nitajuaje napata faida? ???

Hesabu za Kujua kama unajiendesha kihasara unaweza kubaini kupitia kiwango cha makusanyo ya mayai kwa wiki Kisha unatoa garama za chakula na mahitaji yanayo wahusu kuku. 

 Mfano

Una kuku 100 matetea  na kwa siku unapata trey 3 kwa maana asilimia 90.

Kwahiyo ni 3 ×12000=36000/= kwa siku.  

Kwa wiki ni 36000×7= 252,000/= kwa wiki 

Baada ya kupata hiyo pesa unatoa garama ya chakula kwa wiki husika.  Kinachobaki ndio faida yako wewe kwa wiki.  

By experience kuku 100 wanaotaga inatakiwa watumie 87.5kg kwa wiki . Hapa sitaweza kutoa total kwa sababu garama zipo tofauti kulingana na Eneo alipo mfugaji.  Ukiona kwa wiki nzima wanarudisha pesa yao ya chakula unapaswa kujua kwamba unawahudumia kuku ili waendelee kuwepo nyumbani. 

Kutobaini magonjwa kwa wakati.  Hi ni changamoto kubwa kwa sababu itakupelekea kuku washuke kiutagaji au kuacha kabisa kwa muda huku wewe ukitumia garama binafisi kukabiliana na tatizo. Hapa kuna garama mbili madawa +chakula na baada ya kupona itabidi mfugaji uingie mfukoni sana kuwarejesha kwenye hali yao ya awali.  Njia rahisi hapa ni kutumia muda wako  vyema kukagua kuku kabla ugonjwa haujafikia hali mbaya. 

 Matumizi ya dawa yasio sahihi kulingana na shughuli anayofanya kuku au rika.  Kuku anayetaga lazima apewe dawa ambazo hazitaathiri mfumo wake wa utagaji.  Hapa inatakiwa kushaurina na watalamu husika.  Endapo dawa zitatumika Bila kuzingatia utaratibu sahihi ni lazima utagaji ushuke na kujikuta unajiendesha kihasara. 

 Mabanda kuwa machafu.  Hi itakuletea magonjwa mara kwa mara na kujikuta kuku wanaishi kwa madawa kila siku.  

By Magweiga

📞+255757472165

📞+255786155188

Tutaendelea kuangazia somo hili kwa upana hapo kesho Mungu akitujalia uhaI.  :"

Karibu kwa uhitaji wa vifaranga wa kroila wa siku kwa shilingi 1500/=Vifaranga Hawa hupatikana kila wiki .


Comments

Popular posts from this blog

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA UCHUMBA

Yafuatayo ni mambo ya msingi kufanya katika kipindi cha uchumba; Jambo la kwanza –    Mruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana wa uchumba wenu 2Wakorinto 3:17  ‘Basi Bwana’ ndiye Roho; na alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru’. Kumbuka Roho Mtakatifu ni msaidizi. Hivyo basi ni vema kumtumia vema hasa katika nyanja hii ya mahusiano katika kipindi hiki cha uchumba. Ni Roho Mtakatifu pekee mwenye uwezo wa kukujulisha mambo na siri nyingi kuhusu mchumba wako hata kama yeye hataki kukueleza. Ukimruhusu Roho Mtakatifu afanyike Bwana, yeye atakuongoza katIka kufanya maombi yanayolenga maeneo ya msingi juu ya huyo mwenzako. Kila mtu ameumbwa pamoja na mapungufu fulani au kwa lugha nyingine mapungufu/ udhaifu (weakness) ni sehemu ya maisha ya mwanadamu. Roho Mtakatifu anapokuwa Bwana wa mahusiano yako yeye atakusaidia kuona madhaifu au mapungufu ya mwenzako kama kitu cha wewe kujivunia(Strength) kwa maana ya kuona udhaifu wa mwenzako kama kitu chema na si kibaya. Kum...

VITU VYA MSINGI VINAVYOWEZA KUKUSAIDIA KUDUMISHA UPENDO KATIKA MAHUSIANO

Kuna nukuu inayosema “Uhusiano mzuri hautokei tu peke yake bali huchukua muda, uvumilivu, na watu wawili ambao kikweli wanataka kuwa pamoja.” Japo inasemwa kuwa mapenzi hayana njia moja ya kufuatwa lakini kuna vitu ambavyo vinajulikana kuchangia katika kuboresha mahusiano baina ya wapenzi. Mahusiano ya mapenzi yenye kudumu ni sharti yapandwe katika udongo wenye rutuba kama ulivyo mmea, yatahitaji maji ya kumwagilia na mbolea ya kukuzia.  Na zaidi ya yote yanahitaji muda wa kukua kabla matunda kuonekana. 1. Uaminifu Kumwamini mwenza wako ni jambo la msingi sana katika kudumisha mahusiano. Usimshuku mpenzi wako kuwa si muaminifu bila ushahidi wowote. Kushukiwa kukosa uaminifu pasipo ukweli inasononesha sana na kumkosesha raha mpenzi wako. Imesemwa na wanafalsafa wa mawazo ya binadamu kuwa “Unachofikiri na kuamini kinatokea” hivyo unashauriwa kutofikiri vibaya juu ya mpenzi wako kwani haileti afya katika mahusiano. Hali kadhalika na wewe uwe mwaminifu na mwenye kusema kweli...

ZINGATIA HAYA UNAPOKUWA MBALI NA MWENZI WAKO

KAMA UKO MBALI NA MPENZI WAKO ZINGATIA HAYA Kama unaishi mbali na mpenzi wako kwanza kabisa unatakiwa kukubali kua mko mbali, huwezi na wala hutakiwi kucontrol kile anachokifanya kule, acha kufuatilia anafanya nini huko, yuko na nani na mambo kama hayo, kwa kfuupi wivu weka pembeni kwani ukiendekeza utachanganyikiwa. Kuna mambo mengi atayafanya mazuri na mabaya lakini kama hakuonyeshei basi huna haja ya kuyafukunyua. Jambo la pili ni mawasiliano haya ni muhimu na anapokupigia simu au unapompigia tumieni muda wenu vizuri kwa kuongelea kuhusu mapenzi na si kila siku “Mbona hukupokea simu yangu? Mbona nilikuona online hukujibu SMS zangu? Kulalamika sijui nimesikia hivi? Nimesikia vile!” Atakuvumilia kwa muda kisha itaboa na atakua anakwepa kuzungumza nawe na mwisho mapenzi yatakufa. Hata kama mnaongea dakika tano zifanyeni ziwe tamu zihusu mapenzi na si kuzozana mpaka mtu akitaka kupiga simu anawaza hivi nikiongea naye si kelele tu, hakuna mtu anapenda kupigia simu mtu aliyenuna....