MAGWEIGA POULTRY INVESTMENT(wajasiriamali wa kuku na bidhaa zake) MAMBO YANAYOKWAMISHA WAFUGAJI WENGI. Ufugaji ni rahisi ukitumia faida za mezani na kushuhudia watu wanafanya. Hali hi inaweza ikawa tofauti ukianza wewe mwenyewe kwa vitendo. Ni jambo gumu kiasi chake endapo mfugaji atapuza kanuni bora za Ufugaji. Hapa mfugaji mpya anapaswa kujitathimini na kujipima kama anaweza kutoboa na kufikia matamanio yake kiufugaji. Ufugaji ni kazi ngumu lakni imejawa na mafanikio kabambe na pia ni miongoni mwa furusa ambazo zipo wazi. Ila vigezo na mashariti kuzingatiwa. kinacho kwamisha ufugaji kwa asilimia kubwa ni mambo yafuatayo . Mfugaji asipo yavalia njuga ataishia kwenye msongo wa mawazo na kujipa magonjwa ya moyo. Magweiga poultry investment 1. Magonjwa . Kipengele hiki kimekuwa changamoto kubwa sana kwa sisi wafugaji. Yapo magonjwa changizwa ambayo ni mfugaji mwenyewe anakubaliana na ugonjwa husika kutokea ✔️ Typhoid...
MADHARA YA TAMAA KATIKA UFUGAJI Mfugaji yoyote ili aweze kuona faida ya ufugaji wake lazima aweke Tamaa pembeni. Kuna utofauti kati ya Mfugaji mwenye Malengo na Mfugaji mwenye Tamaa. Mfugaji mwenye Malengo hufanya muradi wake kwa uchache na kwa ufanisi, pia huweka ukomo wa kumiliki kuku kwa kiwango ambacho huweza kuwamudu na kumletea faida Mfugaji mwenye Tamaa yeye kwake ukienda utakuta ana kuku 500 wa rika tofauti tofauti ambao hata kuwalisha ni mtihani kwake ila shida yake aonekane anamiliki kuku wengi japo faida yake ni 0%% Mfano : umeweka kuku 100 kroila na umewakuza kwa shida hadi kufikia kutaga . Wanapoanza kutaga ni muda wa kuvuna mayai ili kurudisha garama zako. Cha ajabu hapa utakuta Mfugaji anakurupuka kuingiza vifaranga wapya 200 kwa kutegemea hawa kuku 100 wahudumie vifaranga 200 hadi kufikia kutaga. Pia hao kuku 100 wajiendeshe wao wenyewe kupitia mayai. pia kuku 100 wahudumie familia. Ukweli ni kwamba itafi...