SABABU ZA KUJIENDESHA KIHASARA KATIKA UFUGAJI
Ufugaji ili ukuletee matokeo chanya inakutaka mfugaji utumie akili nyingi na mbinu sitahiki . Kuliko matumizi mengi ya pesa akili kidogo ( maarifa )
Nimewahi kusema huko nyuma Kwamba kabla hujaweka pesa zako kwenye tasinia ya ufugaji inakuhitaji kwanza uwekeze kwenye upatikanaji wa Elimu sahihi kuhusu ufugaji. Kinyume cha hapo ni kuhatarisha mtaji wako.
Wapo watu wanaingia kwenye tasinia hi ya ufugaji kwa sababu wanapesa. Ukweli usiopingika ni kwamba pesa haiwezi kuzuia kuku kufa isipokuwa maarifa sahihi ya ufugaji ndio yatakusaidia kujua 👇
✔️ Anaumwa nini
✔️Atumie dawa gani
✔️Kwa nini Anaumwa
✔️ dozi sahihi kwa ugonjwa alionao
✔️Ataweza kupona?
✔️Anaweza kuambukiza wengine
✔️Ni magonjwa yatokanayo na ukosefu wa chanjo au mazingira wanayoishi? ?
Ukisema unafuga kwa sababu unapesa itakusaidia kuzuia magonjwa kwa kununua madawa sio kweli kwa sababu kuna kipindi inafikia kuku wanagoma dawa zote za ugonjwa husika. Mwisho wa siku itabidi wafe kisha kupata hasara. Tafuta maarifa sahihi kabla ya kuingia huku
Hebu Twende kwenye maada lengwa kuhusu sababu zinazopelekea mfugaji kujiendesha kihasara Bila kupata faida. Wapo wafugaji wanafurahi kuwa na kuku wengi kwa maana ya Namba Lakini hawampi faida sitahiki
Kuchakachua chakula..... hi hupelekea kuku kutaga chini ya kiwango na kusababisha mfugaji kupata mayai ambayo yanatosha kurudisha garama za chakula kwa siku au kwa wiki. Muda mwingine hata kuku kushindwa kujirisha wenyewe na kupelekea mfugaji kuchukua pesa binafsi kwajili ya kulisha kuku.
Kuku anapoanza kutaga inabidi mfugaji kuwa makini kuona kama kuku wako wanakupa faida.
Nitajuaje napata faida? ???
Hesabu za Kujua kama unajiendesha kihasara unaweza kubaini kupitia kiwango cha makusanyo ya mayai kwa wiki Kisha unatoa garama za chakula na mahitaji yanayo wahusu kuku.
Mfano
Una kuku 100 matetea na kwa siku unapata trey 3 kwa maana asilimia 90.
Kwahiyo ni 3 ×12000=36000/= kwa siku.
Kwa wiki ni 36000×7= 252,000/= kwa wiki
Baada ya kupata hiyo pesa unatoa garama ya chakula kwa wiki husika. Kinachobaki ndio faida yako wewe kwa wiki.
By experience kuku 100 wanaotaga inatakiwa watumie 87.5kg kwa wiki . Hapa sitaweza kutoa total kwa sababu garama zipo tofauti kulingana na Eneo alipo mfugaji. Ukiona kwa wiki nzima wanarudisha pesa yao ya chakula unapaswa kujua kwamba unawahudumia kuku ili waendelee kuwepo nyumbani.
Kutobaini magonjwa kwa wakati. Hi ni changamoto kubwa kwa sababu itakupelekea kuku washuke kiutagaji au kuacha kabisa kwa muda huku wewe ukitumia garama binafisi kukabiliana na tatizo. Hapa kuna garama mbili madawa +chakula na baada ya kupona itabidi mfugaji uingie mfukoni sana kuwarejesha kwenye hali yao ya awali. Njia rahisi hapa ni kutumia muda wako vyema kukagua kuku kabla ugonjwa haujafikia hali mbaya.
Matumizi ya dawa yasio sahihi kulingana na shughuli anayofanya kuku au rika. Kuku anayetaga lazima apewe dawa ambazo hazitaathiri mfumo wake wa utagaji. Hapa inatakiwa kushaurina na watalamu husika. Endapo dawa zitatumika Bila kuzingatia utaratibu sahihi ni lazima utagaji ushuke na kujikuta unajiendesha kihasara.
Mabanda kuwa machafu. Hi itakuletea magonjwa mara kwa mara na kujikuta kuku wanaishi kwa madawa kila siku.
By Magweiga
📞+255757472165
📞+255786155188
Tutaendelea kuangazia somo hili kwa upana hapo kesho Mungu akitujalia uhaI. :"
Karibu kwa uhitaji wa vifaranga wa kroila wa siku kwa shilingi 1500/=Vifaranga Hawa hupatikana kila wiki .
Comments
Post a Comment
asante kwa kuichagua tujengane media kuwa sehemu yako ya kujifunza